• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

WAZIRI MCHENGERWA ATOA MWEZI MMOJA KUKAMILISHA KITUO CHA AFYA RUAHA

Posted on: May 22nd, 2024

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Mohamed Mchengerwa (MB) ametoa mwezi mmoja kwa uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga kukamilisha ujenzi wa Kituo cha Afya cha Ruaha baada ya ujenzi wa kituo hicho kutokamilika kwa wakati.

Mhe. Mchengerwa ametoa agiza hilo Mei 22, 2024 baada ya kuanza ziara ya kukagua miradi ya maendeleo katika Halmashauri hiyo akianza na kukagua Kituo cha Afya cha Ruaha na kuonekana uamuzi wa ujenzi wa kituo hicho ni wa muda mrefu kilichokosekana ni nia thabiti ya kukikamilisha kwa wakati.

Amesema, mradi huo uliibuliwa na wananchi tangu mwaka 2019 hadi sasa pasipo kukamilika pamoja na jitihada za Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima kuhakikisha mradi huo unakamilika lakini kumekuwa na vikwazo vinavyosababisha wananchi kukosa huduma ya Afya ambayo ni haki yao ya msingi.

Kwa sababu hiyo Waziri Mchengerwa hakuridhishwa na kasi ya ujenzi huo na kumuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ulanga Bi. Saida Mahugu  pamoja na timu yake kukamilisha ujenzi huo ifikapo Juni 30 mwaka huu bila kuwa na nyongeza ya muda mwingine

"....  ninawataka Kila mmoja wenu kufanya kazi usiku na mchana Kituo hiki kimalizike tarehe 30 mwezi wa sita hakuna nyongeza..."

Sambamba na maagizo hayo ametumia fursa hiyo kumpongeza Mbunge wa Jimbo hilo Mhe. Salim Hashim kwa kutoa fedha shilingi milioni kumi kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa kituo cha Afya cha Ruaha ili kuhakikisha wapiga kura wake wanaondokana na usumbufu wa kufuata huduma ya Afya umbali mrefu.

Baada ya kutoa maagizo hayo Mhe. Mohamed Mchengerwa ambaye ni Waziri wa TAMISEMI alitembelea daraja la mto Luhombelo lililoharibiwa vibaya na mvua kubwa zilizonyesha kipindi cha karibuni daraja linalounganisha Kijiji cha Mwaya na Kijiji cha Mbuga Wilayani Ulanga na kutoa pole kwa wananchi wa vijiji hivyo kutokana na adha kubwa wanayoipata.

Hata hivyo, akiwa katika eneo la tukio, amemwagiza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo kutoa kiasi cha fedha cha shilingi Milioni 250 kwa ajili ya ujenzi wa daraja la muda kuwawezesha wananchi kupita na kupitisha mazao na bidhaa nyingine wakati wakisubiri ujenzi wa daraja la kudumu.

Awali akimkaribisha Waziri huyo wa TAMISEMI, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amesema kuwa maelekezo yote aliyoyatoa Waziri atayasimamia sambamba na kuhakikisha ujenzi wake unakamilika kwa muda uliopangwa ili wananchi waweze kuanza kupata huduma ya afya.

Tayari Waziri huyo amekwishatembelea Halmashauri tatu kati ya Halmashauri Nne alizokusudia kuzitembelea ambazo ni Halmashauri ya Ifakara Mji, Halmashauri ya Mlimba, Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi na Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga.

Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.