• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MOROGORO AWABANA WAKURUGENZI MADENI YA POSI.

Posted on: March 30th, 2024

RC MOROGORO AWABANA WAKURUGENZI MADENI YA POSI


Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amewaagiza wakurugenzi wa Halmashauri za Mkoa huo kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria watumishi wa Serikali ambao ni wadaiwa sugu wa fedha za ndani wanazokusanya kwa kutumia mashine za POSI ili kupunguza ama kukomesha kabisa tabia hiyo.


Mhe. Adamu Malima ametoa agizo hilo wakati wa kikao chake na Kamati ya fedha za Halmashauri ikiwa ni utekelezaji wa maagizo ya Kamati ya kudumu ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) iliyoagiza Halmashauri zote kujibu hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali – CAG.


Akiwa katika kikao hicho kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo, Adam Malima alisikitika kuona kuna baadhi ya halmashauri zina hoja za madeni makubwa ya wadaiwa sugu wa fedha za makusanyo kutoka kwa baadhi ya watumishi wa Serikali huku watumishi hao wakiwa nje bila ya kulipa fedha hizo.


Kwa sababu hiyo, Mkuu wa Mkoa huyo akawaagiza Wakurugenzi wote wa Halmashauri za Mkoa huo kutocheka na watumishi wa Serikali wasiowaaminifu wala kuwa na huruma nao, badala yake wawachukulie hatua kali za kisheria kila wanapobainika.


“Wizi wa fedha za POSI wasiachiwe wala kupewa msamaha, wawekeni ndani” alisema Adam Malima.


Sambamba na maelekezo hayo Mkuu huyo wa Mkoa akaiagiza Taasisi ya Kuzuia na kupambana na Rushwa - TAKUKURU Mkoa wa Morogoro kuchunguza wadaiwa hao na kufikishwa kwenye vyombo vya kisheria lakini pia taarifa zao ziwasilishwe Ofisini kwake.


“…hajawahi kulipa hata senti tano……kafungwa miaka miwili katoka bado hajawahi kulipa hata senti tano, TAKUKURU, nitafutieni Profile ya huyo mtu..” alisisitiza.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa kupitia kikao hicho aliwataka Wakurugenzi wa Halmashauri za Mkoa huo kutoa ushirikiano wa kutosha kwa viongozi walio chini yao Pamoja na watumishi wengine.

Kwa upande mwingine akawataka watumishi nao wafanye kazi zao kwa mujibu wa Sheria, taratibu na Kanuni na kwamba mtumishi atakayethibitika kufanya hujuma yoyote kwa Mkurugenzi wake atamchukulia hatua kali za kisheria.


Halmashauri ambazo zimeonekana zina watumishi wa umma ambao ni wadaiwa sugu wa fedha nyingi za Makusanyo ni Pamoja na Halmashauri ya Mlimba, Ifakara, Ulanga, Mvomero na Morogoro DC.



MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.