• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Huduma za Uvuvi

SEKTA YA UVUVI

Mkoa wa Morogoro umejaliwa kuwa na mito na mabwawa yenye samaki wengi. Sehemu kubwa ya uvuvi hufanyika kutokea kwenye  kambi za wavuvi kandokando ya mto Kilombero.  Kuna  aina  zaidi ya 52 ambapo  zaidi ya 90% ya samaki wote wanapatikana kutokea mto Kilombero. Uvuvi mwingine kwa kiwango kidogo hufanyika katika mabwawa ya asili, ya kuchimbwa na mito imwagayo maji yake katika bonde la mto Rufiji. Kutokana na vyanzo hivyo vyote, kila mwaka mkoa unakadiriwa kuzalisha samaki zaidi ya  tani 350.

Ufugaji wa samaki

Mkoa kwa kushirikiana na Halmashauri umeendelea kutoa elimu na kuhamasisha wananchi kufuga samaki katika mabwawa ya kuchimbwa ili kuongeza upatikanaji wa samaki Mkoani na pia kupunguza utegemezi katika vyanzo vya asili. Kutokana na uhamasishaji huo mkoa una jumla ya mabwawa ya kuchimbwa 674. Mchanganuo wa mabwawa ya samaki kwa kila Halmashauri ni kama inavyoonyesha katika jedwali Na. 1 hapo chini.

Jedwali Na. 1: Mabwawa ya samaki katika Halmashauri

Na.
HALMASHAURI
IDADI
1.
Ifakara Mji

37

2.
Kilombero

97

3.
Kilosa

52

4.
Malinyi

56

5.
Morogoro MC

75

6.
Morogoro DC

206

7.
Mvomero

96

8.
Ulanga

55

9.
Gairo

-

JUMLA 

674

                    Chanzo: Taarifa kutoka Halmashauri

 

Uzalishaji wa samaki

Katika kuongeza uzalishaji wa samaki Mkoani, elimu ya ufugaji wa samaki imekuwa ikitolewa kwa wananchi na udhibiti wa uvuvi haramu kwenye vyanzo vya asili umekuwa ukifanyika kwa kutumia doria, elimu na vikundi vya ulinzi wa rasilimali ya uvuvi (BMUs). Hivyo kutokana na vyanzo vilivyopo Mkoani uzalishaji umeongezeka kutoka tani 282.4 zenye thamani ya shilingi 1,568,543,045.5 mwaka 2016/2017  hadi kufikia  tani 475.9 zenye thamani ya shilingi 2,528,230,683.76 mwaka 2017/2018. Mchanganuo wa uzalishaji kwa kila Halmashauri kwa kipindi cha miaka 2 ni kama inavyoonyesha katika jedwali Na. 2 hapo chini.

Jedwali Na. 2: Mavuno ya samaki kwa msimu wa mwaka 2017/2018 ikilinganishwa na mwaka 2016/2017 katika Halmashauri

Na.
HALMASHAURI

2016/2017

2017/2018

UZITO (tani)
THAMANI (Tsh)
UZITO (tani)
THAMANI (Tsh)
1.
Kilombero

187.8

1,039,985,692.25

158.9

684,501,589.26

2.
Kilosa

1.7

9,801,500

6.75

35,025,000

3.
Morogoro MC

5.3

41,814,000

2.63

9,758,500

4.
Ulanga  DC

25.1

101,980,200

25.98

93,373,820

5.
Mvomero

6.1

33,715,000

4.156

25,863,000

6.
Morogoro DC

2.5

10,000,000

3.25

14,878,000

7.
Ifakara Mji

50.4

310,546,653.25

59.67

356,477,774.5

8.
Malinyi

3.5

20,700,000

214.6

1,308,353,000

9.
Gairo

-

-

-

-

 
JUMLA

282.4

1,568,543,045.5

475.936
2,528,230,683.76

Chanzo: Taarifa kutoka Halmashauri

 

3.3: Changamoto katika sekta ya Uvuvi.

Kuna changamoto nyingi ambazo zinajitokeza katika suala zima la sekta ya uvuvi. Miongoni mwa changamoto hizo ni kama ifuatavyo:

  • Matumizi ya zana au njia haramu za uvuvi; makokoro,nyavu zenye macho madogo na matumizi ya sumu vinatishia ustawi wa samaki.
  • Uharibifu wa mazingira katika bonde la Kilombero na mabwawa ya asili unaofanywa na wafugaji waliovamia maeneo hayo pia unahatarisha ustawi wa samaki.
  • Uhaba wa maji ya kutosha hususani wakati wa kiangazi husababisha mabwawa mengi kuwa ya msimu.
  • Mabadiliko ya tabia nchi yamesababisha kuongezeka kwa ukame kiasi kwamba mito mingi ya asili imekauka na kusababisha kutoweka kwa samaki katika baadhi ya mito na mabwawa.
  • Upungufu wa wataalamu wa uvuvi, fedha na vitendea kazi unapunguza  ufanisi wa usimamizi wa rasilimali hii muhimu.

3.4 Ufumbuzi wa changamoto

  • Kutoa  elimu za mara kwa mara kwa wavuvi na wafugaji wa samaki ili watambue umuhimu wa kuwepo kwa rasilimali ya samaki kwa kizazi cha sasa na kijacho.
  • Kuendelea kuhamasisha jamii kuchimba mabwawa ya kufugia samaki na hatimaye kupunguza utegemezi katika mito.
  • Kuendesha doria mara kwa mara hasa katika maeneo yenye uharibifu mkubwa wa mazingira ili kuhakikisha sheria na kanuni zinafuatwa.
  • Kuongeza kasi ya usambazaji wa maji mijini na vijijini.
  • Sekta ya Uvuvi itengewe kiasi cha fedha cha kutosha na kuendelea kuajiri wataalamu wa uvuvi ili elimu ya kutosha kuhusu rasilimali hii ya samaki itolewe.
  •  





































































































Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • MAONESHO YA NANENANE July 27, 2022
  • View All

Habari Mpya

  • WAALIMU WAAGIZWA KUSIMAMIA USALAMA NA MALEZI BORA KWA WANAFUNZI.

    January 28, 2023
  • MAAFISA ELIMU WAAGIZWA KUSIMAMIA MATUMIZI YA FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELEO

    January 28, 2023
  • RC FATMA MWASSA AWAAPISHA WAKUU WA WILAYA WAWILI.

    January 27, 2023
  • REA MKOANI MOROGORO KUMCHUKULIA HATUA MKANDARASI WA KAMPUNI YA HXJDL.

    January 26, 2023
  • View All

Video

Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.