• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MOROGORO AWAKARIBISHA WAFANYABIASHARA WA COMORO, ANENA WAO NI NDUGU, AWASHANGAA KUTOZUNGUMZA KISWAHILI.

Posted on: July 3rd, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amewataka wakazi wa Mkoa huo hususan Chemba ya Wafanyabiashara, Viwanda na Kilimo (TCCIA) Mkoani humo kutumia ujio wa wafanyabishara kutoka Comoro kuwa ni fursa ya kukuza biashara zao na kuitaka TCCIA kufungua milango ya Biashara na watu wa Comoro.

Mhe. Adam Malima ametoa kauli hiyo Julai 3 mwaka huu wakati akizungumza na ujumbe wa wafanyabiashara kutoka Comoro ambao wako Mkoani Morogoro kwa ajili ya kuimarisha ushirikiano wa kibiashara baina ya nchi yao na Mkoa wa Morogoro.

Akifafanua zaidi, Mkuu huyo wa Mkoa amesema, nchi ya Comoro ina historia ndefu na ya siku nyingi ya kufanya biashara mbalimbali na Tanzania ikiwemo kufanya nayo biashara ya nyama, mchele, maharagwe na biashara nyingine hivyo amesema kuja kwa wafanyabiashara hao ni fursa ya kipekee kwa Mkoa huo.

“Tuione hiyo ziara ya wageni wetu kutoka Comoro kama ni fursa kubwa sana…” amesema Mhe. Adam Malima.

Akisisitiza zaidi kuhusu wafanya biashara hao kuwekeza Mkoani Morogoro, Mhe. Malima amesema, Mkoa huo una maeneo mengi na makubwa ya uwekezaji lakini pia una bahati ya kustawisha karibu kila zao ikiwemo zao la Karafuu, iriki, Vanila, kakaoa, pilipili mtama na bidhaa nyingine huku kisema Mkoa huo ni kinara wa kuzalisha mchele hapa nchini.

Katika hatua nyingine Kiongozi huyo amemtaka Mwenyekiti wa TCCIA Mkoa wa Morogoro Muadhini Mnyanza kufungua milango na wafanyabiashara hao huku akiwataka nao kujipanga Kwenda nchini Comoro kwa lengo la kuangalia fursa za kibiashara zinazopatikana huko.

Aidha, amesema kwa sasa watumie fursa ya ujio wao kufanya nao mazungumzo ya kina kuhusu sekta ya biashara na kuanza ushirikiano nao kwani amesema watu wa Comoro pia ni ndugu kihistoria na huku akiwashawishi kujifunza na kuongea lugha ya Kiswahili.

Kwa upande wao Kiongozi wa Wafanya biashara hao kutoka Comoro Ahmed Rassoul amesema lengo la ziara yao Mkoani Morogoro kuona mazingira ya Mkoa huo na kubadilishana mawazo juu ya pande hizo mbili na kushirikiana katika sekta ya Biashara.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima (aliyevaa kanzu nyeupe, kibagharashia na miwani) akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wafanyabiashara kutoka Comoro kuja Morogoro kwa ziara maalum

Kwa upande wake Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro Mhe. Pascal Kihanga amesema atahakikisha wanafanya nao kikao na kuzungumza kwa kina kuhusu ushirikiano wa kibiashara na kuahidi kutoa ushirikiano kwao wakati wote watakapokuwa Mkoani hapa.

Mwenyekiti wa Chemba ya Wafanyabiashara, Viwanda na Kilimo (TCCIA) Mkoa wa Morogoro Muadhini Mnyanza amesema watafanya mazungumzo ya kina na ikibidi watawekeana makubaliano ya kibiashara kwa faida ya pande hizo mbili.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.