• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

WATOTO WENYE MENO YANAYODHANIWA KUWA YA PLASTIKI, VIMEO VIREFU NA UDATA WAPELEKWE VITUO VYA AFYA – DKT. BEST.

Posted on: March 12th, 2025


Mganga Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Dkt. Best Richard Magoma, amewataka wazazi na walezi kote nchini kuwapeleka watoto wanaodhaniwa kuwa wana meno ya plastiki, vimeo virefu, na tatizo la udata katika vituo vya afya kwa ajili ya kupata matibabu ya kitaalamu badala ya kuendeleza mila potofu ya kuwapeleka watoto hao kwa waganga wa jadi.

Dkt. Magoma ametoa Wito huo Machi 12, 2025, wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni ya kutoa elimu kwa jamii dhidi ya ukatili wa ukeketaji wa viungo vya kinywa kwa watoto wachanga uzinduzi uliofanyika Hoteli ya Glonency Manispaa ya Morogoro.

Amesema, magonjwa hayo ya watoto yanatibika katika vituo vya afya, hivyo ni jukumu la kila mtu kulinda haki za mtoto hao huku akiwataka wazazi na walezi kuachana na dhana potofu ya kuwapeleka watoto kwa waganga wa jadi, kwani kufanya hivyo ni moja ya matendo ya ukeketaji na ni ukatili kwa watoto.

"Napenda kuchukua fursa hii kuwahimiza Watanzania wote kuwapeleka watoto wetu wanaodhaniwa kuwa na meno ya plastiki, kimeo kirefu, udata, na changamoto nyingine za kinywa katika vituo vya afya," amesema Dkt. Best Magoma.

Aidha, Dkt. Magoma amesema programu hiyo imelenga kutoa mafunzo kwa watoa huduma za afya 1,428, walimu wa afya mashuleni 1,327, kamati za maendeleo za kata, viongozi wa madhehebu ya dini 442, wahudumu wa afya ngazi ya jamii 2,101, pamoja na waganga wa tiba asili 450.

Ameongeza kuwa programu hiyo imeanza katika Mkoa wa Morogoro na itaendelea kwa kushirikiana na kamati za Usalama ngazi ya mkoa na wilaya ili kuwajengea uwezo maafisa hao katika kulinda afya za watoto.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za Kinywa na Meno kutoka Wizara ya Afya, Dkt. Baraka Nzobo, amesema wizara imejipanga kutokomeza tatizo hilo, hivyo amewataka wanaofanya shughuli za tiba asili wawe ni wale tu waliosajiliwa na Bodi ya Tiba Asili ili kufuata miiko na matakwa ya sheria katika utoaji wa tiba.

Aifha ameongeza kuwsWizara inalenga kutoa elimu kwa waganga wa jadi wanaotoa tiba zisizo rasmi ambazo zina madhara kwa watoto na kuonya kuwa wale watakaopuuza elimu hiyo na kuendelea na vitendo vinavyokiuka mafunzo, watakabiliwa na hatua kali za kisheria ili kukomesha ukatili huo kwa watoto.

Naye Rais wa Chama cha Wataalamu wa Afya ya Kinywa na Meno Tanzania (TDA), Dkt. Gemma Berege, ametoa wito kwa wataalamu wa tasnia ya afya ya kinywa na meno kuhakikisha wanatoa elimu kwa jamii juu ya dhana potofu zinazoathiri watoto. Pia amesisitiza umuhimu wa kutoa elimu ya afya ya kinywa na meno.


Kwa upande wake, mdau kutoka  Shirika la Sibaba Dental Clinic, Dkt. Nilla Jackson, ambaye amefadhiliwa na Shirika la Bridge 2 Aid, amesema kuna umuhimu wa kushirikisha kamati za usalama katika kulinda afya ya kinywa na meno ya mtoto ili kusaidia kukomesha vitendo vya ukeketaji kwa watoto wadogo nchini.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.