• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Maelezo ya Mkoa

Utangulizi:

Wakati Tanganyika inapata uhuru wake tarehe 9 Desemba 1961, Mkoa wa Morogoro ilikuwa ni Sehemu ya Jimbo la Mashariki. Jimbo hilo lilijumuisha Mikoa ya sasa ya Dar es Salaam, Pwani na Morogoro.

Makao Makuu ya Jimbo yalikuwa Morogoro mjini ambapo pia Mkuu wa Jimbo aliweka makazi na Ofisi yake hapo. Mbunge wa kwaza Mwafrika kuongoza Jimbo hilo alikuwa hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Mkoa wa Morogoro ulianza rasmi mwaka 1962 ukiwa na Wilaya tatu ambazo ni Morogoro Kilosa na Ulanga. Ni Mkoa wa pili kwa ukubwa hapa nchini kwa sasa ukitanguliwa na Mkoa wa Tabora.

Mipaka na ukubwa wa Mkoa

Mkoa wa Morogoro ni Mkoa wa pili kwa ukubwa nchini ukitanguliwa na Mkoa wa Tabora. Mkoa una eneo la kilometa za mraba 73,039. Eneo hili ni sawa na asilimia 7.7 ya eneo lote la Tanzania Bara, kati ya eneo hili Km2 2,240 ni eneo la maji. Mkoa umepakana na Mikoa ya Pwani na Lindi kwa upande wa Mashariki, Manyara na Tanga kwa upande wa Kaskazini na kwa upande wa Magharibi umepakana na Mikoa ya Dodoma na Iringa na Upande wa Kusini unapakana na Mkoa wa Ruvuma na Njombe.

Hali ya Hewa

Mkoa hupata mvua mara mbili kwa mwaka. Mvua za vuli hunyesha kuanzia mwezi Oktoba hadi katikati ya mwezi Januari, na mvua za masika hunyesha katikati ya mwezi Februari na kuishia mwezi Mei mwishoni. Kiwango cha mvua ni kati ya milimita 600 katika sehemu za tambarare na milimita 1,200 katika miinuko. Hata hivyo, zipo sehemu zilizo na ukame ambazo hupata mvua chini ya milimita 600 kwa mwaka. Sehemu hizo ni pamoja na Tarafa za Gairo katika wilaya ya Gairo, Mamboya katika Wilaya ya Kilosa na Tarafa ya Ngerengere katika Wilaya ya Morogoro.

Utawala

Mkoa wa Morogoro kiutawala umegawanyika katika Wilaya saba ambazo ni Wilaya za Morogoro, Mvomero, Kilosa, Kilombero, Ulanga, Malinyi na Gairo.

Kufuatana na Muundo wa Serikali za Mitaa Mkoa una Halmashauri saba za Wilaya na Halmashauri ya Manispaa moja na halmashauri ya Mji wa Ifakara. Halmashauri za Wilaya ni pamoja na Kilosa, Gairo, Kilombero, Morogoro, Ulanga, Mvomero na Malinyi. Mkoa una majimbo ya Uchaguzi 11, Kata 214, Vijiji 673, Mitaa 295, vitongoji 3,452

Idadi ya watu

Kwa mujibu wa matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya kaya za Mkoa wa Morogoro ni 489,688 zenye watu 2,218,492 ambapo kati yao wanawake ni 1, 125,190 sawa asilimia 50.7 na wanaume ni 1,093,302. sawa na asilimia 49. Wastani wa idadi ya watu katika Kaya ni 4:5

WAKUU WA MKOA WA MOROGORO TANGU UHURU MWAKA 1961

 

NA.

JINA

CHEO

KUANZIA

KUISHIA

1.
Bw. Seleimani Kitundu (Mb)
Mkuu wa Mkoa
1962
1963
2.
Chifu Humbi Ziota (Mb)
Mkuu wa Mkoa
1963
1964
3.
Bw. Joseph Kapilima (Mb)
Mkuu wa Mkoa
1964
1965
4.
Bw. Edward Barongo (Mb)
Mkuu wa Mkoa
1965
1968
5.
Bw. Joseph Namata (Mb)
Mkuu wa Mkoa
1968
1971
6.
Bw. Anselm Lyanda (Mb)
Mkuu wa Mkoa
1971
1976
7.
Bibi Anna Margareth Abdallah (Mb)
Mkuu wa Mkoa
1976
1982
8.
Bw. Crisant Majiyatanga Mzindakaya (Mb)
Mkuu wa Mkoa
1982
1986
9.
Bw. Aaron Mhavile (Mb)
Mkuu wa Mkoa
1986
1990
10
Bw. Mustafa Nyang’anyi (Mb)
Mkuu wa Mkoa
1990
1991
11
Bw. Yusufu Rajabu Makamba (Mb)
Mkuu wa Mkoa
1991
1993
12
Bwana Gutram Mkolokoti Aman Itatiro (Mb)
Mkuu wa Mkoa
1993
1995
13
Dkt. Ahmed Mayanja Katorogo Kiwanuka
Mkuu wa Mkoa
1995
1996
14
Dkt. Lawrence Mtazama Gama (Mb)
Mkuu wa Mkoa
1996
2000
15
Alhaji Mussa Sekume kinanga Khangaa
Mkuu wa Mkoa
2000
2003
16
Bw. Stephen Joshua Mashishanga (Mnec)
Mkuu wa Mkoa
2003
2006
17
Said bin Said Kalembo (Meja Jeneral Mstaafu)
Mkuu wa Mkoa
2006
2009
18
Issa Salehe Machibwa
(Luteni Kanali Mstaafu)
Mkuu wa Mkoa
2009
2010
19
Dkt.  Joel Nkaya Bendera
Mkuu wa Mkoa
2010
2015
20
Dkt. Rajab Mtumwa Rutengwe
Mkuu wa Mkoa
2014
2015
21
Dkt. Kebwe Steven Kebwe
Mkuu wa Mkoa
2016
hadi sasa

 

 

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 - MKOA WA MOROGORO December 07, 2019
  • View All

Habari Mpya

  • RC SANARE AAGIZA TAKUKURU KUFANYA UCHUNGUZI WA MIL. 260

    January 24, 2021
  • NIMR YAANZA TAFITI ZA KUTIBU MALARIA.

    January 22, 2021
  • RC Morogoro atoa siku 11.

    January 21, 2021
  • WANACHI KIJIJI CHA WAMI LUHINDO WAHAMASIKA KUJENGA SHULE, WAOMBA SIKU YA HARAMBEE IPANGWE KARIBU.

    January 17, 2021
  • View All

Video

Anayetaka kumuheshimu Rais amuheshimu Mwananchi - RC Sanare
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.