• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Serikali Yatoa Tsh. Bil. 310 Kujenga, Kukarabati Miundombinu ya Shule

Posted on: July 24th, 2024

Serikali imetoa jumla ya shilingi bil. 310 kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya shule 707 hapa nchini ukiwemo ujenzi wa shule mpya, kuongeza vyumba vya madarasa katika shule mbalimbali za sekondari zenye uhitaji pamoja na ukarabati wa miundombinu mingine ya shule hizo.

Hayo yamebainishwa Julai 24, 2024 na Mwl. Ephreim Simbeye ambaye alikuwa Mgeni rasmi kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teklolojia Prof. Carolyne Nombo wakati akifungua Mafunzo ya siku tatu kwa Maafisa Elimu Mikoa, Halmashauri, Maafisa Tehama, Maafisa ugavi, na Wakuu wa shule za sekondari.

Akifafanua zaidi katika kikao hicho kilichofanyika Chuo cha Elimu ya watu wazima cha Morogoro (WAMO) Mwl. Ephreim Simbeye amesema lengo la kikao hicho ni kutoa uwezo kwa maafisa hao katika usimamizi wa miradi ya shule za Msingi na Sekondari.

”…jumla ya Tsh. Bil. 310 zimetumwa katika shule 707 kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya za sekondari…” amesema Mwl. Ephreim Simbeye

Amebainisha kuwa fedha hizo zitatumika katika kujenga madarasa mapya ya shule za sekondari za wavulana za kanda, shule za kata, upanuzi wa shule kwa ajili ya kidato cha tano na ukamilishaji wa miundombinu ya shule za wasichana za Mikoa, hivyo amewataka Wakuu wa Shule za sekondari na Misingi kuwa wadilifu na waminifu katika kutekeleza miradi mbalimbali ya Serikali.

Sambamba na hilo, Mwl. Ephreim amesema kupitia mradi wa Kuimarisha Elimu ya Sekondari (SEQUIP) serikali imedhamiria kuboresha ufundishaji kupitia mpango wa mafunzo endelevu ya Walimu kazini (MEWAKA) ambapo Walimu wa Sayansi na Hisabati wamepatiwa mafunzo ili kuongeza umahiri wa ufundishaji darasani.

Katika hatua nyingine, Mwl. Simbeye amesema serikali imejipanga kuboresha Elimu hapa nchini ikiwemo kuboresha miundombinu ya shule kwa ajili ya kujifunzia na kufundishia ili kuongeza ufaulu, kwani amesema kumekuwa na ongezeko la wanafunzi wanaodahiliwa katika shule za msingi na sekondari huku ikionekana kuwa na changamoto ya miundombinu mashuleni hususan vyumba vya madarasa.

Pia amesema serikali ina mpango wa kuingia katika mafunzo ya kidijitali ambapo vifaa vya Maabara na TEHAMA vitasambazwa kwa shule 281 kupitia wazabuni waliopatikana. 

Kwa sababu hiyo, Mwalimu huyo amewasisitiza Wakuu wa shule kuhakikisha wanaweka mifumo na mikakati thabiti ya kuwalinda watoto kwa kushirikiana na jamii dhidi unyanyasaji na ukatili wa wanafunzi ndani na nje ya shule kwa kuanzisha vilabu vya wanafunzi kwa ajili ya kujitambua na kujiamini ili kuwa na ujasili wa kueleza wanapopatwa na changamoto kama hizo.


Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Elimu ya awali na msingi OR – TAMISEMI Mwl. Sussan Nussu amesema Wizara ya Elimu, Sayansi, na Teknolojia imeweka miongozo mbalimbali itakayotumika katika miradi ya ujenzi wa miundombinu ya shule za serikali lengo ni shule zinazojengwa ziwe zinakidhi viwango bora vilivyokubalika (Value for Money).


Naye, Mratibu wa mradi wa SEQUIP Bw. Richard Makota amesema mafunzo hayo yatatolewa kwa makundi 6 ambapo kwa sasa wameanza na makundi 3 yanayofanyika katika Mikoa ya Mtwara, Morogoro na Mwanza lengo likiwa ni kufikia mikoa yote 26 ya Tanzania Bara na Halmashauri 184 na shule zilizopokea fedha kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu hiyo. 


MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.