• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

HOJA ZA MANUNUZI ZASABABISHA RC KUTOA MAAGIZO MAZITO IFAKARA.

Posted on: June 9th, 2025


Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Mhe. Adam Kighoma Malima, ameutaka uongozi wa Halmashauri ya Mji wa Ifakara kuandaa mafunzo yanayohusu sheria za Manunuzi kwa ajili ya madiwani wa Halmashauri hiyo ili kuwa na uelewa wa kutosha kwa lengo la kusimamia vema fedha za Halmashauri yao.

Mhe. Adam Malima ametoa hilo Juni 9, 2025 wakati wa kikao cha Baraza Maalum la Madiwani cha kujibu hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesaba za Serikali (CAG) kilichofanyika katika Mji mdogo wa Ifakara ambapo hoja 18 zilizotakiwa kujibiwa hoja 12 zinazohusu masuala ya manunuzi.

“Hoja za manunuzi lazima madiwani wawe wanapigwa semina mara kwa mara ili kufungua macho yao kwenye masuala ya msingi…” Amesisitiza Mhe. Adam Malima.

Amesema, mafunzo hayo yatasaidia madiwani kusimamia fedha zinazotolewa na Serikali kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo na maeneo mengine na kujua jinsi ya kuwasimamia wataalam hususan katika kipindi hiki cha matumizi ya mifumo ili kugundua na kuchukua hatua haraka pale upotoshwaji unapotaka kutokea.

Naye Mkaguzi wa nje wa Mkoa wa Morogoro Bw. Baraka Mfugale amesema hoja za manunuzi zilizokosewa katika taratibu za manunuzi zitafutwa baada ya kufanyika ukaguzi na kubaini tatizo hilo halipo tena.

Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro Alhaji Dkt. Mussa Ali Mussa amesema maagizo yote yaliyojitokeza kwenye kikao hicho cha Baraza atayasimami na atakaa na watendaji wake katika kuhakikisha hoja za CAG zinapatiwa ufumbuzi.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Ifakara Mhe. Kassim Nakapala amesema licha ya mapungufu ya uwepo wa hoja nyingi za CAG katika Halmashauri hiyo bado halmashauri ya Ifakara haijawahi kupata hati chafu jambo ambalo linaakisi utendaji kazi mzuri wa Baraza la Madiwani.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Sainari, Mhe. William Walioto, ameunga mkono wito uliototlewa na Mkuu wa Mkoa wa kuwa na mafunzo ili kuwapa nguvu madiwani katika kusimamia fedha za maendeleo. Pia alibainisha kwamba ugeni wa mifumo kwa maafisa manunuzi umechangia kuchelewesha utekelezaji wa miradi.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • ZAIDI YA TRILIONI 3 ZATEKELEZA MIRADI YA MAENDELEO MKOANI MOROGORO

    June 16, 2025
  • UPUNGUFU WATUMISHI WAIBUKA HOJA ZA CAG MLIMBA.

    June 11, 2025
  • UPUNGUFU WA TUMISHI WAIBUKA HOJA ZA CAG MLIMBA.

    June 11, 2025
  • HOJA ZA MANUNUZI ZASABABISHA RC KUTOA MAAGIZO MAZITO IFAKARA.

    June 09, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.