Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe.Martine Shigela ameutaka uongozi wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kutoa vibali kwa dalala zinazofanya kazi katika Manispaa hiyo kupeleka wananchi katika Chuo Kikuu Cha Sokoine cha Kilimo - SUA kwa ajili ya kishiriki maadhimisho ya aliyekuwa Waziri Mkuu wa Tanzania hayati Edward Sokoine.
Mhe. Shigela ametoa kauli hiyo Leo Mei 25 Mwaka huu alipotembelea na kukagua Shughuli za maandalizi ya kilele cha maadhimisho ya kumbukizi ya miaka 37 tangu kufariki kwake yatakayofanyika Mei 27 mwaka huu ambapo Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Philipo Mpango anatarajiwa kuwa Mgeni rasmi.
MWISHO.
Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.