• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Serikali yawaondoa hofu wananchi juu ya upatikanaji wa sukari nchini.

Posted on: January 30th, 2024

Serikali kupitia Wizara ya Kilimo imewahakikishia wananchi juu ya upatikanaji wa Sukari nchini ambapo tayari shehena ya bidhaa hiyo tani 100000 imeshaingia nchini huku ikibainisha kuwa sukari hiyo itauzwa kwa bei elekezi kati ya shilingi 2,700 hadi 3,200 kwa kilo.

Serikali imebainisha hayo Hayo Januari 29, mwaka huu na Naibu Waziri wa Kilimo Mhe. David Silinde (MB) wakati wa ziara ya Kamati ya Bunge ya Biashara, Viwanda, Kilimo na Mifugo ilipotembelea kiwanda cha sukari cha Mkulazi kilichopo Wilayani Kilosa Mkoani humo.

Mhe. Silinde amekili kuwepo kwa uhaba wa sukari nchini unaotokana na viwanda kushindwa kuzalisha kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha hapa nchini na kusababisha bei ya sukari kupanda, hata hivyo amesema Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan imechukua hatua kudhibiti changamoto hiyo kwa kuagiza tani 100000 za sukari ambapo itauzwa kwa bei elekezi ili kila mwananchi aweze kumudu.

“...niwaambie tu wananchi Meli zimeshafika pale bandarini zipo kwenye maandalizi ya kushusha mzigo na sukari iliyoagizwa nchini na itauzwa kwa bei elekezi kati ya shilingi 2,700 na 3,200 kama ambavyo Bodi ya Sukari ilitoa...” amesema Mhe. Silinde.

Aidha, amesema Wizara imejiwekea mikakati ya muda mrefu na mfupi ambapo mkakati wa muda mrefu ni pamoja na kuondoa kabisa changamoto ya uhaba wa sukari nchini kwa kuongeza uzalishaji katika Viwanda vya sukari huku mkakati wa muda mfupi ni kuagiza sukari nje ya nchi hususan katika kipindi ambacho viwanda havizalishi.

Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Biashara, Viwanda, Kilimo na Mifugo Mhe. Deo Mwanyika (Mb) amesema lengo la ziara hiyo ni kuangalia changamoto zinazopelekea kushuka kwa uzalishaji wa sukari nchini katika viwanda mbalimbali huku akithibitisha kuwa kweli mvua zinazoendelea kunyesha ambazo zimeongezeka kutoka mililita 200 hadi mililita 760 zimesababisha miundombinu ya barabara za mashamba na mashamba yenyewe kujaa maji hivyo kupelekea shughuli za uzalishaji sukari kusua sua.

Aidha, ameitaka Serikali kuhakikisha kuwa sukari iliyoagizwa kutoka nje inawafikia wananchi kwa bei elekezi ambayo imepangwa ili kuwaondolea wananchi malalamiko ya kupanda kwa kutokana na  uhaba wa bidhaa hiyo.

Kiwanda cha sukali cha Mkulazi hadi sasa kimezalisha zaidi ya tani 500 za sukari ambapo hivi karibuni zitaingizwa sokoni kwa ajili ya matumizi

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • WAHARIRI NCHINI WAPATIWA MAFUNZO USIMAMIZI WA MNYORORO WA UGAVI.

    June 17, 2025
  • ZAIDI YA TRILIONI 3 ZATEKELEZA MIRADI YA MAENDELEO MKOANI MOROGORO

    June 16, 2025
  • UPUNGUFU WATUMISHI WAIBUKA HOJA ZA CAG MLIMBA.

    June 11, 2025
  • UPUNGUFU WA TUMISHI WAIBUKA HOJA ZA CAG MLIMBA.

    June 11, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.