• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

VYAMA VYA USHIRIKA VYATAKIWA KUZINGATIA MWONGOZO MPYA WA ELEKTRONIKI.

Posted on: December 8th, 2022

Vyama vya Ushirika hapa nchini vimetakiwa kufuata mwongozo wa mfumo mpya wa elektroniki wa usimamizi wa vyama vya ushirika pamoja na Waraka wa Mrajisi Na.2 wa mwaka 2022 ili kuleta ufanisi katika usimamizi wa vyama hivyo.

Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ally Mussa akiongea na viongozi na wanachama wa vyama vya ushirika wakati akifungua mafunzo ya mfumo mpya wa kielektroniki ambao utatumika kusimamia na kuendesha shughuli za vyama vya ushirika.

Hayo yameelezwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa Disemba 7 mwaka huu wakati akifungua mafunzo ya siku tatu ya mfumo wa kielektroniki wa usimamizi wa vyama vya Ushirika kwa Maafisa Ushirika wa Mikoa ya Morogoro na Pwani yaliyoandaliwa na Tume ya maendeleo ya Ushirika ambayo yamefanyika katika Hoteli ya Savoy Manispaa ya Morogoro.

Mrajisi Msaidizi Mkoa wa Pwani akipokea Kompyuta kutoka kwa mgeni rasmi Dkt. Mussa Ally Mussa, kompyuta hizo zimetolea na Tume ya maendeleo ya Vyama vya Ushirika kwa ajili ya kusimamia shughuli za vyama kwa mfumo wa kielektroniki.


Mrajisi Msaidizi wa vyama vya ushirika Mkoa wa Morogoro Bw. Kenneth Shemdoe akipokea kompyuta kwa ajili ya shughuli za vyama vya ushirika kupitia mfumo mpya wa kielektroniki.

Dkt. Mussa Ali Mussa ametaja faida za matumizi ya mfumo huo wa kielektroniki kuwa ni pamoja na kuongoza vyama vya ushirika katika uboreshaji na utekelezaji wa shughuli mbalimbali za Serikali kwenye ushirika, kuboresha usimamizi na uendeshaji wa vyama hivyo vya ushirika, kuwezesha upatikanaji wa masoko kwa wakulima, pamoja na kuinua uchumi wa wanaushiriki na Uchumi wa Taifa kwa jumla.

“...kwa vyama vyote vya ushirika kuzingatia mwongozo wa mfumo wa usimamizi wa vyama vya ushirika pamoja na waraka wa mrajisi namba mbili (2) wa mwaka 2022... aidha kila chama kuhakikisha kinakuwa na vifaa vya tehama..” Amesema Dkt. Mussa Ali Mussa.

Katibu Tawala huyo amesema vyama hivyo vimekuwa vikikabiliwa na changamoto mbalimbali zilizopelekea baadhi yao kuteteleka ama kufa kabisa kutokana na changamoto hizo zikiwemo za ugumu wa kuhuisha daftari la taarifa za usajiri wa vyama vya ushirika na wanachama wa ushirika, utendaji usioridhisha, ukosefu wa taarifa sahihi na uwepo wa mifumo duni ya mawasiliano.

Sambamba na hilo Katibu Tawala huyo amesema Serikali inatambua kuwa vyama vya ushirika ni silaha ya wanyonge na nguzo kuu ya ujenzi wa uchumi jumuishi wa Taifa katika kufikia malengo na mipango ya maendeleo ili kuwafikia wananchi wengi, kwa mantiki hiyo, ikaamua kutunga sheria ya vyama vya ushirika namba sita (6) ya mwaka 2013 kwa lengo la kusimamia na kuratibu maenedeleo ya vyama vya ushirika hapa nchini.

Baadhi ya wataalam viongozi na wanachama wa vyama vya ushirika wakimsikiliza mgeni rasmi Dkt. Mussa Ali Mussa akitoa hotuba yake ya ufunguzi wa mafunzo ya mfumo wa elektroniki.

Kwa upande wake Bw. Kenneth Shemdoe ambaye ni Mrajisi Msaidizi wa Vyama vya Ushirika Mkoa wa Morogoro amesema lengo la kuwepo kwa mafunzo hayo kwa maafisa wa ushirika kutoka mikoa ya Pwani na Morogoro ni kuongeza ufanisi katika kusimamia na kuendesha majukumu ya vyama vya ushirika kwa kupitia mfumo huo mpya wa kielektroniki.

Bw. Kenneth Shemdoe ametoa wito kwa wananchi wa Mikoa hiyo miwili kujiunga na vyama vya Ushirika kwa kuwa Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ipo macho na vyama vya ushirika  na kwamba usimamizi wake unatakiwa uwe wa  hali ya juu wanachama wake wasidhurumiwe kwa aina yoyote.

Bw. Kenneth Shemdoe akielezea lengo na umuhimu wa mafunzo hayo kwa maafisa ushirika katika Mkoa wa Morogoro.

Nae Bw. Beatus Ligogoderi ambaye ni Mhasibu wa chama cha Ushirika cha Ulanga – Kilombero amesema mafunzo hayo yatawasaidia wanaushirika katika kutunza kumbukumbu na mali za ushirika pamoja na kuwasaidia wakulima kupata masoko ya uhakika.

Kwa upande wake Bw. Karunda Mfumo huo utasaidia kuongeza mnyororo wa thamani kwenye kilimo kwa sababu mfumo utaleta taarifa sahihi hususani upatikanaji wa masoko ya uhakika ndani na nje ya nchi hivyo wakulima watakuza kipato chao.

Picha za mgeni rasmi akiwa kwenye picha ya pamoja na Maafisa, Viongozi, na wanachama wa vyama vya ushirika kutoka mikoa ya Morogoro na Pwani baada ya ufunguzi wa mafunzo ya mfumo mpya wa  kielektroniki kwa ajili ya vyama vya ushirika.

Mafunzo hayo ya siku tatu kwa mikoa ya Morogoro na pwani ni mwendelezo wa mafunzo yaliyoanza mwezi Januari mwaka huu na hadi sasa yametolewa kwa Maafisa Ushirika wa kutoka mikoa 19 sasa huku yakitarajiwa kuhitimishwa Disemba 31 mwaka huu. 

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.