• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Huduma za Uvuvi

Sekta ya Uvuvi

Utangulizi.

Katika Mkoa wa Morogoro sehemu kubwa ya uvuvi hufanyika kutokea kwenye  kambi za wavuvi kandokando ya mto Kilombero. Kuna  aina  zaidi ya 52 ambapo  zaidi ya 90% ya samaki wote wanapatikana kutokea mto Kilombero. Baadhi ya aina hizo ni  Kitoga, Kambale, Perege, Njege, Ndungu, Bura, Ningu, Mgundu, Mbala, Mjongwa, Ngulufi, Mbewe, Ngogo, Sulusulu na Mkunga. Uvuvi mwingine kwa kiwango kidogo hufanyika katika mabwawa ya asili, ya kuchimbwa na mito imwagayo maji yake katika bonde la mto Rufiji.

Ufugaji wa Samaki katika Mkoa

Mkoa umeendelea kutoa elimu na kuhamasisha wananchi kufuga samaki katika mabwawa ya kuchimbwa ili kuongeza upatikanaji wa samaki Mkoani na pia kupunguza utegemezi katika vyanzo vya asili. Kutokana na uhamasishaji huo Mkoa kwa sasa una jumla ya mabwawa ya kuchimbwa 857 yanayokadiriwa kuzalisha zaidi ya tani 30 kwa mwaka. Mchanganuo wa mabwawa ya samaki kwa kila Halmashauri ni kama inavyoonyesha katika jedwali Na. 1 hapo chini.

Jedweli Na. 20: Mabwawa ya Samaki katika Halmashauri

Na.

HALMASHAURI

IDADI

1.
Ifakara

37

2.
Mlimba

25

3.
Kilosa

230

4.
Malinyi

15

5.
Morogoro MC

175

6.
Morogoro DC

146

7.
Mvomero

104

8.
Ulanga

90

9.
Gairo

35

JUMLA

857

Chanzo: Taarifa kutoka Halmashauri

 

Uzalishaji wa Samaki katika Mkoa

Katika kuongeza uzalishaji wa samaki Mkoani, elimu ya ufugaji wa samaki imekuwa ikitolewa kwa wananchi na udhibiti wa uvuvi haramu kwenye vyanzo vya asili umekuwa ukifanyika kwa kutumia doria, elimu na vikundi vya ulinzi wa rasilimali ya uvuvi (BMUs). Hivyo kutokana na vyanzo vilivyopo Mkoani, msimu wa mwaka 2021/2022 uzalishaji ulikuwa tani 192.3 zenye thamani ya shilingi 972,555,110 ikilinganishwa na mwaka 2020/2021 ambapo uzalishaji ulikuwa tani 279.5 zenye thamani ya shilingi.1,307,018,617.75. 

 

Uzalishaji umepungua kwa kiasi kikubwa kwa sababu sehemu kubwa ya bonde la Mto Kilombero lilikuwa pori tengefu na sasa limekuwa pori la akiba na hivyo kusababisha wavuvi wengi kushindwa kuingia kuvua samaki kutokana na masharti yaliyowekwa hususani viwango vya tozo ambavyo wengi wao wanashindwa kuvimudu. Mchanganuo wa uzalishaji kwa kila Halmashauri kwa kipindi cha miaka 2 ni kama inavyoonyesha katika jedwali Na. 2 hapo chini.

 

 

Jedweli Na. 21: Mavuno ya Samaki kwa Msimu wa Mwaka 2020/2021 ikilinganishwa na Mwaka 2021/2022 katika Halmashauri

Na.

HALMASHAURI

2020/2021

2021/2022

UZITO (tani)

THAMANI (Tsh)

UZITO (tani)

THAMANI (Tsh)

1.

Mlimba

89.2

369,178,217.75

32.6

125,333,110

2.

Kilosa

47.6

237,930,000.00

51

305,340,000

3.

Morogoro MC

12.1

72,357,500.00

11

20,389,500

4.

Ulanga

32.9

132,228,250.00

22

111,881,150

5.

Mvomero

4.4

21,930,000.00

3.8

23,279,000

6.

Morogoro DC

2.1

11,312,000.00

1.3

7,608,000

7.

Ifakara Mji

41.4

239,144,200.00

43.8

251,912,500

8.

Malinyi

49.8

222,938,450.00

26.8

126,811,850

9.

Gairo

0

0

0

0

 

JUMLA

279.5

1,307,018,617.75

192.3

972,555,110

 

Changamoto katika Sekta ya Uvuvi

Kuna changamoto nyingi ambazo zinajitokeza katika sekta ya uvuvi. Miongoni mwa changamoto hizo ni kama ifuatavyo:

Upungufu au ukosefu wa wataalamu wa Uvuvi katika mamlaka za Serikali za Mitaa unapunguza ufanisi katika kutekeleza majukumu. Mahitaji ya wataalamu wa uvuvi katika Makao Makuu ya Halmashauri ni 18, waliopo ni 12, hivyo upungufu ni 6. Aidha mahitaji katika ngazi ya kata ni 214, waliopo 3 na hivyo pungufu ni 211.

Ukosefu wa vitendea kazi hususani magari na boti za doria kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa unakwamisha ufanisi katika kutekeleza majukumu.

Matumizi ya zana au njia haramu za uvuvi yaani makokoro, nyavu zenye macho madogo na matumizi ya sumu vinatishia ustawi wa samaki

Uhaba wa maji ya kutosha hususani wakati wa kiangazi husababisha mabwawa mengi ya kufugia samaki kuwa ya msimu.

Halmashauri kutorejesha 5% ya mapato yatokanayo na shughuli za uvuvi kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli za uvuvi.

Mapendekezo ya Utatuzi wa Changamoto na Mikakati Iliyopo Kuongeza Uzalishaji wa Samaki

Halmashauri ziendelee kuomba kibali cha kuajiri Maafisa Uvuvi angalau kila Kata iwe na Afisa Uvuvi ili elimu ya kutosha kuhusu rasilimali hii ya samaki isambazwe kwenye maeneo yote Mkoani.

Wakurugenzi wasisitizwe kutenga bajeti za ununuzi wa boti za doria katika mipango yao.

Kuendelea kutoa elimu za mara kwa mara kwa wavuvi na wafugaji wa samaki ili watambue umuhimu wa kuwepo kwa rasilimali ya samaki kwa kizazi cha sasa na kijacho.

Kuendelea kuhamasisha jamii kuchimba mabwawa ya kufugia samaki na hatimaye kupunguza utegemezi katika vyanzo vya asili.

Kuendelea kusisitiza Halmashauri kuendesha doria mara kwa mara hasa katika maeneo yenye uharibifu mkubwa wa mazingira ili kuhakikisha sheria na kanuni zinafuatwa.

Kuendelea kutoa elimu kwa wakulima kupandikiza vifaranga bora na pia kutumia chakula bora cha samaki ili wazalishe kwa tija.

Kuimarisha vikundi vya ulinzi wa rasilimali ya uvuvi (BMUs) katika maeneo yote ya uvuvi.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • Vyama vya Ushirika Vyatakiwa Kutumia TEHAMA

    May 14, 2025
  • ZINGATIENI SHERIA, KATIBA NA KANUNI YA VYAMA VYENU - MUTUNGI.

    May 14, 2025
  • WANAFUNZI 214 WA KIDATO CHA KWANZA SEKONDARI ZA MONGOLA, MGETA WAPEWA MICHE 2140 YA MIKARAFUU

    May 13, 2025
  • RC MALIMA ATOA WITO KWA WANANCHI KUSHIRIKI MAADHIMISHO MIAKA 80 YA HOSPITALI, AMSHUKURU RAIS SAMIA.

    May 13, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.