• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Viongozi wa Dini watakuwa kutoa elimu juu ya mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI.

Posted on: November 29th, 2023

Viongozi wa Dini wametakiwa kutumia majukwaa hayo kutoa elimu kwa jamii kuwa na mwitikio chanya katika mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI kwa kuwa wao wana ushawishi katika mkubwa kwa jamii zao.

Nasaha hizo zimetolewa leo Novemba 29, 2023 na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu Dkt. Jim Yonazi wakati akifungua mdahalo wa Vijana na Viongozi wa Dini uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Nashera iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Dkt. Yonazi amesema kuwa Viongozi wa Dini wanaushawishi mkubwa katika jamii zao hivyo wanatakiwa watoe elimu kwa waumini wao kupitia nyumba hizo za ibada kwani kwa kufanya hivyo jamii itakuwa na mwitikio chanya juu ya mapambano dhidi ya UKIMWI na kuisaidia jamii kuwa na uelewa wa masuala ya UKIMWI.

“...nitoe rai kwa viongozi wa dini kutumia majukwaa yao kutoa elimu ili kusaidia kuhamasisha waumini na jamii ambayo ni vijana, watoto na watu wazima kuwa na mwitikio uliyochanya dhidi ya mapambano ya UKIMWI...” amesema Katibu Mkuu.

Aidha, Katibu Mkuu huyo amebainisha kuwa kupitia elimu hiyo itawezesha nchi kufikia malengo ya 95 tatu ifikapo 2025 dhidi ya mapambano ya ugonjwa wa UKIMWI yaani asilimia 95 ya watu wawe wanajua hali zao, asilimia 95 ya watu wanaotumia dawa za kufubaza virusi vya UKIMWI – ARV na asilimia 95 ya tatu watu wanaotumia dawa za ARV wawe wamefubaza virusi hiyo.

Katika hatua nyingine Dkt. Jim Yonazi amewashauri wadau wanaotekeleza afua za UKIMWI nchini kuwajengea uwezo Viongozi wa dini kuhusu elimu ya VVU na UKIMWI, ukatili wa kijinsia, elimu ya Afya ya uzazi, unyanyapaa na ubaguzi, mimba na ndoa katika umri mdogo hii itasaidia kuongeza ushiriki wa Viongozi hao katika mapambano ya dhidi ya UKIMWI.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maridhiano Mkoa wa Morogoro Shekhe Juma Yahaya ametumia mdahalo huo kuwakumbusha Vijana kuwa ni Taifa la Kesho hivyo amewataka kujikinga na maambukizi ya VVU pamoja na kuwashauri Vijana waliopo katika ndoa kuheshimu ndoa zao huku akisisitiza vijana kufuata maamrisho ya dini zao.

Naye Mwakilishi kutoka Wizara ya Afya Dkt. Catherine Joakim amewashukuru Viongozi wa dini kwa niaba ya Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu kwa kuwa viongozi hao wamekuwa na mchango mkubwa katika kufikisha elimu ya masuala ya Afya kwa waumini wao hususan mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.