• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RAS MOROGORO AFUNGA MAFUNZO YA PEPMIS, ATAKA UWAJIBIKAJI NA UAMINIFU

Posted on: June 28th, 2025


Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro, Alhaji Dkt. Mussa Ali Mussa, amewataka watumishi wa umma mkoani humo kuwajibika na kuwa waaminifu katika kujaza mfumo wa mwongozo wa utekelezaji wa usimamizi wa utendaji kazi (PEPMIS), ili kuhakikisha mkoa huo unatekeleza kikamilifu agizo la Serikali.

Dkt. Mussa alitoa kauli hiyo tarehe 28 Juni 2025, wakati akifunga mafunzo ya siku sita kuhusu ujazaji wa mfumo huo wa PEPMIS, yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro, ikiwa ni siku ya mwisho ya mafunzo hayo mkoani humo.

Amesema kuwa wakuu wa seksheni, idara na vitengo wasipokuwa waaminifu na kuruhusu ujazaji holela wa taarifa katika mfumo huo, itakuwa vigumu kufikia malengo ya Serikali.

Aliongeza kuwa viongozi hao watakuwa wameshiriki moja kwa moja katika kuushusha mkoa huo kiutendaji, ambao kwa sasa uko nafasi ya pili kitaifa kwa ujazaji wa mfumo wa PEPMIS, na kwa upande wa vyuo, Mkoa wa Morogoro ndio kinara.

“Ombi langu sasa, kila mmoja atimize wajibu wake anavyotakiwa… tujaze fomu hizo kwa mantiki kwamba kila mmoja anajaziwa kwa kile anachostahili,” alisisitiza Dkt. Mussa.

Mafunzo hayo ya PEPMIS yalianza tarehe 23 Juni 2025, yakitolewa na maofisa kutoka Ofisi ya Rais – Utumishi, yakiwahusisha makundi mbalimbali ya watumishi wa umma, hususan wakuu wa idara na vitengo kutoka halmashauri za mkoa huo, Sekretarieti ya Mkoa, na taasisi za umma zilizoko mkoani humo.

Mfumo wa utendaji kazi, yaani Performance Management Information System (PEPMIS), una lengo la kuongeza ufanisi na uwajibikaji kwa watumishi wa umma. Pia ni nyenzo muhimu ya kiutumishi inayosaidia mtumishi wa umma kuweka malengo yake ya utendaji kazi na kuyatekeleza ipasavyo.


MWISHO


Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • RAS MOROGORO AFUNGA MAFUNZO YA PEPMIS, ATAKA UWAJIBIKAJI NA UAMINIFU

    June 28, 2025
  • RC MALIMA AMUUMA SIKIO DC MVOMERO, KUTUMIA BUSARA ZAIDI.

    June 27, 2025
  • RC MALIMA AENDELEA NA MAONO YA KUKUZA KILIMO MKOANI MOROGORO.

    June 27, 2025
  • Maadhimisho ya miaka 80 hospitali ya Rufaa Morogoro yaanza kuleta Matokeo

    June 25, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.