• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

TRA Morogoro yazindua Wiki ya Huduma kwa Mlipakodi.

Posted on: October 3rd, 2023

Mamlaka ya Mapato nchini Tanzania (TRA) Mkoani Morogoro imezindua Wiki ya Huduma kwa mlipakodi ikiwa na lengo la kuboresha huduma zake kwa kuwakutanisha walipakodi na wataalam wa TRA ili kutatua changamoto zinazowakabili wakati wa ulipaji wa kodi. 

Akizindua hafla hiyo Oktoba 03 mwaka huu iliyofanyika katika Ofisi za Mamlaka hiyo, Meneja wa TRA Mkoani humo Bw. Sylver Rutagwelera amesema lengo ni kumuwezesha mlipakodi kulipa kodi kwa urahisi kutokana na umuhim wa walipakodi hao.

Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoani Morogoro Bw. Sylver Rutagwelera (kushoto) akimlisha keki Makamu Mwenyekiti wa Chemba ya Wafanyabiashara Mkoani humo Prof. Faustin Lekule wakati wa hafla ya uzinduzi wiki ya Huduma kwa Mlipakodi Mkoani Morogoro.

“...leo tunazindua Wiki ya Huduma kwa Mlipakodi...Focus ya Mamlaka ni mlipakodi, namna gani tunamuwezesha huyu mtu kulipa kodi kiurahisi...” amesema Bw. Rutagwelera.

Aidha, Bw. Rutagwelera amebainisha kuwa TRA imelenga kuwafikia wateja wake kwa kusogeza huduma katika Wilaya za Mkoa huo, kuweka mifumo ya kisasa ambayo itawawezesha walipa kodi kulipa kodi zao katika maeneo waliyopo bila kufika ofisini.

Meneja huyo ameongeza kuwa Mamlaka ya Mapato Mkoani humo inapokea malalamiko, ushauri na changamoto za walipakodi wakati wote hivyo amewataka kufika katika Ofisi za TRA ili waweze kusikilizwa na kuhudumiwa.

Kwa upande wake Afisa Mfawidhi anayeshughulikia ushuru wa Forodha Bw. Shadrack Mbonea amewataka wafanyabiashara kuacha tabia ya kupitisha bidhaa kwa magendo bila kulipia ushuru na kukaguliwa ili kuepuka athari zitokanazo na bidhaa kama vile pombe kali na vipodozi. Pia, amesema kwa kufanya hivyo wanapunguza mapato ambayo Serikali ingeyatumia kuwaletea maendeleo wananchi wake.

Meneja wa TRA Mkoa wa Morogoro Bw. Sylver Rutagwelera akifurahia kinywaji pamoja na wadau mbalimbali wakati wa hafla ya uzinduzi wa Wiki ya Huduma kwa Mlipakodi.

Naye, Makamu Mwenyekiti wa Chemba ya Biashara, Viwanda na Kilimo (TCCIA) Mkoani Morogoro Prof. Faustin Lekule ameipongeza TRA Mkoani humo kwa kutoa elimu ya kodi kwa wafanyabiashara kwa kuwa elimu hiyo imesaidia kukuza mitaji yao ambapo kwa sasa wanapata mikopo kutoka taasisi mbalimbali za kifedha.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti baadhi ya walipa kodi Mkoani humo akiwemo Mkurugenzi wa Moro Batiki Dkt. Herriet Mkaanga  amewataka wafanyabishara kulipa kodi ili Serikali iweze kutekeleza miradi mbalimbali ya kimaendeleo hapa nchini.

Naye Bw. Dastan Mziwanda Mjasiliamali mdogo katika Manispaa ya Morogoro ameipongeza TRA kwa huduma bora huku akiwataka wataalam wa Mamlaka hiyo kuwafikia wafanyabiasha waliopo maeneo ya vijijini ili kuwapa elimu ya kodi.

Hawa ni baadhi ya wafanyakazi wa TRA Mkoani Morogoro wakiwa kwenye hafla ya uzinduzi wa Wiki ya Huduma kwa Mlipakodi.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.