• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Uchumi na Uzalishaji

KILIMO, MIFUGO, UVUVI, USHIRIKA, MALIASILI NA UTALII, MISITU NA MAZINGIRA

KILIMO

Mkoa wa Morogoro una eneo la hekta 2,226,396 linalofaa kwa Kilimo ambapo eneo linalolimwa kwa sasa ni wastani wa Hekta 960,034 sawa na asilimia 43. Eneo linalofaa kwa Kilimo cha Umwagiliaji ni hekta 1,510,339.51 na eneo linalomwagiliwa kwa sasa ni wastani wa hekta 79,429 sawa na asilimia 5. Mkoa una Skimu za Umwagiliaji 106 (asili na zilizoendelezwa) zinazotambulika zenye ukubwa wa hekta 323,758.15. 

Asilimia 75 ya Wananchi wa Mkoa wa Morogoro wanategemea kilimo kwa ajili ya Ajira, Kipato na Chakula. Mazao ya Chakula yanayozalishwa kwa wingi ni Mpunga, Mahindi, Ndizi, Viazi vitamu, Muhogo, Mtama na Maharage. Mazao ya biashara yanayozalishwa kwa wingi ni Miwa, Ufuta, Alizeti, Mkonge, Korosho, Pamba, Kokoa, Matunda, Viungo na Mboga mboga.

Idadi ya watumishi (Maafisa Ugani Kilimo) katika Mkoa

Mkoa wa Morogoro una jumla ya Maafisa Ugani Kilimo 462, mahitaji ni 960 na hivyo upungufu ni watumishi 498 kama ilivyo kwenye jedwali namba 20.

Jedwali Na. 1:  Idadi ya Watumishi wa Kilimo Waliopo Kwenye Halmashauri

H/Wilaya

Mahitaji ya Maafisa Ugani Kilimo

Waliopo

Upungufu

Gairo

  55

29

26

Mji Ifakara

78

49

29

Kilosa

184

89

95

Mlimba

81

34

47

Malinyi

65

23

42

Morogoro MC

34

33

1

Morogoro DC

192

73

119

Mvomero

179

102

77

Ulanga

87

26

61

RS Morogoro

5

4

1

Jumla

960

462

498

 

Malengo na Utekelezaji wa Mazao ya Chakula na Biashara

Katika msimu wa Kilimo wa mwaka 2021/2022, Mkoa ulilenga kulima hekta 940,509.07 ili kuvuna tani 3,035,485.96 za mazao ya chakula. Kwa mazao ya biashara Mkoa ulilenga kulima hekta 205,083.83 ili kuvuna tani 2,704,383.95.

Utekelezaji wake mazao ya chakula, Mkoa ulilima hekta 681,550.68 sawa na asilimia 72 ya lengo na kuvuna tani 1,775,511.71 sawa na asilimia 58 ya lengo. Kwa mazao ya biashara, Mkoa ulilima hekta 155,773.76 sawa na asilimia 76 ya lengo na kuvuna tani 1,743,853.87 sawa na asilimia 64 ya lengo. Kwa msimu wa 2021/2022-unyeshaji wa mvua uliathiri uzalishaji wa mazao kwani Mvua zilianza kwa kuchelewa na hazikunyesha kwa mtawanyiko mzuri na pia ziliwahi kuisha hivyo, kusababisha kutofikia malengo tuliyojiwekea.

Kwa msimu wa mwaka 2022/2023, Mkoa umelenga kulima hekta 938,448.30 ili kuvuna tani 3,068,101.58 za mazao ya chakula na Mazao ya biashara Mkoa umelenga kulima hekta 226,900.73 ili kuvuna tani 2,909,321.78.

Jedwal Na. 2: Mchanganuo wa Eneo Linalofaa kwa Kilimo na Eneo Linalolimwa

Halmashauri

Eneo linalofaa kwa Kilimo 

Eneo linalo lengwa kulimwa kwa sasa

% Eneo faa vs lengwa 

Mazao Makuu 5 yanayolimwa kwa wingi  kwa sasa

  Mazao ya Kipaumbele

Gairo
111,080.4
 100,610.72
91%

Mahindi, Viazi vitamu, Maharage, Alizeti na Mbaazi.

Mahindi na Alizeti.

Ifakara (TC)
131,271.4
46,965.40
36%

Miwa, Mpunga, Mahindi, Ndizi na Muhogo

Mpunga na Miwa.

Kilosa
417,210
262,830.00
63%

Miwa, Mahindi, Mpunga, Viazi Vitamu na Mkonge.

Mkonge na Mpunga.

Malinyi
127,761.06
72,291.70
57%

Mpunga, Mahindi, Ufuta, Korosho na Viazi vitamu.

Korosho, Ufuta/

Mpunga

Manispaa (M)
8,004
6,145.33
77%

Mahindi, Ndizi, Nyanya, Vitunguu na Viungo

Nyanya na Mahindi

Morogoro (DC)
447,000
216,241.50
48%

Mpunga, Ndizi, Mahindi, Muhogo, Ufuta na Viungo

Mpunga na Ufuta/ Viungo

Mlimba
383,884.4
159,850.60
42%

Mpunga, Ndizi, Ufuta, Kokoa na Mahindi

Mpunga na Ufuta/ Kokoa

Mvomero
549,375
202,977.00
37%

Mpunga, Mahindi, Miwa, Maharage na Nyanya.

Mpunga/

Malisho

Ulanga
245,600
97,436.78
40%

Mpunga, Ufuta, Pamba, Kunde na Mahindi.

Korosho na Ufuta/ Karanga Miti

Chanzo: Takwimu kutoka Halmashauri, (2022)

Hali ya Chakula katika Mkoa kwa Msimu wa 2022/2023

Hali ya chakula kwa msimu wa 2022/2023 ni ya wastani katika Halmashauri zote za Mkoa wa Morogoro kutokana na mavuno ya msimu wa 2021/2022 ambapo Mkoa ulivuna tani 1,775,511.71 sawa na asilimia 58 ya lengo la kuvuna tani 3,035,485.96 ya mazao yote ya chakula. Uzalishaji wa Mazao ya chakula ulishuka kwa asilimia 42 ya lengo kutokana na mvua kuchelewa kuanza, kuwa na kipindi kirefu cha jua na mvua kuisha mapema wakati mazao bado hayajakomaa. Hata hivyo, Halmashauri zote zilivuna Mazao ya chakula kwa utoshelevu hadi ziada.

Jedwal Na. 3:  Uzalishaji wa mazao ya chakula kwa kila Halmashauri 2021/2022

Halmashauri

Malengo

Utekelezaji wa Malengo

Eneo lengwa (ha)

Makisio ya uzalishaji (tani)

Eneo lililolimwa (ha)

% ya lengo la hekta

Uzaliishaji (tani)

% ya uzalishaji

Gairo

79,727.67

218,233.14

61,161.29

77%

84,787.43

39%

Ifakara

39,295.60

180,507.40

32,965.70

84%

86,146.90

48%

Mlimba

135,565.50

419,519.30

121,171.50

89%

385,099.00

92%

Kilosa

191,077.00

579,610.00

111,260.00

58%

265,373.00

46%

Malinyi

73,995.70

219,696.08

61,973.00

84%

132,597.45

60%

Morogoro (DC)

174,547.00

564,142.70

158,870.00

91%

448,819.17

80%

Morogoro (MC)

5,751.16

23,085.62

5,648.88

98%

13,104.84

57%

Mvomero

163,177.00

545,837.00

73,456.00

45%

211,604.00

39%

Ulanga

77,372.44

284,854.72

55,044.31

71%

147,979.93

52%

Mkoa

940,509.07

3,035,485.96

681,550.68

72%

1,775,511.72

58%

Chanzo: Takwimu kutoka Halmashauri, 2022

Aidha, kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 idadi ya watu katika Mkoa wa Morogoro ni 3,197,104. Kutokana na idadi hiyo ya watu mahitaji ya Chakula kwa mwaka 2022/2023 yalikadiriwa kuwa tani 758,512.92 na kufanya Mkoa kuwa na ziada ya chakula tani 1,016,998.79 bila Mlinganisho wa Nafaka. Kuanzia Mwaka 2014/2015 hadi 2021/2022 Mkoa umekuwa ukijitosheleza kwa chakula na kuwa na ziada ni kama ifuatavyo.

Jedwal Na. 4: Uzalishaji na Mahitaji ya Chakula 2014/2015 Hadi 2021/2022

Mwaka

Eneo lililo limwa (He)

Uzalishaji (Tani)

Mahitaji ya chakula (Tani)

Ziada (Tani)

2014/2015

589,231.00

1,877,942.1

565,779.35

1,312,162.75

2015/2016

563,826.18

1,597,895.65

578,446.05

1,019,449.60

2016/2017

738,282.00

2,298,859.00

591,112.76

1,707,746.24

2017/2018

808,669.00

2,262,227.00

603,779.46

1,658,447.54

2018/2019

784,320.90

2,229,745.92

616,446.16

1,613,299.76

2019/2020

758,568.90

2,016,332.20

629,112.86

1,387,219.34

2020/2021

735,230.97

2,113,776.38

651,573.91

1,462,202.47

2021/2022

681,550.68

1,775,511.71

758,512.92

1,016,998.79

2022/2023
Mkoa umelenga kulima Hekta 938,448.30 ili kuvuna tani, 3,068,101.58 za mazao ya chakula.

Chanzo: Taarifa kutoka Halmashauri za Mkoa wa Morogoro 2014/2015 Hadi 2022/2023

Jedweli Na. 5: Wastani wa Bei za Vyakula Sokoni

Aina ya mazao

Bei (Tsh.) Desemba, 2022

Bei (Tsh.) Januari 2023

Bei (Tsh.) Februari 2023

Gunia la Mahindi (Kg 100)

120,245/=

120,245/=

105,450/=

Gunia la Mpunga (Kg 100)

132,812.50/=-

187,500/=

187,500/=

Unga wa Sembe (Kg 1)

2,000/=

2,000/=

2,000/=

Unga wa Ngano (Kg)

2,000/=

2,000/=

2,000/=

Mchele (Kg 1)

2,800/=-3,400/=

2,800/=3,400/=

2,800/=3,400/

Maharage (Kg 1)

3,000/=

3,200/=

3,200/=-3,400/=

Mkungu wa Ndizi

15,000/=

15,000/=

15,000/=

Viazi mviringo (Kg 1)

1,000/=

1,000/=

1,200/=

Viazi vitamu (Fungu)

2,000-3,000/=

2,000-5,000/=

2,000-5,000/=

 Uzalishaji wa Mazao ya Chakula 2021/2022

Mwenendo wa Mvua na Utekelezaji wa Malengo ya Kilimo Msimu wa 2022/2023

Mvua za Vuli na Masika msimu wa 2022/2023 zilitabiriwa kuwa za Chini ya Wastani hadi Wastani. Mvua hizo zilitabiriwa kuanza kwa kuchelewa, zenye mtawanyiko usioridhisha na kuambatana na vipindi virefu vya ukavu. Mvua hizo zlinyesha kama ilivyotabiriwa ambapo mvua za vuli zilianza kwa kuchelewa mwishoni mwa mwezi Novemba, 2022 na hazikua na mtawanyiko mzuri na kuambatana na vipindi virefu vya ukavu (jua) hivyo, kusababisha wakulima wachache kuanza kilimo katika kipindi hicho.

Hata hivyo, kuanzia wiki ya pili ya Mwezi Desemba, 2022 hadi wiki ya tatu Mwezi Januari, 2023 mvua ziliongezeka na kufanya wakulima wengi kuandaa mashamba na kupanda mazao mbalimbali. Hata hivyo, Mwezi Februari hadi mwishoni mwa Mwezi Machi, 2023 mvua ilisimama na kusababisha Mazao yaliyopandwa kunyauka na jua.

Mazao yaliyoathirika zaidi ni nafaka (hasa Mahindi) ambayo yalipandwa kipindi cha mvua za vuli na masika. Halmashauri zinazozalisha mahindi kwa wingi kama Gairo, Kilosa, Morogoro na Mvomero ndizo zimeathirika sana ukilinganisha na Halmashauri zinazozalisha zao la mpunga kwa wingi ambazo ni Mlimba, Malinyi, Ulanga na Ifakara ambapo baada ya Mvua kuanza kunyesha mwezi Aprili Mpunga umeimarika.

Aidha, Eneo lililokuwa limelengwa kulimwa mazao ya chakula ni hekta 938,448.30 ambapo hadi kufikia tarehe 31 Machi, 2023 eneo lililokuwa limelimwa ni hekta 746,668.26 sawa na asilimia 79 ya lengo na kati ya eneo lililolimwa hekta 225,151.98 sawa na asilimia 30.2 zimeathirika na athari za Ukavu wa muda mrefu.

Jedweli Na. 6: Tathimini ya eneo lililoathirika kwa Mazao ya Chakula katika Halmashauri

Halmashauri

Eneo lengwa (Ha)

Eneo lililolimwa

Eneo lililoathirika (Ha)

Asilimia ya Eneo lililoathirika

Gairo
  79,527.65
55,195.85
23,894.4

43%

Ifakara
  39,295.60
26,322
490.2

2%

Mlimba
148,279.00
143,067.8
32,190.26

22%

Kilosa
190,191.00
162,447
61,442

38%

Malinyi
  69,104.00
66,313
17,241.38

26%

Morogoro (DC)
168,710.00
112,948
28,719.2

25%

Morogoro (MC)
    5,792.16
5,075.61
2,537.8

49%

Mvomero
163,254.00
114,278
53,253.5

46.6%

Ulanga
  74,294.89
61,021
5,383.24

9%

Jumla Mkoa 
938,448.30
746,668.26
225,151.98

30.2

 

Hali ya chakula tarajiwa kwa msimu wa 2022/2023 kutokana na tathmini hiyo, Halmashauri zote za Mkoa wa Morogoro zinatarajiwa kuwa na utoshelevu wa chakula hadi ziada isipokuwa Halmashauri za Gairo, Kilosa na Mvomero zinaweza kuwa na upungufu wa chakula kwa baadhi ya Kata zinazotegemea sana zao la Mahindi kama zao kuu la chakula. Hata hivyo, maeneo mengi Wakulima walishauriwa kufyeka Mahindi yaliyoathirika zaidi na kupanda upya mazao ya muda mfupi pamoja na mazao jamii ya mizizi baada ya Mvua kuanza kunyesha mwezi Aprili.

 Hatua zilizochukuliwa kukabiliana na Athari za Ukavu wa Muda Mrefu

Halmashauri zilishauriwa kuwanunulia wakulima mbegu za mazao ya muda mfupi na kupandwa kwenye maeneo yaliyoathirika zaidi na ukame. Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero ilinunua jumla ya tani 3 za Mbegu za Mahindi ya muda mfupi (DK 777) na kugawa kwa Wakulima 750 wa Vijiji vya Kata ya Kibati.

Kuendelea kutoa elimu ya uhifadhi na matumizi bora ya chakula kwa mazao yatakayovunwa ili kujihakikishia usalama wa chakula kwa Msimu ujao.

Kuhamasisha Wakulima kulima mazao yenye kustahimili ukame na yanayo komaa kwa muda mfupi kama vile Viazi Vitamu, Mihogo, Mikunde, Mtama na Mahindi ya muda mfupi.

Kuwashauri Wakulima wafugaji kupunguza mifugo kwa kuuza na kununua chakula.

Kubaini Maeneo/kaya zilizoathirika zaidi na ukame ili kushirikiana na Wizara ya kilimo kuangalia uwezekano wa Maeneo/kaya hizo kupata mahindi ya chakula kwa bei nafuu kutoka kwa Wakala wa Hifadhi ya Chakula nchini (NFRA) kwa ajili ya kupunguza makali ya bei ya vyakula katika maeneo husika. Ambapo, Mwezi Machi, 2023 Halmashauri ya Wilaya ya Gairo ilipokea jumla ya tani 65 za Mahindi ya bei nafuu.

Mahitaji ya Pembejeo za Kilimo

Mbolea 

Wizara ya Kilimo kupitia Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (Tanzania Fertilizer Regulatory Authority –TFRA) imeandaa utaratibu wa mfumo wa kielektroniki katika kutoa ruzuku ya mbolea kwa lengo la kuongeza ufanisi wa utoaji wa ruzuku, kupunguza mianya ya udanganyifu na gharama za usimamizi. Mfumo huo unatumia programu maalum ya kidigitali kusajili wakulima, wasambazaji/wazalishaji, mawakala pamoja na kuratibu usambazaji wa mbolea kwa wakulima na malipo ya mbolea ya ruzuku.

Utekelezaji wa Rukuzu ya Mbolea katika Mkoa wa Morogoro

Mkoa wa Morogoro umepokea jumla ya Vitabu 3,120 kwa ajili ya kusajili Wakulima ambapo kitabu kimoja kina uwezo wa kusajili (kuandikisha) wakulima 384 hivyo, Mkoa umepokea vitabu vyenye uwezo wa kusajili wakulima 1,198,080. Mkoa umelenga kusajili Wakulima 388,928 ambapo hadi kufikia Aprili 18, 2023, jumla ya wakulima 124,860 walikuwa wamesajiliwa sawa na asilimia 32 ya lengo ambapo kati yao Wakulima 15,752 wamenufaika na Ruzuku ya Mbolea sawa na asilimia 13 ya wakulima waliosajiliwa hata hivyo, usajili wa Wakulima bado unaendelea.

    

Mkoa una jumla ya Makampuni 4 (ETG, Minjingu, TFC na ITRACOM) na mawakala 24 wanaosambaza na kuuza Mbolea kwa Wakulima kwa bei ya Ruzuku isiyozidi shilingi 70,000/= kwa mfuko wa Mbolea wa kilo 50. Vilevile kuna Vyama vya Ushirika 8 vinavyojishughulisha na Kilimo cha miwa katika Bonde la Kilombero ambavyo vinasambaza mbolea. Mahitaji ya mbolea katika Mkoa wa Morogoro kwa msimu wa kilimo 2022/2023 yalikuwa jumla ya tani 27,440.

Hadi kufikia tarehe 18 Aprili, 2023, jumla ya tani 7,976.300 zenye thamani ya shilingi 18,281,872,993 zilinunuliwa kupitia mpango wa Ruzuku kati yake Shilingi 7,522,980,993 ni Mchango wa Serikali (Ruzuku) na Shilingi 10,758,892,000 ni mchango wa Wakulima. Uwepo wa Ruzuku kwenye Mbolea umesababisaha Mahitaji ya Mbolea kuongezeka kutoka tani 27,440 mwaka 2022/2023 hadi tani 36,406 kwa mwaka ujao wa 2023/2024 kama majedwali ya Mahitaji ya Mbolea yanavyoonesha hapo chini.

Jedweli Na. 7: Taarifa ya Matumizi ya Mbolea kwa Mwaka 2021/22 na Makisio ya Mahitaji ya Mbolea kwa Mwaka 2022/23

Halmashauri

Aina ya Mbolea

Matumizi 2021/22 (Tani)

Makadirio ya Mahitaji 2022/23 (Tani)

KILOSA
DAP

600

1,195

UREA

750

1,354

NPK

58

100

CAN

18

20

SA

4

5

Jumla ndogo

1,430

2,674

MALINYI
DAP

5

42

UREA

43

102

NPK

6

16

CAN

16

30

SA

5

30

Jumla ndogo

76

220

MVOMERO
DAP

1,336

2,162

UREA

1,829

3,120

SA

528

1,306

Yara Cereal

15

50

Yara mila winner

12

40

Yara Nitrabor

6

20

Yara sulfan 

12

40

Yara Amidas

45

150

Yara Otesha

15

50

Samadi

131

130

Booster

228

351

Jumla ndogo

4,157

7,419

Gairo
DAP

23

100

UREA

43

100

CAN

17

50

Jumla ndogo

83

250

MOROGORO
DAP

54

1,000

UREA

120

1,000

CAN

96

200

NPK

-

5

YARA CEREAL

55

30

YARA AMIDAS

48

30

Jumla ndogo

373

2,265

MLIMBA
DAP

6

851

UREA

14

1,898

CAN

10

1,265

YARA VELA AMIDAS

32

1,582

Yara Otesha

20

681

SA

14

949

Booster

3

10

YARA CEREAL

3

633

MOP

5

316

Jumla ndogo

108

8,185

MANISPAA
UREA

290

295

DAP

150

215

CAN

70

80

SA

45

45

YARAWINNER

195

YARACEREAL

30

YARAOTESHA

145

OCP

90

SULFANI

45

MOP

10

10

MAGNISIUM

10

10

CALICINITY

30

35

NITRABOR

30

35

AMIGRAN

20

25

AMIDAS

25

KYNOPLAS

10

10

Jumla ndogo

665

1,290

IFAKARA
DAP

115

834

UREA

492

1,050

SA

9

50

CAN

55

100

YARA AMIDAS

35

101

YARA CEREAL

50

99

Jumla ndogo

755

2,234

ULANGA
DAP

210

401

UREA

650

898

CAN

460

665

SA

600

649

NPK

290

290

Jumla ndogo

2,210

2,903

JUMLA KUU

9,857

27,440

Chanzo: Takwimu kutoka Halmashauri 2021/2022

 

Jedweli Na. 8: Mchanganuo wa Mahitaji ya Mbolea kwa Msimu ujao wa 2023/2024

NA.

HALMASHAURI

AINA YA MBOLEA (TANI)

DAP

UREA

CAN

SA

NPK

MINJINGU

ITRACOM

JUMLA

1.
GAIRO

1,611

2,025

741

565

73

-

-

5,016

2.
IFAKARA

699

6,515

2,764

-

323

285

-

10,586

3.
KILOSA

973

3,676

767

10

151

-

3

5,579

4.
MALINYI

47

127

30

-

-

-

-

204

5.
MANISPAA

447

705

100

15

345

4

-

1,616

6.
MOROGORO

765

765

-

-

20

-

-

1,550

7.
MLIMBA

817

1,597

286

78

155

193

-

3,125

8.
MVOMERO

2,162

4,324

-

1,081

-

33

-

7,600

9.
ULANGA

185

785

75

30

55

-

-

1,130

JUMLA MKOA

7,706

20,520

4,763

1,778

1,121

515

3

36,406

Chanzo: Takwimu kutoka Halmashauri 2022/2023

Mbegu Bora

Mahitaji ya Mbegu bora za Mazao ya chakula na Biashara ni kama ilivyo kwenye Jedwali lifuatalo hapo Chini.

Jedweli Na. 9: Mahitaji ya Mbegu bora za Mazao kwa Msimu wa 2022/2023

Mbegu bora ya Zao la

Mahitaji ya Mbegu (Tani/Miche)

Mpunga

5,538.88

Mahindi

8,942.21

Ufuta

136.99

Alizeti

320.10

Korosho

Miche 639,275

Mkonge

Miche 52,005,600

Karafuu

Miche 1,480,867

Kokoa

Miche 1,625,312.5

Nyanya

1.5

Chanzo: Takwimu kutoka Halmashauri 2021/2022

Viuatilifu

Katika msimu wa Kilimo 2022/2023, Mkoa umekabiliwa na uwepo wa visumbufu vya mazao aina ya Panya waharibifu, Viwavijeshi na viwavijeshi vamizi ambavyo vimeshambulia mazao mbalimbali. Mkoa uliomba kiasi cha lita 40,500 aina ya Powercron 720 EC (Profenofos 720g/l) kutoka Wizara ya Kilimo (Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu - TPHPA) ambapo kiasi cha lita 8,400 zilipokelewa katika Halmashauri za Gairo (lita 3,000), Kilosa (lita 1,400) na Morogoro DC (lita 4,000). Aidha, Wataalam kutoka Wizara ya Kilimo kitengo cha Udhibiti wa panya waharibifu wa Mazao baada ya kupokea taarifa ya Uwepo wa Panya katika Mkoa wa Morogoro walifika katika Halmashauri za Ulanga, Mlimba na Malinyi kwenda Kudhibiti Panya waharibifu wa Mazao.

Kilimo cha Umwagiliaji

Mkoa una eneo linalofaa kwa Kilimo cha Umwagiliaji lenye ukubwa wa hekta 1,510,339.51. Eneo linalomwagiliwa kwa sasa ni wastani wa hekta 79,429 sawa na asilimia 5. Mkoa una Skimu za Umwagiliaji 106 (asili na zilizoendelezwa) zinazotambulika zenye ukubwa wa hekta 323,758.15. 

Miradi ya umwagiliaji inayotekelezwa 2022/2023

Kwa mwaka wa fedha 2022/2023, Mkoa unaendelea na utekelezaji wa miradi minne (4) ya Umwagiliaji katika Wilaya tatu (3) kama jedwali linavyoonesha hapo chini.

 

Jedweli Na. 10: Mchanganuo wa Miradi ya Umwagiliaji iliyopata Fedha katika Mkoa wa Morogoro

Wilaya

Mradi

Hatua ya Utekelezaji

Kiasi

Kilosa

Ujenzi wa skimu ya Rudewa

Mradi umefikia 25%. Mkandarasi yuko eneo la kazi na anaendelea na ujenzi.

7,202,268,404.00

Mvomero

Ujenzi wa skimu Kijiji cha Lukenge

Mradi unaendelea na utekelezaji. Mita 1200 kati ya 2750 sawa na 43% zimesakafiwa. Changamoto kubwa ni mahitaji ya pampu ili mradi uweze kutumika.

632,050,865.00

Mvomero

Ukarabati wa skimu ya Mgongola

Mradi umefikia 35%. Mkandarasi yuko eneo la kazi na anaendelea na ujenzi.

5,645,751,182.00

Kilombero

Ukarabati wa skimu ya Idete

Mradi umefikia 13% badala ya 55% iliyotarajiwa. Mkandarasi bado yuko kwenye hatua za awali za utekelezaji. Kasi ya utekelezaji hairidhishi

2,321,015,160.00

JUMLA

15,801,085,611.00

Chanzo: Taarifa za Kilimo Mkoa 2022/2023

Aidha, tarehe 28 Machi, 2023 Tume ya Taifa ya Umwagiliaji imetangaza zabuni kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mingine minne (4) ambayo mchakato wa manunuzi ya Wakandarasi bado unaendelea. Miradi hii ni Itete uliopo Halmashauri ya Malinyi, Tulo/Kongwa, Kiroka na Mbalangwe iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro. Gharama za miradi zitafahamika baada ya mchakato wa manunuzi kukamilika.

Zana za Kilimo

Mkoa wa Morogoro unajumla ya trekta 1,515, trekta ndogo (power tiller) 624 na maksai (majembe ya kukokotwa na wanyamakazi) 16,915 zinazotumika kulima wastani wa hekta 920,680.1. Kati ya hizo, hekta 578,061.80 zinalimwa kwa kutumia trekta, hekta 153,189.90 zinalimwa kwa Maksai, hekta 145,853.00 zinalimwa kwa jembe la mkono na hekta 43,575.40 zinalimwa kwa trekta ndogo. Takwimu hizi zinaashiria mwamko mkubwa kwa wananchi katika matumizi ya trekta katika uandaaji wa mashamba.

Jedweli Na. 11: Mchanganuo wa Zana kwa Halmashauri ni Kama Unavyoonekana Kwenye Jedwali

Na.

H/Wilaya

Matrekta

Powertiller

Maksao

1.

Gairo

42

8

47

2.

Ifakara TC

227

104

816

3.

Kilosa

274

143

1,872

4.

Malinyi

106

42

2,696

5.

Morogoro MC

250

11

5,000

6.

Morogoro DC

153

35

181

7.
Mlimba

174

194

194

8.
Mvomero

239

87

278

9.
Ulanga

50

-

5,831

JUMLA

1,515

624

16,915

Chanzo: Taarifa kutoka Halmashauri 2022/2023

Maghala ya Kuhifadhia Mazao

Mkoa una Jumla ya maghala 842 yenye uwezo wa kuhifadhi Jumla ya tani 476,726.8. Kati ya maghala hayo ya Serikali ni 79 na watu binafsi ni 763.

 

Jedweli Na. 12: Mchanganuo wa Maghala ya Kuhifadhia Mazao katika Halmashauri

Na.

H/Wilaya

Idadi ya Maghala

Uwezo wa Kuhifadhi (Tani)


Gairo

175

13,418


Ifakara TC

151

241,355


Kilosa

111

15,561


Malinyi

59

14,545


Morogoro MC

9

1,825


Morogoro

26

3,921


Mlimba

159

95,087


Mvomero

56

27,080


Ulanga

96

63,934.5

JUMLA

842

476,726.5

Chanzo: Taarifa kutoka Halmashauri 2022/2023

M – Kilimo

M – Kilimo ni mfumo wa kielektroniki unaotoa huduma za ugani na masoko kwa wakulima, wafugaji, wavuvi na wadau mbalimbali kwa kutumia simu ya mkononi. Lengo la mfumo huu ni kutatua changamoto ya uhaba wa Maafisa Ugani, upatikanaji wa masoko na kuunganisha wakulima, wafugaji, wavuvi na wadau wengine katika mnyororo wa thamani. Kwa kutumia mfumo huu, wakulima wanapata fursa ya kuuliza maswali kuhusu changamoto wanazokabiliana nazo na kupata majibu ya hapo kwa papo kutoka kwa Wataalam husika. Ili Mkulima aweze kutumi mfumo anapiga simu na. x152x00#.

Wizara ya Kilimo iliweka lengo la kusajili wakulima 419,776 kwa Mkoa wa Morogoro, mpaka kufikia Januari, 2023, wakulima 445,331 sawa na asilimia 106 ya lengo. Wanunuzi waliosajiliwa ni 1196, wauzaji 1,676 na wataalam wa Kilimo 503.

Kilimo cha Mashamba Makubwa

Katika kuhakikisha lengo la Wizara ya Kilimo la kukuza kilimo kwa asilimia 10 ifikiapo 2030 linafikiwa, moja ya eneo ambalo linatiliwa mkazo ni kuhamsisha kilimo cha Mashamba Makubwa kwa kuweka mazingira wezeshi kwa vijana kushiriki katika Kilimo. Hili linatekelezwa kupitia mradi wa Jenga Kesho Bora (Building a Better Tomorrow – BBT) ambapo Mkoa utatumia fursa ya mashamba yaliyofutwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dr. Samia Suluhu Hassan ili kuwawezesha Vijana kupata Ardhi ya Kilimo.

Hadi kufikia Aprili 2023, Mkoa wa Morogoro umepokea jumla ya vijana 124 katika vituo vya mafunzo vitatu; MATI Katrin Vijana 52, Chuo cha Sukari Kilombero vijana 15, MATI Ilonga vijana 57 ambapo wanapata mafunzo ya kilimo biashara katika mnyororo wa thamani wa mazao mbalimbali ya kilimo kabla ya kukabidhiwa ardhi kwa ajili ya kilimo.

Mashamba yaliyofutwa

Mheshimiwa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, mama yetu Samia Suluhu Hassan mnamo tarehe 2021 aliridhia ufutaji wa mashamba kumi na moja (11) yenye ukubwa wa ekari 24,119 yaliyopo katika Wilaya ya kilosa na Mashamba 2 (ekari 11,310) katika Halmashauri ya Mvomero. Aidha, Mhe. Rais aliridhia ugawaji wa mashamba 49 yaliyopo katika vijiji 23 Wilayani Kilosa yenye ukubwa wa ekari 45,788.5 ambayo milki zake zilitwaliwa na kubatilishwa katika vipindi mbalimbali ambayo uhakiki ulibaini sehemu kubwa ya mashamba hayo yanatumiwa na wananchi kwa shughuli mbalimbali ikiwemo kilimo na ufugaji. Wananchi wanaogawiwa sharti wawe wamejiunga kwenye vikundi ili kuondoa tabia ya wananchi kuuza maeneo.

Mazao ya Kimkakati

 

Mazao ya Viungo

Mkoa wa Morogoro ni miongoni mwa Mikoa inayozalisha mazao ya viungo kwa wingi kama vile karafuu, iliki, mdalasini, vanilla na pilipilimanga. Katika kuendeleza mazao ya viungo, Mkoa kwa kushirikiana na Halmashauri ya Morogoro wamefanya tathmini ya hali ilivyo kwa kukusanya takwimu za majina ya wakulima wa karafuu, ukubwa wa maeneo yanayolimwa, hali ya uzalishaji, bei, mahitaji ya miche na kubaini maeneo ya wazi kwa ajili ya kilimo cha mazao ya viungo. Jumla ya ekari 84,024 zimebainika kuwa zinafaa kwa kilimo cha mazao ya viungo. Takwimu zinaonyesha kuwa jumla ya ekari 17,219 zimepandwa karafuu, eneo linaloweza kulimwa Karafuu ni ekari 5,931, mdalasini ni ekari 2,263, iliki ni ekari 589 na pilipilimanga ni ekari 1,299. Mahitaji ya miche ya Karafuu ni 1,459,785. Mpaka mwishoni mwa Aprili 2023, Mkoa kwa kushirikiana na Kampuni Viridium na WWF imetoa miche ya karafuu 27,000 katika Halmashauri ya Morogoro na kusambazwa kwa wakulima bure katika msimu wa 2022/2023.

Zao la Korosho

Mkoa wa Morogoro ni moja kati ya Mikoa inayolima korosho nchini na umeendelea na utekelezaji wa Mpango wa maendeleo ya zao la Korosho katika Halmashauri nane kati ya tisa zilizopo na jumla ya wakulima 1,653 wamesajiliwa na Bodi ya korosho Tanzania kwa ajili ya kupewa vitambulisho vya wakulima wa zao la Korosho. Halmashauri za Wilaya zinazolima zao la Korosho ni Gairo, Kilosa, Malinyi, Morogoro, Mlimba, Mvomero Ulanga pamoja na Halmashauri ya Mji wa Ifakara. Mkoa una jumla ekari 36,840 zenye jumla ya Mikorosho 1,550,504.  Kati ya hiyo, mikorosho 408,159 imeanza kuzaa.

Katika msimu wa kilimo wa 2021/2022 Mkoa ulizalisha jumla ya tani 325.07 za Korosho na kuuzwa kwa mfumo wa stakabadhi ghalani.

Mpango/Makadirio ya Uzalishaji Kiwilaya Hadi Kufikia 2025/2026

Mkoa umejipanga kuongeza uzalishaji wa zao la Korosho kutoka tani 231 hadi kufikia tani 858.5 ifikapo mwaka 2025/2026 kama inavyoonekana katika jedwali.

Jedweli Na. 13: Mpango wa Uzalishaji zao la Korosho kwa miaka mitano ijayo 2021/2022 hadi 2025/2026

S/N
HALMASHAURI

MAKADIRIO YA UZALISHAJI (T)

2021/2022

2022/2023

2023/2024

2024/2025

2025/2026

1
Gairo

5

7

9

13

34

2
Ifakara

2.3

8.6

10.7

24.0

53.5

3
Kilosa

30

45

60

90

120

4
Malinyi

91

108

125

135

150

5
Mlimba

22.5

25.8

55

75

100

6
Morogoro

41

62

91

137

158

7
Mvomero

11

17

25

42

103

8
Ulanga

40

60

85

110

140

Jumla

231.8

333.4

460.7

626

858.5

 

Zao la Pamba

Katika Mkoa wa Morogoro Wilaya zinazozalisha zao la Pamba ni Kilosa, Gairo, Malinyi, Morogoro, Mvomero na Ulanga. Katika msimu wa 2021/2022 jumla ya hekta 2,565 zililimwa na kuzalisha jumla ya tani 1943.49. Pamba yote ilinunuliwa na Bodi ya pamba kwa wastani wa bei ya shilingi 1560 kwa kila Kilo ya Pamba. Katika Msimu wa 2022/2023 Mkoa umelenga kulima hekta 4,357 ili kuvuna tani 3481.20.

Zao la Mkonge

Mkoa wa Morogoro ni Miongoni mwa Mikoa inayozalisha kwa wingi zao la Mkongo nchini. Halmashauri zinazozalisha Mkonge katika Mkoa wa Morogoro ni Kilosa, Morogoro, Mvomero na Gairo. Hata hivyo, Halmashauri za Gairo na Mvomero hazijaanza kuvuna Mkonge zipo kwenye hatua ya kuhamasisha Wakulima na upandaji wa Mkonge. Maeneo yanayolimwa Mkonge ni wastani wa Hekta 10,573.55 na kuvuna wastani wa tani 12,216.91 kwa mwaka.

Wazalishaji wa Zao la Mkonge Katika Mkoa wa Morogoro

Jedweli Na. 14: Wazalishaji wakubwa na wakati wa zao la Mkonge katika Mkoa wa Morogoro ni kama ifuatavyo

 

Na.

 

Jina la Shamba

 

Mahali lilipo

Ukubwa wa shamba (Hekta)

Eneo lenye Mkonge

Wastani wa Mavuno kwa mwaka


Pangawe Highland Estate
Mkambarani Pangawe – Morogoro vijijini

3,698

1,472.65

2,061.71


FATEMI (Mohamed Enterprises Tanzania Limited)

Kidugalo – Morogoro Vijijini

6,412

3,637

5,819.2


M/S New kimamba Fbres Co. Ltd
Kimamba – kilosa

2,947

2,323.5

1,409


China State Farms Ltd
Rudewa – Kilosa

5,300

2,480

2,573


New Msowero Farm
Msowero – Kilosa

1,360

440

354


Igembe Nsabo - AMCOS
Rudewa – Kilosa

21.4

8.8

0


Josephat Rwezaura
Mkonowamara – Morogoro Vijijini

40

20

0


Mohamed Ramadhani
Mkonowamara – Morogoro Vijijini

80

80

0


Clement Munish ambae
Mkonowamara – Morogoro Vijijini

32

32

0


Wami Sokoine
Mvomero

40

40



Kimambila
Mvomero

11.2

11.2



Vianzi
Mvomero

20

20


 
Gairo
Gairo

8.4

8.4

 

JUMLA

19,970.00

10,573.55

12,216.91

Katika Wilaya ya Kilosa Ipo pia AMCOS ya Lukwambe ambayo imepatiwa na Serikali eneo la kulima Mkonge upandaji unaendelea. Aidha wananchi wanaendelea kugawiwa maeneo ili wajiunge kwenye AMCOS kwa ajili ya kilimo cha Mkonge.

Kilimo cha Kahawa

Zao la Kahawa lilikuwa linalimwa Katika Wilaya za Mvomero, Morogoro Gairo na Ulanga. Aina ya kahawa inayolimwa katika Mkoa wetu ni Robusta na Arabica. Ili kuhakikisha kuwa zao la Kahawa linafufuliwa Mkoa unashirikiana na Watafiti kutoka Taasisi ya utafiti wa kahawa Tanzania – TACRI na kutoa elimu ya kuzalisha zao la Kahawa kwa wataalam. TACRI kwa kushirikiana na Halmashauri za Ulanga, Gairo, Mvomero, Morogoro inatoa mbegu na miche kwa wakulima ili kuendeleza zao hilo. Jumla ya kata 28 na wakulima 2,104 wametambuliwa kuwa wakulima wa kahawa Kimkoa.

Ushiriki wa Wadau

Mkoa unashirikiana na wadau mbalimbali kutekeleza programu ya sekata ya kilimo katika Mkoa. Baadhi ya wadau hao ni SAGCOT, USAID, CAU, SAT, MVIWATA, MINJINGU nk.

Mapokezi ya Pikipiki kwa Maafisa Ugani wa Kilimo

Katika kuhakikisha sekta ya kilimo inakuwa na tija pamoja na kuongeza uzalishaji wa mazao ya kilimo, Serikali imeweka mikakati mbalimbali ya kuimarisha na kuboresha huduma za ugani nchini kwa kugawa vitendea kazi zikiwemo pikipiki, vifaa vya kupima afya ya udongo, vishikwambi na visanduku vya ugani kwa Maafisa Ugani kilimo nchini.

Mpango huu ulizinduliwa na Mheshimiwa Dr. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 4 Aprili, 2022. Mnamo mwezi Februari, 2023 Mkoa wa Morogoro ulipokea jumla ya pikipiki 436 kwa ajili ya Maafisa Ugani Kilimo kama ilivyo kwenye mchanganuo ufuatao (Jedwali Na. 23).

Jedweli Na. 15: Mchanganuo wa Maafisa Ugani Kilimo na Mgawanyo wa Pikipiki

Na.

H/Wilaya

Maafisa Waliopo

Wenye Pikipiki kutoka Taasisi za Kilimo/Halmashauri

Pikipiki zilizoletwa na mh Rais


RS Morogoro

4

1

3

1.
Gairo

29

3

26

2.
Mji Ifakara

49

2

52

3.
Kilosa

89

4

87

4.
Mlimba

34

3

34

5.
Malinyi

23

3

20

6.
Morogoro MC

33

6

20

7.
Morogoro DC

73

3

68

8.
Mvomero

102

3

99

9.
Ulanga

26

1

27

Jumla

462

29

436

Pikipiki zote 436 zimefungwa GPS ili kufuatilia utendaji kazi wa Maafisa ugani katika maeneo yao ya kazi ambapo Afisa ugani anapaswa kuitumia Pikipiki hiyo katika kituo chake cha Kazi na endapo atataka kutoka nayo nje ya Kituo chake cha kazi anapaswa kuomba ruhusa kwa Mkuu wake wa Idara.

Wito kwa Maafisa Ugani wote wa Mkoa wa Morogoro ni kuhakikisha wanazitumia Pikipiki hizo kwa shughuli za Ugani pekee ili kuhakikisha kuwa kilimo katika Mkoa wetu kinaboreshwa zaidi na kuchangia katika uchumi wa Mtu mmoja na Taifa kwa ujumla.

Changamoto ya Sekta ya Kilimo katika Mkoa wa Morogoro

Upungufu na Ubovu wa Miundombinu ya Umwagiliaji iliyopo, inachangia wakulima wengi kutegemea kilimo cha Mvua ambayo huwa haitabiriki na kusababisha wakulima wengi kushindwa kufikia malengo.

Upungufu wa Watumishi katika Idara za Kilimo, unaokwamisha utendaji kazi kwani baadhi ya maeneo muhimu hasa katika maeneo ya Kata na Vijiji hakuna Wataalam.

Uhaba wa Fedha za Ufuatiliaji, Fedha za usimamizi wa shughuli za Kilimo zinatolewa kidogo sana ukilinganisha na Mahitaji hasa katika ngazi ya Halmashauri.

Baadhi ya Halmashauri kutotoa asilimia 20 ya fedha za Mapato ya Ndani yanayotokana na Kilimo kw ajili ya uendelezaji wa Sekta ya Kilimo (miundombinu ya Umwagiliaji, Mbegu bora, Maghala na WARC) kitendo hicho kinachangia Sekta ya Kilimo kuonekana siyo kipaumbele wakati ndio inategemewa katika ukusanyaji wa Mapato ya Halmashauri hizo.

Kutokuwa na Mafunzo Rejea (On Job Training) kwa Wataalam wa Kilimo hivyo, kusababisha baadhi ya Wataalam kutoendana na teknolojia za kisasa hivyo, kulalamikiwa na Wananchi.

Mikopo kwa Wakulima, taasisi za mkopo (Mabenki) kuwa na masharti yasiyorafiki kwa Wakulima hivyo, kusababisha Wakulima kuendelea kunyonywa na Madalali ambao Wakati wa Kulima na Palizi kipindi ambacho wakulima hawana hela wanakopeshwa fedha na madalali kwa kigezo kuwa Mkulima akivuna mazao atamlipa Mazao badala ya fedha hasa kwa zao la mpunga.

Kutokuwa na bei ya kueleweka ya mazao ya Nafaka (Kupanda na kushuka kwa bei bila mpangilio) Price fluctuation. Kunasababisha wakulima kushindwa kupanga bei ya mazao ili wapate faida.

Maeneo ya kuhifadhia mazao (Maghala) ni machache hivyo, kusababisha wakulima kuuza bila mpangilio.

Uingizaji wa Mbegu za mazao za Nafaka kutoka nje ya nchi kunachangia kupotea kwa mbegu nzuri za asili.

Baadhi ya mawakala waliosajiliwa kupitia mfumo wa Mbolea ya Ruzuku kupitia TFRA kutokuwa na uwezo wa kimtaji wa kuuza mbolea kusababisha wakulima wengi kufuata mbolea kwa umbali mrefu maeneo ya Mjini na kuona kuwa ni kero.

Namna ya kutatua baadhi ya changamoto hizo ni kama ifuatavyo;

Kuimarisha AMCOS kwa ili wakulima waweze kuhifadhi mazao kwa pamoja na kutafuta masoko ili kuuza mazao kwa bei nzuri.

Kuimarisha Miundombinu ya Kuhifadhia mazao (Maghala) ambapo Halmashauri zimeshauriwa kutumia mapato ya ndani (asilimia 20 ya mapato yanayotokana na kilimo) kujenga maghala angalau kila Kata kuwe na ghala na vifaa vyote muhimu vinavyo hitajika ikiwemo kipima unyevu (Moisture meter) ili wakulima waweze kuhifadhi mazao na kuuza kwa pamoja.

Kutumia fursa ya Mhe. Rais kutoendeshwa na Wahisani (Donors) kwa kupigania Sera zetu badala ya kufuata wanachotaka wao.

Kutozuia mazao ya Chakula kuuzwa nje ya Mkoa na nje ya nchi ili wakulima kuuza kwa faida.

Kuwe na vituo maalum vya kuuzia Nafaka kwa kila Kijiji/Kata ili kudhibiti Madalali na ubora wa mazao ya Nafaka.

Kutoa elimu kwa wakulima ili wauze mazao yao kwa njia ya Minada ya Soko la bidhaa (TMX) badala ya kuuza mmoja mmoja.

Kuainisha Vituo vya Kuuzia Mbolea kulingana na Mahitaji ili Msimu wa Kilimo wa 2023/2024 Wakulima wapelekewe Mbolea katika Maeneo yao.

Pamoja na changamoto hizo, tunamshukuru Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa Vitendea kazi (Pikipiki) kwa Maafisa Ugani Kilimo na Ruzuku ya Mbolea kwa Wakulima, kwani mwamko umekuwa mkubwa sana Wakulima wengi wamelima mazao mbalimbali kutokana na kupunguziwa bei ya Mbolea pia Wataalam wanawafikia Wakulima kwa urahisi kutatua changamoto zao.

MIFUGO

Mkoa wa Morogoro unakadiriwa kuwa na Ng’ombe 1,129,883, Mbuzi 468,210, Kondoo 185,487 na Punda 9,026. Kwa kuzingatia idadi hiyo ya mifugo, Mkoa unahitaji wastani wa eneo la malisho lenye ukubwa wa hekta 1,269,668. Hivyo kwa eneo lililopo la hekta 323,686 ambalo limepimwa, Mkoa una upungufu wa zaidi ya hekta 945,982.59 za Malisho.

Jedweli Na. 16: Idadi ya Mifugo na Maeneo ya Malisho kwa kila Halmashauri, 2022

Na.

 

Halmashauri

Idadi ya Mifugo

 

Ukubwa wa Eeneo la Malisho pimwa

Ng’ombe
Mbuzi
Kondoo
Punda
1.
Morogoro DC

204,836

103,048

43,504

1,113

38,548

2.
Mvomero

212,154

90,080

13,627

2,128

10,385.

3.
Kilosa

328,169

131,854

42,675

3,753

225,150

4.
Malinyi

130,048

41,218

31,767

169

14,119

5.
Mlimba

103,783

28,287

26,457

126

5,395

6.
Gairo

45,494

45,310

11,811

1,426

86.6

7.
Ulanga

80,634

18,367

10,484

238

21,720

8.
Ifakara

15,739

4,854

3,778

73

8,282

9.
Manispaa

9026

5192

1384

0

0

JUMLA

1,129,883

468,210

185,487

9,026

323,686

Chanzo: Taarifa kutoka Halmashauri, 2022

Miundombinu ya Mifugo

Mkoa una jumla ya Minada 35, Majosho 71, malambo 42, mabanio 23, Machinjio 19, Makaro 51, Mabanda ya ngozi 8, Maabara 2, vituo vinavyotoa huduma ya mifugo (vet centre) 28 na Hospitali ya mifugo 1.

Majosho 45 yanafanya kazi na 23 ni mabovu. Katika Mwaka wa fedha 2022/2023 majosho mapya 32 yenye jumla ya shilingi 736,000,000/= yamepangwa kujengwa katika Halmashauri 8 za mkoa wa Morogoro kwa fedha kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi.

Jedweli Na. 17: Mahitaji ya Majosho katika Mkoa wa Morogoro

Na
Halmashauri

Mahitaji

Yaliyopo

Yanayofanyakazi

Mabovu

1
Mvomero

31

14

10

4

2
Ulanga

14

6

4

2

3
Mlimba

8

3

3

0

4
Gairo

20

18

11

7

5
MoroDC

39

12

8

4

6
Ifakara

4

3

1

1

7
Kilosa

51

12

7

3

8
Malinyi

14

2

1

1

9
Manispaa

2

1

0

1

 
JUMLA

183

71

45

23



Mikakati ya Kuboresha Sekta ya Mifugo Mkoa Wa Morogoro

Mkoa umeweka mikakati ya kufuga mifugo kisasa kwa kuzingatia eneo lililopo ili kufuga kwa tija na kupunguza uharibifu wa mazingira na kumuingiliano kati ya wafugaji na wakulima.

Kuwahamasisha wafugaji kutumia Ranchi ndogo ndogo katika kufuga mifugo yao. Mkoa utatumia maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya mifugo kuwapanga wafugaji katika Ranchi ndogondogo.

Unenepeshaji wa mifugo na kupeleka katika kiwanda cha nyama cha Nguru Hill ambacho kina uwezo wa kuchinja ngombe 100 na mbuzi 1,000 kwa siku. Uwepo wa kiwanda hiki utasaidia wafugaji kuvuna mifugo yao na kuuza kwa faida.

Unenepeshaji wa mifugo utafanyika kwa hatua 2, hatua ya kwanza Katika kila Halmashauri kutakuwepo na ranchi zisizopungua 5 zenye ukubwa wa hekta 500 kila moja ambazo zitatumika kunenepesha mifugo inayotoka kwa wafugaji wa kawaida. Mifugo ikitoka katika hatua ya kwanza itapelekwa hatua ya pili ya unenepeshaji kwenye eneo lililotengwa na mkoa lililopo Wilaya ya Mvomero lenye ukubwa wa Ekari 30,000. Baada ya kutoka katika hatua hii mifugo itauzwa kiwandani ikiwa na uzito wa zaidi ya kilo 250 ambao ndio unaokubalika na kiwanda

Kila Halmashauri kuhakikisha kwamba Wafugaji wanafuga mifugo yao kisasa kwa kuzingatia eneo lililopo ili kufuga kwa tija na kupunguza uharibifu wa mazingira.

Kila Halmashauri kuanzisha mashamba darasa ya Malisho na kutumia mashamba hayo kuwafundisha na kuwahamasisha wafugaji kuzalisha malisho.

Kila Halmashauri kuwahamasisha Wafugaji kuboresha Kosaafu za mifugo yao kwa kutumia madume bora yatakayosambazwa na Wizara ya Mifugo kupitia vikundi vya wafugaji.

 

 

 

 

UVUVI

Katika Mkoa wa Morogoro sehemu kubwa ya uvuvi hufanyika kutokea kwenye  kambi za wavuvi kandokando ya mto Kilombero. Kuna  aina  zaidi ya 52 ambapo  zaidi ya 90% ya samaki wote wanapatikana kutokea mto Kilombero. Baadhi ya aina hizo ni  Kitoga, Kambale, Perege, Njege, Ndungu, Bura, Ningu, Mgundu, Mbala, Mjongwa, Ngulufi, Mbewe, Ngogo, Sulusulu na Mkunga. Uvuvi mwingine kwa kiwango kidogo hufanyika katika mabwawa ya asili, ya kuchimbwa na mito imwagayo maji yake katika bonde la mto Rufiji.

Ufugaji wa Samaki katika Mkoa

Mkoa umeendelea kutoa elimu na kuhamasisha wananchi kufuga samaki katika mabwawa ya kuchimbwa ili kuongeza upatikanaji wa samaki Mkoani na pia kupunguza utegemezi katika vyanzo vya asili. Kutokana na uhamasishaji huo Mkoa kwa sasa una jumla ya mabwawa ya kuchimbwa 857 yanayokadiriwa kuzalisha zaidi ya tani 30 kwa mwaka. Mchanganuo wa mabwawa ya samaki kwa kila Halmashauri ni kama inavyoonyesha katika jedwali Na. 1 hapo chini.

Jedweli Na. 20: Mabwawa ya Samaki katika Halmashauri

Na.

HALMASHAURI

IDADI

1.
Ifakara

37

2.
Mlimba

25

3.
Kilosa

230

4.
Malinyi

15

5.
Morogoro MC

175

6.
Morogoro DC

146

7.
Mvomero

104

8.
Ulanga

90

9.
Gairo

35

JUMLA

857

Chanzo: Taarifa kutoka Halmashauri

 

Uzalishaji wa Samaki katika Mkoa

Katika kuongeza uzalishaji wa samaki Mkoani, elimu ya ufugaji wa samaki imekuwa ikitolewa kwa wananchi na udhibiti wa uvuvi haramu kwenye vyanzo vya asili umekuwa ukifanyika kwa kutumia doria, elimu na vikundi vya ulinzi wa rasilimali ya uvuvi (BMUs). Hivyo kutokana na vyanzo vilivyopo Mkoani, msimu wa mwaka 2021/2022 uzalishaji ulikuwa tani 192.3 zenye thamani ya shilingi 972,555,110 ikilinganishwa na mwaka 2020/2021 ambapo uzalishaji ulikuwa tani 279.5 zenye thamani ya shilingi.1,307,018,617.75. 

 

Uzalishaji umepungua kwa kiasi kikubwa kwa sababu sehemu kubwa ya bonde la Mto Kilombero lilikuwa pori tengefu na sasa limekuwa pori la akiba na hivyo kusababisha wavuvi wengi kushindwa kuingia kuvua samaki kutokana na masharti yaliyowekwa hususani viwango vya tozo ambavyo wengi wao wanashindwa kuvimudu. Mchanganuo wa uzalishaji kwa kila Halmashauri kwa kipindi cha miaka 2 ni kama inavyoonyesha katika jedwali Na. 2 hapo chini.

 

 

Jedweli Na. 21: Mavuno ya Samaki kwa Msimu wa Mwaka 2020/2021 ikilinganishwa na Mwaka 2021/2022 katika Halmashauri

Na.

HALMASHAURI

2020/2021

2021/2022

UZITO (tani)

THAMANI (Tsh)

UZITO (tani)

THAMANI (Tsh)

1.

Mlimba

89.2

369,178,217.75

32.6

125,333,110

2.

Kilosa

47.6

237,930,000.00

51

305,340,000

3.

Morogoro MC

12.1

72,357,500.00

11

20,389,500

4.

Ulanga

32.9

132,228,250.00

22

111,881,150

5.

Mvomero

4.4

21,930,000.00

3.8

23,279,000

6.

Morogoro DC

2.1

11,312,000.00

1.3

7,608,000

7.

Ifakara Mji

41.4

239,144,200.00

43.8

251,912,500

8.

Malinyi

49.8

222,938,450.00

26.8

126,811,850

9.

Gairo

0

0

0

0

 

JUMLA

279.5

1,307,018,617.75

192.3

972,555,110

 

Changamoto katika Sekta ya Uvuvi

Kuna changamoto nyingi ambazo zinajitokeza katika sekta ya uvuvi. Miongoni mwa changamoto hizo ni kama ifuatavyo:

Upungufu au ukosefu wa wataalamu wa Uvuvi katika mamlaka za Serikali za Mitaa unapunguza ufanisi katika kutekeleza majukumu. Mahitaji ya wataalamu wa uvuvi katika Makao Makuu ya Halmashauri ni 18, waliopo ni 12, hivyo upungufu ni 6. Aidha mahitaji katika ngazi ya kata ni 214, waliopo 3 na hivyo pungufu ni 211.

Ukosefu wa vitendea kazi hususani magari na boti za doria kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa unakwamisha ufanisi katika kutekeleza majukumu.

Matumizi ya zana au njia haramu za uvuvi yaani makokoro, nyavu zenye macho madogo na matumizi ya sumu vinatishia ustawi wa samaki

Uhaba wa maji ya kutosha hususani wakati wa kiangazi husababisha mabwawa mengi ya kufugia samaki kuwa ya msimu.

Halmashauri kutorejesha 5% ya mapato yatokanayo na shughuli za uvuvi kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli za uvuvi.

Mapendekezo ya Utatuzi wa Changamoto na Mikakati Iliyopo Kuongeza Uzalishaji wa Samaki

Halmashauri ziendelee kuomba kibali cha kuajiri Maafisa Uvuvi angalau kila Kata iwe na Afisa Uvuvi ili elimu ya kutosha kuhusu rasilimali hii ya samaki isambazwe kwenye maeneo yote Mkoani.

Wakurugenzi wasisitizwe kutenga bajeti za ununuzi wa boti za doria katika mipango yao.

Kuendelea kutoa elimu za mara kwa mara kwa wavuvi na wafugaji wa samaki ili watambue umuhimu wa kuwepo kwa rasilimali ya samaki kwa kizazi cha sasa na kijacho.

Kuendelea kuhamasisha jamii kuchimba mabwawa ya kufugia samaki na hatimaye kupunguza utegemezi katika vyanzo vya asili.

Kuendelea kusisitiza Halmashauri kuendesha doria mara kwa mara hasa katika maeneo yenye uharibifu mkubwa wa mazingira ili kuhakikisha sheria na kanuni zinafuatwa.

Kuendelea kutoa elimu kwa wakulima kupandikiza vifaranga bora na pia kutumia chakula bora cha samaki ili wazalishe kwa tija.

Kuimarisha vikundi vya ulinzi wa rasilimali ya uvuvi (BMUs) katika maeneo yote ya uvuvi.

USHIRIKA

Vyama vya Ushirika ni muungano wa watu au Vyama vyenyewe wenye/vyenye nia moja ya kuinua hali za kiuchumi na kijamii kwa wanachama wake na ndio njia mbadala ya kuleta maendeleo kwa urahisi na haraka kwa mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla. Vyama vya Ushirika vilivyosajiliwa kuanzia Aprili 2021 hadi 31 marchi, 2023 ni 32 vyenye wanachama 2,219 na Mtaji wa shilingi 159,292,000 kama ifuatavyo:

Jedweli Na. 22: Idadi ya Vyama vya Ushirika vilivyosajiliwa tangu Mwezi Aprili, 2021

SN
JINA LA CHAMA
HALMASHAURI
MTAJI

IDADI YA WANACHAMA

1.
TUAMKE AMCOS
ULANGA

6,734,000

50

2.
ERETO LIVESTOCK
MVOMERO

780,000

40

3.
GOMBO AMCOS
MOROGORO

3,960,000

43

4.
NGUVUKAZI AMCOS
MOROGORO

2,800,000

24

5.
WASASOMA COOPERATIVE
MANISPAA

3,000,000

30

6.
ILUMATA AMCOS
KILOMBERO

33,000,000

139

7.
UWAMA AMCOS
KILOSA

470,000

88

8.
DUMILA AMCOS
KILOSA

1,848,000

44

9.
WASUMAGRO AMCOS
KILOSA

810,000

34

10.
KIMAMBA AMCOS
KILOSA

1,140,000

50

11.
MLIMBA AMCOS
MLIMBA

5,120,000

32

12.
URAFIKI AMCOS
MVOMERO

870,000

20

13.
BWAKIRA AMCOS
MOROGORO

1,540,000

20

14.
MIMKA AMCOS
MOROGORO

2,520,000

21

15.
KIDOGOBASI AMCOS
IFAKARA

22,900,000

718

16.
KILOCHACOS LTD
KILOSA

10,000,000

15

17.
KINDA AMCOS
MVOMERO

890,000

20

18.
MASOKI AMCOS
MALINYI

2,000,000

103

19.
KILOMBERO FISHERS LTD
IFAKARA

1,500,000

33

20.
LUMEMO AMCOS
IFAKARA

870,000

30

21.
KATURUKILA SACCOS
IFAKARA

10,920,000

42

22.
KWALUKWAMBE AMCOS
KILOSA

2,400,000

20

23.
NYERERE SACCOS
MOROGORO

16,000,000

80

24.
LUMANGO AMCOS
KILOSA

2,500,000

124

25.
MILAMA AMCOS
MVOMERO

3,700,000

41

26.
KIWAVIMEKI AMCOS
MVOMERO

6,120,000

56

27.
SUNGAJI AMCOS
MVOMERO

340,000

34

28.
MOROGORO YOUTH COOP.
MANISPAA

3,800,000

20

29.
MBWADE AMCOS
MOROGORO

5,370,000

179

30.
MOROGORO SOYBEANS
MVOMERO

2,570,000

22

31.
KANGA AMCOS
GAIRO

220,000

23

32.
UWASAMO LTD
MANISPAA

2,600,000

24

JUMLA

159,292,000

2219

 

MIRADI YA MIFUGO INAYOTEKELEZWA KWA MWAKA WA FEDHA 2022/2023KUPITIA FEDHA ZA MFUKO WA SERIKALI KUU.

S/N
JINA LA HALMASHAURI
AINA YA MRADI
KIASI CHA FEDHA
1
GAIRO
MAJOSHO 5
115,000,000
2
IFAKARA
MAJOSHO 3
69,000,000
3
MALINYI
MAJOSHO 4
92,000,000
4
KILOSA
MAJOSHO 3
69,000,000
5
MLIMBA
MAJOSHO 4
92,000,000
6
MOROGORO DC
MAJOSHO 5
115,000,000
7
MVOMERO
MAJOSHO 4
92,000,000
8
ULANGA
MAJOSHO 4
92,000,000


JUMLA 32
JUMLA 736,000,000











Usajili wa SACCOS kuwa na Leseni ya BOT

Hadi tarehe 31.3.2023 Vyama vya Ushirika wa Akiba na Mikopo (SACCOS) vipatavyo 70 vimehamasishwa na kusimamiwa kubadilisha masharti na sera mbalimbali za uendeshaji, ili ziweze kukamilisha maombi ya Leseni za kutoa huduma za kifedha kwa mujibu wa Sheria Na.10 ya Huduma Ndogo za Kifedha ya mwaka 2018 na Kanuni zake za mwaka 2019, kati ya hizo SACCOS 35 zimeshapata Leseni kwa mchangunuo ufuatao, daraja A vyama 29 na daraja B vyama 6, maombi ya vyama 25 ya daraja A yanaendelea kufanyiwa kazi baada ya marekebisho ya awali.  SACCOS 35 zilizopata Leseni kama inavyoonekana hapa chini:

Jedweli Na. 23: Mchanganuo wa SACCOS zilizopata Leseni ya BOT

Na 
Wilaya 

Jina la SACCOS

1.
Morogoro MC

Veta Kihonda SACCOS LTD, Ufundi SACCOS LTD, Cetex SACCOS LTD, MVITC SACCOS LTD, Pass Trust SACCOS LTD, Dimon SACCOS na MMT SACCOS, Lusemo SACCOS, SUA SACCOS LTD, Eligbo SACCOS LTD, ACT Tumaini SACCOS LTD, Uzima SACCOS LTD.na Jitegemee Adventist SACCOS LTD.

2.
Morogoro DC

M & MT SACCOS LTD, Tawa SACCOS LTD, Mkuyuni Juhudi SACCOS LTD, Kinole SACCOS LTD

3.
Gairo
0
4.
Kilosa

Veta Mikumi SACCOS LTD, Kantui SACCOS LTD,

Umoja Mvumi SACCOS LTD, Mikoche SACCOS LTD, United SACCOS

5.
Malinyi

Lugala HOSPTAL SACCOS LTD, 

6.
Ulanga

0

7.
Mvomero

Mvomero Rural SACCOS LTD, Elimu SACCOS LTD, Kikeo SACCOS LTD, Tur   SACCOS LTD, MU SACCOS LTD na Mvomero District Teachers SACCOS LTD.

8.
Ifakara Mji

Ifakara Centre SACCOS LTD, Udzungwa SACCOS LTD, Mitiki Workers

SACCOS LTD, TPWU SACCOS LTD, Mgude SACCOS, KDW SACCOS LTD

9.
Mlimba
0

Uwekezaji kwenye Vyama vya Ushirika

Katika kuhakikisha kuwa Vyama vinajenga na kukuza mitaji yake, Vyama vya Ushirika 16 vinamiliki Hisa zenye thamani ya shilingi milioni arobaini na nane laki tatu hamsini na nne elfu mia moja kumi na nne (48,354,114/=) kwenye taasisi ya kifedha ambayo ni KCBL kwa mchanganuo ufuatao:

Jedweli Na. 24: Mchanganuo wa Vyama vya Ushirika Vinavyomiliki Hisa KCBL

SN
Name of Cooperative
Region/ location
 AMOUNT PAID 
1
TURI SACCOS LTD
Morogoro

2,000,000

2
UWAWAKUDA
Morogoro

2,000,000

3
SPM SACCOS LTD
Morogoro

2,000,000

4
Morogoro and Mvomero Teachers Saccos
Morogoro

2,000,000

5
IFAKARA CENTER SACCOS
Morogoro

2,000,000

6

TABACCO CO-OPERATIVE JOINT ENTERPRISE LTD

Morogoro

4,000,000

7

MVOMERO TEACHERS SACCOS LTD

Morogoro

4,000,000

8

MOFACU LTD

Morogoro

500,000

9

MOROGORO MUNICIPAL TEACHERS SACCOS LTD

Morogoro

2,000,000

10

TOBACCO CO-OPERATIVE JOINT ENTERPRISE LTD

Morogoro

4,000,000

11
DIMON MOROGORO SACCOS LTD
Morogoro

5,644,816

12
UWAWAKUDA LTD
Morogoro

5,644,816

13
TUR SACCOS LTD
Morogoro

564,482

15
Kinole saccos
Morogoro

10,000,000

16
Mzumbe SACCOS LTD
Morogoro

2,000,000

 
TOTAL

48,354,114

Makusanyo ya Fedha za Mfuko wa Ukaguzi

Kwa mwaka huu Makadirio ni   SH 100,000,000/=, lakini uhalisia wa makusanyo ya fedha za Mfuko wa Ukaguzi na Usimamizi kwa robo hii ya tatu ya mwaka 2022/2023 ni SH   124,332,124.59 na Kufanya tuvuke lengo kwa asilimia 24.3 kama inavyoonekana hapa chini: -

Jedweli Na. 25: Mchanganuo wa Makusanyo ya Fedha za Mfuko wa Ukaguzi

NA. 

CHANZO 

MAKADIRIO

UHALISIA MWAKA  2022/2023  

TOFAUTI (ONGEZEKO)

1.

 

 

 

-SACCOS
-Vyama vya Mazao
-Mikataba mbalimbali
-Vyanzo vingine

100,000,000.00

 124,332,124.59

 

 

24,332,124.59

JUMLA KUU 

100,000,000.00

124,332,124.59 

24,332,124.59 

 

Kuongeza Uzalishaji, Kusimamia Mifumo ya Masoko na Mitaji  kwenye Vyama vya Ushirika

 Uzalishaji/Makusanyo ya Zao la Miwa. 

Mazao yanayolimwa Mkoa wa Morogoro ni pamoja na Pamba, Tumbaku, Miwa, Kakao, Mkonge n.k ambayo pia yanauzwa kupitia kwenye Vyama vya Ushirika vya Msingi. Kati ya hayo zao linalolimwa na kuzalishwa kwa wingi ni Miwa, hadi kufikia tarehe 31 Machi, 2023 uvunaji ni tani 565,702 zenye thamani ya shilingi 63,924,213,000, zilikuwa zimeuzwa kiwandani na Wakulima wamelipwa fedha hizo.

Mifumo ya Masoko Inayotumika Kwenye Vyama 

Kwa upande wa mazao ya Kokoa na Iliki, baada ya kukusanywa kutoka kwa Wakulima ngazi ya AMCOS, Unions hutafuta masoko na kuuza kwa kutumia Mfumo wa Stakabadhi ghalani unaotumiwa na TMX.  Kwa upande wa zao la Miwa Vyama vya msingi huuza moja kwa moja kiwandani.

Changamoto zilizopo wakati wa Utekelezaji wa Majukumu ya Ushirika Mkoa Wa Morogoro.

Katika kutekeleza majukumu ya usimamizi, udhibiti na uhamasishaji wa Wananchi kujiunga, kuendeleza na kuanzisha Vyama vya Ushirika, Mkoa wa Morogoro unakabiliwa pia na changamoto zifuatazo: -

Uhaba wa Maafisa Ushirika ngazi ya Mkoa na Halmashauri na kupelekea kupungua kwa uwajibikaji katika Vyama kutokana na kutofikiwa ipasavyo.   Hitaji la Maafisa Kimkoa ni ishirini na mbili (22).

Upungufu wa vyombo vya usafiri kama vile Magari na vitendea kazi kuanzia Ofisi ya Mrajis Msaidizi Mkoa na Wilaya japokuwa kuna uzalishaji mkubwa wa Miwa na idadi kubwa ya Vyama vya Ushirika.

Baadhi ya Vyama kukabiliwa na migogoro na kesi kutokana na utendaji usioridhisha kwa Viongozi na Watendaji wasiokuwa waadilifu katika kutekeleza majukumu yao.

Vyama kutumia mifumo ya kizamani katika utunzaji wa kumbukumbu na kupelekea kukosekana taarifa/takwimu sahihi kwenye Vyama pindi zinapohitajika kwa ajili ya kuandaa taarifa ya jumla na mipango ili kufanya maamuzi juu ya maendeleo ya tasnia ya Ushirika,

Baadhi ya Watendaji na Wajumbe wa Bodi kuwa na uelewa mdogo juu ya uwajibikaji na uendeshaji wa Vyama, hivyo kupelekea utendaji usiofaa na kutofikiwa malengo tarajiwa.

Mikakati ya Kuimarisha Vyama vya Ushirika Mkoa Wa Morogoro

Ofisi ya Mrajis Msaidizi wa Vyama vya Ushirika Mkoa kwa kushirikiana na

Mamlaka mbalimbali katika Mkoa inaendelea kutekeleza majukumu yake ya

Kisheria kwa kupitia mikakati ifuatayo:

Kuendelea kusajili vyama vya ushirika vipya kwa kuzingatia mahitaji ya kiuchumi ya Wananchi, ambavyo vitaendelea kutoa huduma stahiki kwa wanachama na jamii ili kusaidia kuharakisha kuwaletea wananchi maendeleo,

Kufufua Vyama vya msingi vya ushirika, ambavyo havifanyi kazi ipasavyo na kuhamasisha jamii kujiunga na vyama vya ushirika vilivyopo ili kuongeza wanachama wapya.

Kushirikiana na Bodi za AMCOS kupitia ajira za Watendaji/Makarani na kuwafanyia upekuzi (Vetting) kabla ya msimu kuanza ili kupunguza malalamiko na ubadhirifu wa mali za ushirika.

Kuzisimamia Bodi za Union na kuhakikisha zinaingia makubaliano ya kiutendaji na watendaji wake wakuu ili kuongeza udhibiti na uwajibikaji.

Kusimamia kufanyika kwa Ukaguzi wa mara kwa mara, ufanyikaji wa mikutano ya kisheria, uidhinishaji wa makisio na kudhibiti matumizi mabaya ya fedha katika vyama. 

Kusimamia SACCOS 35 zilizopata leseni kuandaa na kuwasilisha taarifa mbalimbali za utendaji kwa mujibu wa Sheria na kuchukua hatua za kurekebisha mapungufu mbalimbali yatakayobainika ili kuziimarisha.

Kuhimiza SACCOS zenye sifa kuomba leseni ya uendeshaji wa huduma ndogo za Fedha kwa mujibu wa Sheria ya Hunduma ndogo za fedha Na.10 ya mwaka 2018,

Kuendelea kufuatilia matumizi ya fedha za ushuru wa AMCOS ili zitumike kwa kuzingatia makisio yaliyoidhinishwa, 

Kuendelea kutoa elimu ya uongozi na uendeshaji wa ushirika kwa wajumbe wa Bodi wa Vyama vya Ushirika kwa kupitia vikao vyao vya kujadili taarifa za ukaguzi.

Kuendelea kuhimiza na kusimamia Vyama ili viweze kuchangia ada ya mfuko wa ukaguzi na tozo mbalimbali za Mrajis kwa ajili ya kutatua changamoto ya uhaba wa bajeti ya fedha za usimamizi,

Kuendelea kushirikiana na Mamlaka nyingine za Serikali ili kuweze kuvisimamia Vyama kwa mujibu wa Sheria ya Ushirika Na 6 ya mwaka 2013, Kanuni zake za mwaka 2015 na sheria nyingine za nchi.

 

Mafanikio

Kutekeleza Mfumo wa stakabadhi ghalani kwa kuuza zao la Kokoa.

Kuajiri watendaji wenye sifa kwa baadhi ya Vyama.

Kufanya Ukaguzi kwenye Vyama

Kusimamia mikutano mikuu ya vyama

Kufanya Uchaguzi wa Viongozi wa Bodi za Vyama kwa wakati

Kutatua Migogoro ya vyama vya Ushirika

Kutoa Elimu na Mafunzo ya ushirika

Kusimamia SACCOS kuomba Leseni za BOT

Kuunganisha Vyama vya Ushirika na Taasisi mabilimbali za fedha

Kusajili watoa huduma mbalimbali kwenye Vyama vya ushirika

Mapendekezo

Elimu ya ushirika kuendelea kutolewa kwa Wanachama na Wananchi kwa ujumla.

Kuendelea kusisitiza Vyama vya Ushirika wa mazao kufanya shughuli lengwa ya kuanzishwa kwake

Kuajiri watumishi wa Sekta ya ushirika wa kutosha ili angalau Afisa mmoja asimamie vyama vya ushirika saba (7)

Kuongeza vitendea kazi (Gari) na rasilimali kwa maafisa Ushirika ili kuweza kuvifikia Vyama

Kuendelea kusisitiza Vyama vya Ushirika kuajiri watendaji wenye sifa

Maafisa ushirika wote wawezeshwe kuvifikia vyama vya Ushirika ili kuvishauri ipasavyo na kuwa na takwimu sahihi.

Vyama vya Ushirika wa Kilimo na Masoko viendelee kutumia mfumo wa Stakabadhi za Ghala kuuza mazao yao kwa faida zaidi.

MALIASILI NA UTALII

Mkoa wa Morogoro umebarikiwa kwa kuwa na vivutio vingi ukihusisha mbuga zenye bio-anuai nyingi na mandhari za kupendeza, milima, maporomoko ya maji, vyanzo vya maji, na wanyamapori, ndege wa aina mbalimbali, mapango ya kihistoria, maeneo ya njia za watumwa na misitu minene na safu za milima ya Tao la Mashariki. Mkoa wa Morogoro ni wa pili kwa kuwa na vivutio vingi vya aina mbalimbali hasa Mimea na Wanyama katika ukanda wa kusini (Southern Tourist Circult) baada ya Mkoa wa Arusha katika ukanda wa Kaskazini (Northern Tourist circuit).

Aina ya hifadhi (Protected Areas) ndani ya Mkoa wa Morogoro

Hifadhi za Taifa (National Parks):  Mkoa una Hifadhi tatu za Taifa ambazo ni Hifadhi ya Taifa ya Mikumi (4,471 sq km), Hifadhi ya Milima ya Udzungwa (52 sq km), na Hifadhi ya Taifa Mwl. Nyerere (30,893sq km)

Misitu ya Asili (Catchment Forest Reserves).  Mkoa una misitu 39 yenye ukubwa wa hekta (321,236).

Hifadhi za Mazingira Asilia (Nature Reserves):  Mkoa una Hifadhi za Mazingira Asilia (Nature Reserves) tano ambazo ni Kilombero (134,000 Ha), Uluguru (24,115.09 Ha), Mkingu (23,387.88 Ha), Uzungwa scarp (32,763.2 Ha) na Magombera (Ha)

Mapori mawili ya akiba, Pori la akiba la Kilombero (Kilombero Game Controlled Area): Ni kiini cha eneo la ardhi-oevu ambalo ni RAMSAR site (698,930Ha) na Pori la akiba la Wami Mbiki (Wami-Mbiki Game Controled area) yenye ukubwa wa (2466.58 Ha)

Hifadhi mbili za jamii za Iluma na Jukumu (Community Wildlife Management Areas): Mkoa una hifadhi mbili za jamii, Iluma (509Ha), Jukumu (639 Ha). Hifadhi hizi zimeidhinishwa (Authorized Association) na kupewa Hati ya matumizi (User Rights). Utalii upo kidogo lakini mpango wa kupata wawekezaji unaendelea.

Mwingiliano wa Wanyamapori na Binadamu

Mwingiliano wa Wanyamapori na binadamu bado ni mkubwa kwani wanyamapori waharibifu wameendelea kuharibu mazao mashambani ikiwa ni pamoja na kusababisha majeruhi pamoja na vifo Mkoani hapa.

Hata hivyo wananchi wameendelea kufundishwa mbinu mbalimbali za kukabiliana na wanyamapori waharibifu kama kutumia vilipuzi, kuweka fensi ya pilipili, vitofali pamoja na kuweka mizinga ya nyuki.

Mpango wa Kuimarisha Utalii Morogoro

Mkoa wa Morogoro una mkakati wa kuimarisha utalii kwa kuendelea kuvitangaza vivutio tulivyonavyo, kuweka kituo cha kisasa cha kukusanya Taarifa za Utalii yaani (Tourism Collection centre), Kuweka mabango ya kidigitali katika mji wa Morogoro ili kuendelea kuvitangaza vivutio vyetu hata kwa wageni na wasafiri.

Taarifa ya TANAPA Mkoa wa Morogoro

Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) ni Shirika la Umma lililo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii lenye dhamana ya kusimamia uhifadhi ndani ya mipaka ya maeneo yaliyotangazwa kuwa Hifadhi za Taifa Tanzania bara.

TANAPA inasimamia Hifadhi za Taifa 22 zilizo gawanywa kiutawala kwenye Kanda nne ambazo ni Kaskazini, Kusini, Magharibi na Mashariki.

Kanda ya Mashariki inasimamia Hifadhi nne ambazo ni hifadhi ya Taifa Nyerere, Mikumi, Udzungwa na Saadani. Kati ya hizo, hifadhi tatu zipo ndani na Mkoa wa Morogoro.

Mwenendo wa Idadi ya Wageni na Mapato

Kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita kuanzia 2018/19 hadi 2022/23 hifadhi tatu zilizopo ndani ya Mkoa wa Morogoro (Nyerere, Mikumi na Udzungwa) zilipokea watalii 446,950 ambao wameingizia Serikali jumla ya shilingi 32,327,712,980.86 kama inavyoonekana kwenye Jedwali 1 na 2.

Kabla ya dunia kukumbwa na janga la UVIKO-19, Hifadhi hizi zilikuwa zikipokea watalii wengi pamoja na mapato. Baada ya utalii kukumbwa na janga la UVIKO 19, idadi ya watalii ilipungua ambapo mwaka 2019/2020 hifadhi hizi kwa pamoja ilipokea watalii 61,052 na kukusanya TShs 2,782,279,749.25 kutokana na huduma za utalii.

Kutokana na jitihada za Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania za kutangaza utalii kwa kupitia Filamu ya “The Royal Tour” ilisaidia kuongeza idadi ya watalii na uwekezaji nchini. Hifadhi ya Nyerere, Mikumi na Udzungwa nazo pia zilinufaika kwa kupokea watalii wengi.

Mwaka 2020/21 idadi ya watalii na mapato walio tembelea hifadhi ya Nyerere, Mikumi na Udzungwa iliongezeka na kufikia watalii 71,391 na kukusanya TShs 4,820,773,785.78

 

Kwa mwaka huu 2022/2023 idadi ya watalii walio tembelea hifadhini hizi tatu zilizo mkoani Morogoro imeongezeka sambamba na ongezeko kubwa la mapato yatokanayo na utalii. Kuanzia mwezi Julai 2022 - Machi 2022/23 hifadhi hizi tatu (Nyerere, Mikumi na Udzungwa) zimepokea watalii 141,951 na kukusanya Tshs 13,424,104,959.85 (Jedwali Na. 1 na 2).

 

Jedweli Na. 26: Takwimu za Watalii Walio Mtembelea Hifadhi Kuanzia Mwezi Julai 2022 hadi Machi 2023

SN
HIFADHI

Julai 2022 - Machi 2023

2021/2022

2020/2021

2019/2020

2018/2019

1.
Nyerere

46,744

29,576

19,642

0

0

2.
Mikumi

85,373

66,790

45,677

54,183

59,260

3.
Udzungwa

9,834

8,083

6,075

6,869

8,844



141,951

104,449

71,394

61,052

68,104

 Ukusanyaji wa Mapato kwa Miaka Mitano 2018/19-Julai-Machi 2022/23

Jedweli Na.27: Ulinganisho wa Mapato (Revenue) yaliyo kusanywa kutokana na Utalii Mwezi Julai 2022 – Machi 2023 ikilinganishwa na Miaka iliyopita kwa Hifadhi za Kanda ya Mashariki

S/N

HIFADHI

MAPATO

Julai 2022 - Machi 2023

2021/22

2020/21

2019/20

2018/19

1.
Nyerere

9,381,506,308.50

5,561,674,165.80

3,015,044,411.99

0

0

2.
Mikumi

3,744,152,465.00

2,523,376,544.88

1,667,651,136.47

2,387,731,075.79

2,556,099,558.96

3.
Udzungwa

298,446,186.35

264,168,821.95

138,078,237.32

394,548,673.46

395,235,394.39


JUMLA

13,424,104,959.85

8,349,219,532.63

4,820,773,785.78

2,782,279,749.25

2,951,334,953.35

Ukusanyaji wa Mapato kwa Miaka Mitano 2018/19-Julai-Machi 2022/23

Hali ya Usalama wa Maliasili Kwenye Hifadhi za Taifa

Hali ya usalama kwenye maeneo ya Hifadhi za Taifa ni salama. Ulinzi na usalama wa maliasili umeendelea kuimarishwa ikiwa ni pamoja na kulinda maeneo ya vyanzo vya maji na mito inayo tiririsha maji kwenye mradi mkakati wa bwawa la kuzalisha la Mwalimu Nyerere. Jitihada hizi za ulinzi zinafanywa na Jeshi la Uhifadhi kwa kushirikiana na vyombo vya usalama ngazi za Wilaya na Mkoa.

Katika kipindi cha Julai 2022 – Machi 2023 hifadhi hizi tatu iliendelea kutekeleza shughuli za ulinzi na usalama kuzuia ujangiri na uhalifu mwingine kwenye maeneo ya hifadhi za Taifa. Katika kipindi hicho, majangili 494 walikamatwa hifadhini na kufikishwa mahakamani. Katika kipindi hicho, nyara za serikali ambazo ni meno 49 ya tembo yalikamatwa kutoka kwa majangili. Aidha, bunduki 6 zilizo kuwa zikitumiwa kuwinda zilikamatwa. Katika kipindi hicho pia mifugo 4593 ilikamatwa hifadhini ikichungia kinyume cha sheria.

Jedweli Na.28: Takwimu za Ujangili na idadi ya Mifugo iliyo kamatwa Hifadhi ya Nyerere na Mikumi Kuanzia Mwezi Julai 2022 hadi Machi 2023

Na

Ukamataji

Hifadhi

Jumla

Nyerere

Mikumi

Udzungwa

1.

Majangili walio kamatwa hifadhini

387

28

79

494

2.

Meno ya Tembo yaliyo okolewa kutoka kwa majangiri

31

14

4

49

3.

Silaha (bunduki & gobole) zilizo kamatwa

4

0

2

6

4.

Mifugo iliyo kamatwa hifadhini

3918

675

0

4593

Miradi ya Maendeleo Inayo Tekelezwa kwa Fedha za UVIKO - 19.

Kati ya hifadhi hizi tatu zinazo husika na taarifa hii ni Hifadhi ya Taifa Nyerere iliyopata fedha za UVIKO-19 kwa ajili ya kutengeneza miradi ya maendeleo.

Miradi inayo tekelezwa imejengeka kuboresha miundombinu ya watalii ambayo kwenye hifadhi hii ili kuvutia idadi kubwa ya watalii waitembelee na kuwesha serikali kukusanya fedha nyingi kama tozo ambazo zitainua pato la Taifa. Miradi inayo tekelezwa kwa fedha hizo ni:

Miradi ya Ujenzi wa Barabara Kiwango cha Changarawe

Kupitia fedha za mradi wa UVIKO-19, kilometa 374 za barabara zimetengenezwa katika hifadhi ya Nyerere ili kufungua maeneo yenye vivutio vya utalii kwenye hifadhi hiyo kama ifuatavyo:

Barabara ya Likuyuseka yenye urefu wa kilometa 100 - Nyerere Kusini (wilaya ya Namtumbo). Hadi kukamilika, mradi huu utagharimu Tshs 642,506,012.00

Barabara ya Kalulu yenye urefu wa kilometa 100 - Nyerere Kusini (wilaya ya Tunduru). Hadi kukamilika, mradi huu utagharimu Tshs 611,685,925.78 

Barabara ya Liwale yenye urefu wa kilometa 104 - Nyerere Kusini (wilaya Liwale). Hadi kukamilika, mradi huu utagharimu Tshs 741,911,477.20

Barabara ya Bomaulanga yenye urefu wa kilometa 42 - Nyerere Kaskazini (wilaya ya Ulanga). Hadi kukamilika, mradi huu utaghatimu Tshs 1,075,553,598.00

Barabara ya Msolwa yenye urefu wa 28 - Nyerere Kaskazini (wilaya ya Kilombero). Mradi huu unatekelezwa kwa Tshs 598,005,946.00

Matengenezo ya Viwanja vya Ndege

Kupitia mradi huo wa UVIKO-19, viwanja viwili (2) vya ndege vimejengwa ndani ya hifadhi ya Nyerere kwa kiwango cha changarawe ili kurahisisha usafirishaji wa watalii kwa njia ya anga kutembelea hifadhi hiyo. Viwanja hivyo ni:

Kiwanja cha Bomaulanga (wilaya ya Ulanga). Utekelezaji wa huu upo kwenye hatua za umaliziaji. Mradi huu unatekelezwa kwa Tshs 593,799,600.00

Kiwanja cha ndege Likuyuseka (wilaya ya Namtumbo). Utekelezaji wa mradi huu upo kwenye hatua za umaliziaji. Mradi huu unatekelezwa kwa Tshs 601,472,856.80

Ujenzi wa Malango ya Kupokelea Wageni

Kupitia fedha za mradi wa UVIKO, TANAPA inatekeleza miradi mwili ya ujenzi wa malango ya kupokelea wageni na pamoja nyumba 6 za watumishi katika hifadhi ya Taifa Nyerere. Maeneo inapotekeleza miradi hiyo ni:

Ujenzi wa lango la Msolwa (Wilaya ya Kilombero). Mradi huu katika upo hatua za umaliziaji. Hadi kukamilika, mradi huu wa jengo la ofisi na nyumba 3 za familia 8 utatumia Tshs 1,979,860,172.01.

Ujenzi wa lango la Likuyu-Sekamaganga (Wilaya ya Kilombero) upo katika hatua za umaliziaji. Hadi kukamilika, mradi huu wa jengo la ofisi na nyumba 3 za familia 8 utagharimu TShs 2,274,862,397.29.

Maeneo Yanayosimamiwa na Tawa Katika Mkoa wa Morogoro

Mamlaka ya Usimamizi wa Wanayampori Tanzania inasimamia shughuli uhifadhi katika maeneo yaliyopo nje ya Hifadhi za Taifa na Eneo la Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro. Katika Mkoa wa Morogoro, TAWA inasimamia Mapori ya Akiba ya Wamimbiki (2,466.58km2) na Kilombero (6,989.3km2). Mapori haya yameanzishwa katika Serikali ya awamu ya sita.

Katika juhudi za kuimarisha ulinzi wa vyanzo vya maji na rasilimali ya wanyamapori, Mkoa unapongeza kwa dhati uamuzi wa Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi mahiri wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa kupandisha hadhi maeneo ya Pori tengefu kilombero, maeneo ya wazi, na hifadhi ya jamii ya wanyamapori ya Wamimbiki kuwa Mapori ya Akiba. Hatua hiyo imeimarisha uhifadhi na ulinzi wa vyanzo vya maji ikiwemo Bonde la Kilombero linalochangia takribani 65% ya maji ya Mradi wa kufua umeme wa Bwawa la Mwalimu Nyerere, uhifadhi wa vyanzo vya mito Wami, Mbiki, Ngerengere, Likigula na ambayo ni chanzo cha maji kwa Mikoa ya Pwani na Dar es salaam.

Katika kuboresha shughuli za utalii, TAWA imejenga miradi ya maendeleo kwa fedha za Mpango wa Ustawi wa Taifa kwa Jamii na Mapambano dhidi ya UVIKO 19 yenye thamani ya shilingi 2,298,126,825/=. Miradi hiyo ni ujenzi wa barabara yenye urefu wa kilometa 47.2, ujenzi wa lango la utalii na kituo cha askari, ununuzi wa gari Toyota Land Cruiser moja kwa ajili ya usimamizi wa shughuli za utalii na ukarabati wa mabanda 6 ya watalii katika Pori la akiba Wamimbiki. Vilevile vimejengwa vituo vitatu (3) vya kukusanya mapato, eneo la kupumzikia wageni na ununuzi wa boti ya doria katika Pori la akiba Kilombero.

Aidha, kutokana na fedha za bajeti TAWA imenunua magari manne (4) kwa ajili ya doria za kuzuia ujangili, kudhibiti wanyamapori wakali na waharibifu na ulinzi wa vyanzo vya maji katika maeneo hayo.

Katika kupunguza migogoro baina ya wahifadhi na wananchi TAWA imeweka alama za mipaka (vigingi 722) katika Mapori ya Akiba Wamimbiki na Kilombero.  Aidha, TAWA imeweka utaratibu unaowaruhusu wananchi wa Wilaya za Kilombro, Malinyi na Ulanga kufanya uvuvi endelevu katika Pori la akiba Kilombero kwa vibali maalum pamoja na kujenga soko la kuuza samaki katika Wilaya ya Kilombero. Utaratibu huu una tija kwa uhifadhi na uchumi kwa wananchi.

Katika juhudi za kudhibiti matukio ya wanyamapori wakali na waharibifu, TAWA imejenga kituo cha askari wa mwitikio wa haraka katika kijiji cha Sangasanga. TAWA itaendelea kuwashirikisha wananchi katika shughuli za Uhifadhi ikiwemo kutoa elimu ya kuepuka madhara ya wanyamapori wakali na waharibifu na kusaidia miradi ya maendeleo.

 

Changamoto za Uhifadhi na Utalii Mkoani Morogoro

Pamoja na Mkoa kuwa na vivutio vingi vya mambo ya kihistoria na Kiikolojia bado Utalii ni mdogo sana na zaidi ya asilimia tisini (90%) ya vivutio hivi havijatumika au kupewa vipaumbele kwani utalii wa ndani (Domestic Tourism) na kwa wageni wa nje ni kiasi kidogo sana katika hifadhi za Taifa za Udzungwa na Mikumi.

 

Kwa Hifadhi ya Taifa Mikumi pekee kuna changamoto kubwa ya madhara yatokanayo na watumiaji wa barabara kuu inayokatisha hifadhini yenye urefu wa kilomita 50. Takwimu zinaonyesha wastani wa magari 1,758 hupita ndani ya Hifadhi kila siku. Magari haya pamoja na abiria husababisha madhara yafuatayo:

Kuongezeka kwa idadi ya vifo vya wanyamapori wanaogongwa na magari. Takwimu zinaonesha jumla ya wanyama 956 waligongwa katika barabara hii kwa kipindi cha miaka 5 (2011 - 2015) wakiwemo Simba, Chui, Tembo na Twiga. Pia takwimu za hivi karibuni zinaonesha wastani wa mnyama mmoja (1) hugongwa kila siku sawa na wastani wa wanyama 360 kwa mwaka. Pengine idadi hii ya vifo ni zaidi ya ile inayotokana na majangili katika hifadhi hiyo.

Kuongezeka kwa uchafuzi wa mazingira unaofanywa na wasafiri/wasafirishaji wanaotumia barabara hii.  Kwa kipindi cha miaka mitano (2011 - 2015) jumla ya tani 36 za taka ngumu ziliokotwa ndani ya Hifadhi. Takataka hizo husababisha wanyamapori hasa jamii ya nyani (primates) kubadili tabia zao za asili kwa sababu ya kuzoea kula mabaki ya vyakula vinavyotupwa na watumiaji wa barabara hiyo.

Utalii usiolipiwa unaoikosesha Hifadhi ya Taifa Mikumi mapato na serikali kwa ujumla. Kwa mfano kwa wastani wa magari 1, 758 kwa takwimu za miaka 5 (2011 - 2015) ukihusisha magari ya ndani ya nchi na nje niwazi kabisa kwamba mapato mengi hayakusanywi na serikali inakosa kodi na zaidi kipande hiki cha kilometa 50 kinapita mbugani na hakina mchango wowote kwa wananchi wa Halmashauri za Wilaya za Mvomero na Kilosa.

Madhara mengine ni pamoja na Ujangili. Uwepo wa barabara hii ndani ya Hifadhi unatoa fursa ya majangili kuingia hifadhini kwa njia mbalimbali ikiwemo magari na pikipiki na kufanya uhalifu ukiwemo uwindaji haramu wa wanyamapori, hasa tembo, ukataji miti na upasuaji mbao. Aidha, imekuwepo tabia ya baadhi ya madereva kuegesha magari pembezoni mwa barabara kwa kisingizio kuwa yameharibika ikiwa ni mbinu ya kusubiri nyara mbalimbali zitokanazo na ujangili na hivyo kufanikisha malengo yao ya kuzisafirisha bila kubainika.

Ujangili unaosababisha kupungua kwa wanyamapori husuan wa meno ya tembo na ule wa nyama.

Uvamizi wa mifugo ni tatizo ambalo linalikabili hifadhi nyingi ndani ya Mkoa hususan Bonde la Kilombero ambalo wanyama hukidhi mahitaji yao ya mzunguko hutoka Selous kwenda bonde la Kilombero, Hifadhi za Udzungwa, Mikumi, Wami mbiki hadi Saadani.

Uharibifu wa mazingira unaotishia uwepo wa vivutio hivi mfano upanuzi wa maeneo ya kilimo, makazi na wingi wa mifugo katika bonde la ardhi oevu la Kilombero, misitu ya hifadhi, Hifadhi za Taifa pamoja na uharibifu wa vyanzo vya maji. Hii ni pamoja na kutoweka kwa njia za mapito (Ushoroba) ya wanyama kutoka hifadhi moja kwenda nyingine jambo linalosababisha mwingiliano kubwa kati ya wanayapori na wananchi wanaozunguka Hifadhi na kusababisha uharibifu wa mazao ya wakulima, mifugo kuliwa au kuuwawa na pia vifo kwa watu.

Ubovu wa miundo mbinu ya barabara, ufinyu wa bajeti katika kutenga maeneo kwa ajili ya uwekezaji   pamoja na kutotangazwa kwa vivutio vya utalii.

Mapendekezo na jitihada Zilizofanyika

Mkoa umefanya juhudi za makusudi za kufanya kikao na wadau wote wa uhifadhi kwa ajili ya kuandaa mikakati ya kuwa na Makala ya vivutio vyote vya utalii vilivyopo katika Mkoa wa Morogoro

Ili kukabiliana na tatizo la vifo vya wanyamapori wanaogogwa na magari, Serikali kuharakisha ujenzi wa barabara (Melela-Kilosa-Mikumi), ambayo imeshafanyiwa upembuzi yakinifu. Pamoja na kuokoa vifo vya wanyama uthibiti wa upotevu wa mapato ya serikali unaotokana na utalii wa bure  na uchafuzi wa mazingira litakuwa ni suluhisho la kudumu.

MISITU

Mkoa una eneo la Misitu lenye ukubwa wa Hekta 757,621.57 imegawanyika katika makundi yafuatayo Misitu ya Hifadhi ya Serikali kuu ipo 39, yenye ukubwa wa Hekta 321,236, Misitu ya Hifadhi za vijiji 109, yenye ukubwa wa Hekta 222,119.4, Misitu ya Hifadhi ya asili 6, yenye jumla ya Hekta 214,266.17.

Mkoa pia unatekeleza zoezi la upandaji miti kutekeleza agizo la Serikali la kutaka kila wilaya kupanda miti isiyopungua 1,500,000. Kwa kipindi cha Mwaka 2021/22 Mkoa ulipanda jumla ya miti 5,862,377 sawa asilimia arobaini na tatu (43%) ya lengo la upandaji miti 13,500,000 kwa mkoa mzima. Halmashauri ya Mlimba iliongoza kwa kupanda miti 1,900,00 Mchanganuo kwa upandaji wa wilaya ni kama ifuatavyo.

Jedweli Na. 29: Mchanganuo wa Upandaji Miti kwa Mwaka 2021/2022

NA.
WILAYA

IDADI YA MITI


MLIMBA

1,900,000


IFAKARA

782,423


KILOSA

463,000


ULANGA

714,000


GAIRO

124,300


MVOMERO

814,654


MOROGORO

1,064,000

JUMLA

5,862,377

Mapato yatokanayo na Mazao ya Misitu

Kwa kipindi cha mwezi Julai mpaka Desemba 2022 jumla ya shilingi 1,848,417,951 zimekusanywa ambapo shilingi 1,475,806,659 zimekusanywa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania na shilingi 372,611,292 zimekusanywa na Halmashauri.

Mchanganuo wa mapato kwa kila wilaya ni kama ifuatavyo

Jedweli Na. 30: Mchanganuo wa Fedha za Mazao Yatokanayo na Misitu

NA

WILAYA

TFS

HALMASHAURI


ULANGA

216,327,153

121,404,659.65


MALINYI

207,864,842

12,757,500.00


KILOMBERO

126,119,912

47,995,270.00


KILOSA

201,766,164

76,338,700.00


MVOMERO

190,828,981

34,304,763.00


MOROGORO

532,899,607

74,000,000.00


GAIRO

-

5,810,400.00

JUMLA

1,475,806,659

372,611,292.

Mpango wa Mkoa wa kupanda Miti yenye Faida 2022/2023

Ili kuhakikisha Miti inayopandwa inatunza vizuri na kukua pamoja na kuthibiti Uchomaji wa Moto Misitu, Mkoa wa Morogoro umezindua Kampeni ya Kupanda Miti yenye Faida. Kampeni hii ilizinduliwa mwezi Februari 2023, kwa lengo la kuhamasisha wananchi kupanda miti yenye faida ile kutunza mazingira na wakati huo kupata kipato. Miti inayohamasishwa ni Miti ya matunda na Miti ya Viungo. Hadi sasa Jumla ya Miche 37,000 ya Mikarafuu imegawiwa bure kwa wakulima wa Wilaya ya Morogoro na kupandwa katika maeneo mbalimbali hasa yale yenye vyanzo vya Maji. 

Biashara ya Hewa Ukaa

Mkoa kwa sasa umeanza taratibu ya biashara ya uuzaji hewa ukaa (Carbon Dioxide) ambapo kuna mashirika manne ambayo yapo katika hatua za kufanya biashara hii. Mashirika haya ni PAMs Foundation yenye makao yake makuu mjini Arusha, ambalo linafanya shughuli hizi katika kijiji cha Pemba wilaya ya Mvomero, Shirika la Compassionate yenye makao makuu mjini Arusha linafanya shughuli hizi katika vijiji 22 vinavyozunguka misitu ya Ukwiva na Paraulanga wilayani Kilosa, na mashirika ya Tanzania Forest Conservation Group (TFCG) na Mpingo Conservation Development Institute (MCDI) ambayo yanafanya shughuli hizi katika vijiji 20 vya Wilaya ya Kilosa. Kwa upande wa Kilosa wapo katika hatua za kutambulisha mradi na kwa upande wa Mvomero utekelezaji umeeanza

Ufugaji Nyuki

Mkoa wa Morogoro una maeneo mengi ya misitu ya jamii ya Miombo ambayo pia ni muhimu sana kwa ufugaji nyuki. Kwa kipindi cha miaka mitano yani 2015-2020, Mkoa ulikuwa na jumla ya Mizinga ya kufugia nyuki ipatayo 14,997, kati ya hiyo mizinga 9,310 ni ya kisasa na mizinga 5,687 ni ya kiasili/kienyeji. Uzalishaji wa mazao ya nyuki ikiwemo asali na nta kwa mkoa wa Morogoro ni lita 48,721.8. Wastani wa uzalishaji kwa kila mzinga ni lita 3.25 ambacho ni chini ya wastani ambao ni lita 15/mzinga. 

Changamoto Katika Sekta Ya Misitu

Uvamizi wa mifugo kwenye hifadhi za misitu na mapori ya hifadhi hasa misitu ya ya Ukwiva na Paraulanga wilayani Kilosa,Msitu wa Magombera wilayani Kilombero,Misitu wa Kanga Magotwe na Pagale wilayani Mvomero,Misitu ya Nawenge,Mzelezi na Mahenge Scarp wilayani Ulanga uvamizi huu kwa kiasi kikubwa unaathiri uoto wa asili katika misitu hii na pia misitu hii ndio chanzo cha maji ya mito mingi inayotiririsha maji katika bonde la mto Kilombero.

Halmashauri kutotoa kipaumbele kwenye shughuli zinazohusiana na misitu kama shughuli za doria, upandaji miti hii inapelekea sekta ya misitu kwenye Halmashauri kutotekeleza wajibu wake ipasavyo.

Serikali kuu kutorejesha kwa wakati na kuwepo kwa masharti mengi katika kurejesha fedha za upandaji miti kwa Halmashauri zinazofanya shughuli za uvunaji.

Uvunaji wa mazao ya misitu usiofuata taratibu za uvunaji.

Kasi ya upandaji miti sio ya kuridhisha kwa mwaka 2021/22 Mkoa ulifikisha asilimia arobaini na saba (47%) tu ya lengo la upandaji miti 13,500,000.

Utatuzi

Kufanyike doria za pamoja ili kuondoa mifugo na wavamizi wote waliovamia ndani ya hifadhi za misitu na mapori ya hifadhi jambo hili lifanyike kwa haraka kwa kuwa uharibifu uliopo kwenye misitu hii ni mkubwa na aharibifu unachangia upungufu wa maji katika mito inayopelekea maji mto Rufiji hivyo kuhatarisha mradi wa umeme wa Stigglers Gorge.

Halmashauri kutoa fedha inazotenga kwenye bajeti za sekta ya maliasili ili kuwawezesha maafisa maliasili kutekeleza shughuli zao.Kwa kuwa halmashauri zinakusanya mapato yatokanayo na mazao ya misitu nashauri kuwa asilimia 20 ya mapato haya iwezeshe sekta ya misitu kutekeleze shughuli zake.

Halmashauri kufata miti yote inayotolewa na TFS na kupanda katika maeneo yao pia Halmashauri zinapaswa kuanzisha bustani zao za miti ili kuwezesha idadi kubwa ya miche kuzalishwa katika Halmashauri husika.

Halmashauri kujikita zaidi katika miradi ya uuzwaji wa kaboni ambayo inaingiza fedha nyingi na pia kwa kuwa mikataba mingi inafungwa baina ya mashirika haya na vijiji Halmashauri zinapaswa kuwa sehemu ya mikataba na kuhakikisha kuwa sehemu ya fedha zinaingia kama mapato kwa Halmashauri hizi.

Viongozi wa Mkoa kuhamasisha kuhusu biashara ya Kaboni kwani biashara hii ni rafiki Kwa mazingira na ina faida kubwa kwa jamiii.

 

Jedweli Na. 31: Takwimu za Ufugaji Nyuki kwa kila Wilaya

Wilaya

Idadi ya mizinga

Uzalishaji wa asali (lita)

Nta (KG)

Mizinga ya Kisasa

Mizinga ya Kienyeji

Mvomero

5512

2814

19558

83

Kilombero

133

2814

20994

250.5

Gairo

2043

300

1700


Ulanga

 522

167

889

23.5

Kilosa

1100

203

846

0

Morogoro

165

0

0

0

JUMLA

9,310

5,687

48,721.8.

357

Chanzo: Takwimu za Halmashauri

MAZINGIRA

Mkoa wa Morogoro unendelea kusimamia utekelezaji wa Sheria ya Mazingira Na. 20 ya mwaka 2004 na kutekeleza mikakati na maagizo mbalimbali ya kitaifa ya kuhifadhi mazingira na vyanzo vya maji. Mikakati hiyo ni; utekelezaji wa agizo la kuhifadhi mazingira na vyanzo vya maji; utekelezaji wa marufuku ya matumizi ya mifuko ya plastiki; utekelezaji wa Kampeni ya Kitaifa ya Usafi wa Mwisho wa mwezi na utekelezaji wa kampeni ya Kitaifa ya Upandaji Miti.

Changamoto kuu za kimazingira za Mkoa wa Morogoro zinazosababishwa na shughuli au matendo ya kibinadamu hususani kilimo, ufugaji, makazi, mahitaji ya nishati ya kuni na mkaa, na uchimbaji wa madini. Shughuli hizi zimesababisha uharibifu wa misitu, uvamizi wa milima na vilima kama vile milima ya Uluguru, uharibifu wa ardhioevu kama vile bonde la Mto Kilombero na uharibifu wa maeneo mengine ya hifadhi ya vijiji kwa kutaja machache.

Hatua Zilizochukuliwa Kutatua Changamoto Hizo

Kuandaa Mkakati wa Kuondoa wavamizi wa vyanzo vya maji katika Milima ya Uluguru. Mkakati huu umeandaliwa na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Morogoro.

Kupandisha hadhi eneo la hifadhi ya Kilombero (Kilombero Game Controlled area) kuwa pori la akiba (Kilombero Game Reserve) ambapo sasa shughuli za kibinadamu hazitaruhusiwa kufanyika ndani ya eneo la Hifadhi. Vilevile, jumuia ya Wanyama pori ya Wami-Mbiki imepandishwa na kuwa pori la akiba

Kundoa mifugo katika maeneo ya hifadhi na vyanzo vya maji. Kwa mfano mifugo zaidi ya 19,000 iliondolewa kata ya Kolelo, Bwakila juu, matombo, na mvuha katika halmashauri ya Morogoro kati ya tarehe 13 hadi 22 mwezi wa October 2022. Aidha, katika bonde la Kilombero jumla ya ngombe 500,000 waliondolewa katika nyakati tofauti.

Utekelezaji wa miradi ya kuhimili mabadiliko ya tabia nchi katika Wilaya ya Mvomero (eco-system based adaptaptation for rural resiliance). Ambapo katika mradi huu rambo moja la mifugo linajengwa, visima vinne vinajimbwa katika Kijiji cha Melela na mfereji wenye urefu wa kilomiter 2.75 katika Kijiji cha Lukenge unakarabatiwa

Kusafisha mito ya Mgeta, Mlali, Lukurunge, Mgera, na Ngerengere ili kutoa tope na udongo uliojaa ambao unazuia mtiririko wa maji kwa kuanzia mwezi august, 2022.

Kuondoa wachepushaji wa maji, wazibaji wa mto na wachenjuaji wa madini katika mito ya Mvuha, Mngazi, Dutumi, na Kibungo.

Kuweka alama (beacons) katika mito eneo la mita 60 ya hifadhi ya mito kwa mito ya Mlali, Mkurunge, Morogoro, Dutumi, na Kibungo. Ambapo alama zaidi 2,000 zimewekwa katika maeneo hayo

Aidha, Mkoa wa Morogoro umeendelea kutekeleza agizo la serikali la kudhibiti matumizi ya mifuko ya plastiki. Shughuli zilizotekelezwa ni pamoja na:

Kuandaa kikosi kazi cha utekelezaji wa agizo kwa kila halmashauri

Utengaji wa maeneo maalum ya kuhifadhia mifuko itakayopatikana

Utoaji elimu kuhusu katazo na kuhamasisha matumizi ya mifuko mbadala.

Kufanya ukaguzi wa maeneo mbalimbali kubaini mifiko iliyopo na kuratibu ukusanyaji

Uwekaji wa mabango kwenye maeneo ya kimkakati ili kuhabarisha umma kuhusu katazo hilo na

Kuzihabarisha taasisi hususan shule, hospitli, vituo vya afya, masoko, asasi za kiraia na mashirika ya dini kuhusu katazo.

Changamoto za Utekelezaji wa Marufuku ya Matumizi ya Mifuko ya Plastiki

Uwepo na ongezeko la usambazaji wa mifuko hii katika maeneo mbalimbali mkoani Morogoro.

Vifungashio kutumika kama Vibebeo

Utatuzi wa Changamoto

Kuendelea kufanya Operation Mbalimba katika Masoko na Maduka ili kubaini mifuko ya plastiki isiyo na kiwango na kuiteketeza

Kuendelea kutua elimu kwa wafanyabiasha juu ya mathara ya matumi ya mifuko ya Plastiki iliyopigwa marufuku na matumizi ya mifuko mbadala

Kubaini Viwandaau njia za usambazaji wa mifuko iliyopigwa marufuku na kuchukua hatua za kisheria

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • Vyama vya Ushirika Vyatakiwa Kutumia TEHAMA

    May 14, 2025
  • ZINGATIENI SHERIA, KATIBA NA KANUNI YA VYAMA VYENU - MUTUNGI.

    May 14, 2025
  • WANAFUNZI 214 WA KIDATO CHA KWANZA SEKONDARI ZA MONGOLA, MGETA WAPEWA MICHE 2140 YA MIKARAFUU

    May 13, 2025
  • RC MALIMA ATOA WITO KWA WANANCHI KUSHIRIKI MAADHIMISHO MIAKA 80 YA HOSPITALI, AMSHUKURU RAIS SAMIA.

    May 13, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.