• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MOROGORO AZUNGUMZIA UTAJIRI WA ULANGA, AMSIFU MWEKEZAJI WA MADINI

Posted on: November 20th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma Mwassa amesema Wilaya ya Ulanga ina madini mengi yenye thamani kubwa yakiwemo madini ya Rubi Pamoja na vivutio vingi vya utalii, na kuwataka watu kutoka ndani na nje ya nchi Kwenda wilayani Ulanga kuwekeza katika sekta hizo.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma Mwassa akihutubia wananchi Wilayani Ulanga kwenye Uzinduzi wa tamasha la Uwekezaji linalojulikana  kama Iherepa 2.

Mhe. Fatma Mwassa ametoa rai hiyo Novemba 19 mwaka huu kwenye uzinduzi wa Tamasha la Uwekezaji linalojulikana kama Iherepa 2 lililofanyika Wilaya ya Ulanga, Mkoani humo.

Aidha, Mkuu wa Mkoa amesema utajiri uliopo kwenye Wilaya hiyo unaotokana na wingi wa aina mbalimbali za madini yenye thamani kubwa hivyo kuvutia wageni wengi kutoka nje ya Wilaya hiyo na mzunguko mkubwa wa fedha zinazotokana na uchimbaji wa madini au utalii katika Wilaya hiyo.

Hapa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma Mwassa anasikiliza ufafanuzi wa uchimbaji madini kutoka kwa wataalamu wa madini kwenye banda mojawapo yaliyoshiriki kwenye tamasha hilo la Iherepa.

“...lakini kuzinduliwa kwa jambo hili kunatoa fursa kwa wageni wengi kuja, kwanza kufanya utalii, kwa sababu idea hii ya ku connect madini na utalii imekuwa ni kitu kipya kwa eneo hili na kwa watanzania wengi...” amesema Fatma Mwassa.

Mkuu huyo wa Mkoa ameongeza kuwa Wilaya hiyo imebarikiwa kuwa na vivutio mbalimbali vya utalii vya kipekee na kuifanya Wilaya hiyo kuwa ya kipekee kupitia Sekta hiyo ya utalii, vivutio hivyo ni Pamoja na Hifadhi ya Taifa ya Mwalimu Nyerere ambayo imesheheni baianuai ya kuvutia.

Muonekano wa nje wa jengo la kitalii ambalo limejengwa na kunakishiwa kwa miamba ya mawe .

Muonekano wa ndani wa jengo la kitalii ambamo kuna samani za kuvutia zilizotengenezwa kutokana na mawe yaliyochongwa yanayotokana na miamba iliyopo eneo hilo.

Aidha, Mhe. Fatma Mwassa ametumia tamasha hilo kusisitiza Halmashauri zote Mkoani humo kutunza mazingira kwa kupanda miti Zaidi ya milioni moja kwa kila mwaka ili kurudisha uoto wa asili na majira ya mvua kunyesha inavyotakiwa.

Sambamba na hilo, Mkuu wa Mkoa amempongeza Mbunge wa Jimbo la Ulanga Mhe. Salim Hasham, ambaye pia ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Ruby International, kwa kujitoa na kuwekeza katika sekta ya Madini Wilayani humo.

Mhe. Fatma Mwassa akimpongeza Mhe. Salim Hasham Mbunge wa Jimbo la Ulanga ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Ruby International kwa kuwa mzalendo kuwekeza katika Jimbo lake.

Mhe. Majid Mwanga Mkuu wa Wilaya ya Kilosa akiwa pamoja na Mhe. Mathayo Maselle Mkuu wa Wilaya ya Malinyi.

Katika hatua nyingine amempongeza Mbunge huyo kuwa na nia ya kuwa mchimbaji mkubwa wa madini na kuwainua wachimbaji wadogo anaofanya nao kazi hiyo kwa kuwawezesha kuchimba kisasa.

Kwa upande wake Mbunge wa Ulanga Mhe. Salim Hasham amesema wamejipanga kuhamasisha utangazaji wa fursa za uwekezaji zilizopo katika Wilaya hiyo na Mkoa kwa ujumla, pia amesema wanatarajia kukuza sekta ya kilimo kwa kulima mazao ya kimkakati.

Nae Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Morogoro Paul Ngwembe ameomba kuwepo ushirikiano na mhimili wa mahakama kwakuwa wote wanalenga kujenga jamii isiyo migogoro, ameongeza kuwa wako mbioni kujenga Mahakama za Wilaya za kisasa za ulanga, Malinyi na Kilosa, na baada ya miaka miwili Wilaya zote ndani ya Mkoa huo zitakuwa na Mahakama.

Mhe. Fatma Mwassa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro akiwa pamoja na Mhe. Paul Ngwembe Jaji Mkuu wa Mahakama Kuu Kanda ya Morogoro.

Tamasha hilo la Ulanga Iherepa limeambatana na shughuli mbalimbali ikiwa ni Pamoja na maonesho ya utalii, uchimbaji madini, michezo ya mbio za baiskeli milimani na utalii wa mbuga ya Mwalimu Nyerere.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma Mwassa akitoa vyeti vya pongezi kwa washindi na washiriki mbalimbali katika tamasha hilo.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.