• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Serikali ya Awamu ya Sita yapongezwa ujenzi bwawa la Kidunda.

Posted on: October 14th, 2023

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira imeipongeza Serikali ya  Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa zaidi ya shilingi bilioni 300 kwa ajiri ya ujenzi wa bwawa la Kidunda ambalo litaondoa changamoto ya upatikanaji wa maji katika mikoa ya Morogoro, Pwani na Dar es salaam.

Pongezi hizo zimetolewa Oktoba 13 mwaka huu na Kaimu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Felix Kavejuru Mbunge wa jimbo la Buhigwe baada ya kamati hiyo kutembelea eneo la mradi lililopo katika Tarafa ya Ngerengere, Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro kwa lengo la kuona hatua ya ujenzi iliyofikiwa.

Mhe. Kavejuru amesema bwawa hilo ambalo lilitakiwa kujengwa toka mwaka 1955 bila mafanikio lakini Mhe. Samia Suluhu Hassan ameamua lijengwe ili kuondoa adha ya upatikanaji wa maji kwa wananchi wa mikoa mitatu ya Morogoro, Pwani na Dar es Salaam.

“...tunampongeza sana Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania... yeye ni jasiri ameamua kwa dhati kutatua changamoto ya maji katika Mkoa huu wa Morogoro na kwa Mkoa wa Dar es Salaam...” amesema Mhe.Felix Kavejuru.

Aidha, Kamati hiyo imeipongeza Serikali kwa mikakati ya kupunguza changamoto ya kukosa umeme kwa wakazi wa eneo la mradi unaotarajiwa kuzalisha umeme Megawati 20 kati ya hizo KV 33 utasambazwa kwa vijiji vinne vya eneo la mradi na mwingine kuingizwa katika gridi ya Taifa hivyo kuchochea ukuwaji wa viwanda nchini.

Kamati imeuagiza uongozi wa Bodi ya Maji Bonde la Wami/Ruvu kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na Wilaya ya Morogoro kuhakikisha vyanzo vya maji vinavyolisha bwawa hilo vinalindwa ili kuwa na uhakika wa maji ambayo ndiyo uhai wa bwawa hilo.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Maji Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi amesema bwawa la kidunda ni miongoni mwa jitihada za Serikali za kuvuna maji ya mvua ili kuwa na uhakika wa maji katika kipindi chote cha mwaka huku akibainisha kuwa ujenzi huo ambao tayri umefikia asilimia 15 unatarajia kukamilika ifikapo Juni 2026.

Ameongeza kuwa, wakazi wa maeneo ya mradi ambapo kuna vijiji zaidi ya vinne watakuwa wakwanza kunufaika na mradi huo ili kuwaondolea adha ya kutumia maji chumvi.

Naye Msimamizi wa mradi huo Mhandisi Christian Gava amesema bwawa hilo litakuwa na uwezo wa kuhifadhi maji kipindi cha mvua zaidi ya lita za ujazo bilioni 190 litakuwa na urefu wa mita 870 na kina cha mita 21. Mradi huo umetoa ajira 326 ambapo asilimia kubwa ni wakazi wa maeneo ya mradi unapojengwa.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.