• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

SERIKALI KUTENGA BIL. 15 KUONDOA CHANGAMOTO YA USAFIRI KWA JESHI LA POLISI.

Posted on: July 15th, 2023

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Mhandisi Hamad Masauni (Mb) amesema Serikali imetenga bilioni 15 kwa mwaka wa fedha 2023/2024 kwa ajili ya kununua magari na pikipiki nchi nzima ili kuondoa changamoto ya ukosefu wa vyombo vya usafiri kwa Jeshi la Polisi.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Mhandisi Hamad Masauni (kushoto) akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima wakati wakikagua kituo cha Polisi kata ya Mvomero.

Waziri Masauni ameyasema hayo Julai 14 mwaka huu alipotembelea na kukagua ujenzi wa kituo cha Polisi kat a ya Mvomero ikiwa ni ziara ya siku moja katika Wilaya hiyo Mkoani Morogoro.

" ...Serikali itanunua pikipiki kwa ajili ya vituo vya Polisi vya kata nchi nzima pamoja na magari kila Wilaya, tayari bilioni 15 zimetengwa kwa ajili ya kufanikisha hilo..."amesema Waziri Masauni.

Wakati akiwa kwenye mkutano na wananchi wa Kata hiyo Waziri Masauni amewataka wananchi kuthamini juhudi zinazofanywa na Serikali ya awamu ya sita chini ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwaletea wananchi wake maendeleo katika sekta mbalimbali zikiwemo Sekta za Afya, maji, elimu, umeme na miundombinu ya barabara.

Mhe. Mhandisi Hamad Masauni Waziri wa Mambo ya Ndani akizungumza kwenye mkutano na wananchi wa eneo la Wami-Dakawa Wilayani Mvomero.

Sambamba na hilo, Mhe. Hamadi Masauni ameahidi kufanyia kazi kero zilizotolewa na wananchi ili kuhakikisha kuwa haki inapatikana kwa wanyonge na kwa wale wanaostahili kupata haki hiyo.

Nae, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima amemshukuru Waziri huyo kwa kuwapatia vitendea kazi jeshi la polisi ikiwemo vyombo vya usafiri ili kuongeza ufanisi wa jeshi hilo katika utendaji wao wa kazi.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima akizungumza na wananchi wakati wa mkutano.

Aidha, Mkuu wa Mkoa ameahidi kufanya ziara katika Wilaya hiyo kusikiliza na kutatua kero za wananchi.

Kwa upande wake Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro ACP Hassan Omary amesema suala la ulinzi na usalama ni jukumu la kila raia, hivyo amewataka wananchi kuunda vikundi vya ulinzi shirikishi katika maeneo yao kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi. 

Bw. Haruna Ally mkazi wa Wami-Dakawa wakati akitoa kero zinazowasumbua amesema wakulima wa eneo hilo wanasumbuliwa na wafugaji kulisha mifugo kwenye mashamba ya wakulima, hivyo ameiomba mamlaka husika kushughulikia suala hilo.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.