• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

SHIGELA AAGIZA MIRADI YA MAJI KUKAMILIKA HARAKA

Posted on: June 11th, 2022

       SHIGELA AAGIZA MIRADI YA MAJI KUKAMILIKA HARAKA       

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela amewaagiza Maafisa wa Mamlaka ya maji safi na Usafi wa Mazingira Mkoa wa Morogoro (MORUWASA) pamoja na wakandarasi wanaosimamia Ujenzi wa matenki mawili ya maji yatakayohudumia kutoa maji maeneo ya Mkundi, Kihonda na Tungi kuhakikisha mradi huo unakamilika kwa wakati ili kutatua changamoto ya maji kwa wananchi wa maeneo hayo.

Martine Shigela ametoa agizo hilo Juni 9 mwaka huu wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro na kusikiliza kero za wananchi kwa Kata zote zilizoko katika Halmashauri hiyo.   


Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela (mwenye shati ya dhambarau) akitoa maelekezo kwa wahandisi na MORUWASA kama wasimamizi wa mradi wa ujenzi wa kituo cha kusambaza maji kukamilisha mradi huo ndani wakati uliopangwa.

Aidha, Martine Shigela amesema Serikali katika kutatua changamoto hiyo tayari imetoa kiasi cha zaidi ya shilingi     1.5 Bil. ili kugharamia ujenzi wa matenki hayo na kituo kimoja cha kusambazia maji kwa wananchi wa maeneo hayo.

Shigela amebainisha kuwa ujenzi wa atenki kubwa la kuhifadhia maji upande wa Kihonda na Mkundi hadi kukamilika kwake litagharimu shilingi milioni 600, ujenzi wa tenki la maji lenye ujazo wa maji lita 1mil. upande wa Tungi na Kilimanjaro limegharimu shilingi 467mil pamoja na ujenzi wa kituo cha pampu mbili za kusukuma maji kilichogharimu kiasi cha milioni 590.


“zaidi ya Tsh 1.6 Bil. zimeshatolewa kwa wakandarasi, hivyo ninaagiza kwa wakandarasi na MORUWASA kuhakikisha mradi huu unakamilika kwa wakati ili ndani ya mwaka huu wananchi waanze kupata huduma ya maji” ameagiza Shigela.

Kwa upande wake Mstahiki Meya wa Hamashauri ya Manispaa ya Morogoro Mhe. Pascal Kihanga ameishukuru Serikali kwa jitihada za kutatua kero ya maji kwa wananchi wa maeneo hayo kwani huduma ya maji kimekuwa ni kilio cha muda mrefu kwa wananchi hao, hivyo kukamilika kwa miradi hiyo kutasaidia wananchi kuondokana na changamoto hiyo.



Naye meneja ufundi wa MORUWASA Mhandisi Victor Ngowi amemuhakikishia Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kukamilisha mradi huo wa maji kwa muda uliopangwa na kuahidi kufanya kazi hiyo usiku na mchana.



Mradi huo wa maji ambao unahusisha ujenzi wa  matenki mawili ya maji na kiutuo cha kusukuma maji umeanza Machi 30 na unatarajia kukamilika Juni 30 mwaka huu lengo ni kuharakisha kukamilika kwake ili kutatua kero hiyo ya maji kwa wananchi wa maeneo ya Mkundi, Kihonda na Tungi.

Muonekano wa kituo cha kusambaza maji kilichopo Kihonda Mizani ambapo kilikaguliwa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Juni 9 Mwaka huu wakati ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.




MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.