SEKTA YA UVUVI
Mkoa wa Morogoro umejaliwa kuwa na mito na mabwawa yenye samaki wengi. Sehemu kubwa ya uvuvi hufanyika kutokea kwenye kambi za wavuvi kandokando ya mto Kilombero. Kuna aina zaidi ya 52 ambapo zaidi ya 90% ya samaki wote wanapatikana kutokea mto Kilombero. Uvuvi mwingine kwa kiwango kidogo hufanyika katika mabwawa ya asili, ya kuchimbwa na mito imwagayo maji yake katika bonde la mto Rufiji. Kutokana na vyanzo hivyo vyote, kila mwaka mkoa unakadiriwa kuzalisha samaki zaidi ya tani 350.
Ufugaji wa samaki
Mkoa kwa kushirikiana na Halmashauri umeendelea kutoa elimu na kuhamasisha wananchi kufuga samaki katika mabwawa ya kuchimbwa ili kuongeza upatikanaji wa samaki Mkoani na pia kupunguza utegemezi katika vyanzo vya asili. Kutokana na uhamasishaji huo mkoa una jumla ya mabwawa ya kuchimbwa 674. Mchanganuo wa mabwawa ya samaki kwa kila Halmashauri ni kama inavyoonyesha katika jedwali Na. 1 hapo chini.
Jedwali Na. 1: Mabwawa ya samaki katika Halmashauri
Na.
|
HALMASHAURI
|
IDADI
|
1.
|
Ifakara Mji
|
37 |
2.
|
Kilombero
|
97 |
3.
|
Kilosa
|
52 |
4.
|
Malinyi
|
56 |
5.
|
Morogoro MC
|
75 |
6.
|
Morogoro DC
|
206 |
7.
|
Mvomero
|
96 |
8.
|
Ulanga
|
55 |
9.
|
Gairo
|
- |
JUMLA
|
674 |
Chanzo: Taarifa kutoka Halmashauri
Uzalishaji wa samaki
Katika kuongeza uzalishaji wa samaki Mkoani, elimu ya ufugaji wa samaki imekuwa ikitolewa kwa wananchi na udhibiti wa uvuvi haramu kwenye vyanzo vya asili umekuwa ukifanyika kwa kutumia doria, elimu na vikundi vya ulinzi wa rasilimali ya uvuvi (BMUs). Hivyo kutokana na vyanzo vilivyopo Mkoani uzalishaji umeongezeka kutoka tani 282.4 zenye thamani ya shilingi 1,568,543,045.5 mwaka 2016/2017 hadi kufikia tani 475.9 zenye thamani ya shilingi 2,528,230,683.76 mwaka 2017/2018. Mchanganuo wa uzalishaji kwa kila Halmashauri kwa kipindi cha miaka 2 ni kama inavyoonyesha katika jedwali Na. 2 hapo chini.
Jedwali Na. 2: Mavuno ya samaki kwa msimu wa mwaka 2017/2018 ikilinganishwa na mwaka 2016/2017 katika Halmashauri
Na.
|
HALMASHAURI
|
2016/2017 |
2017/2018 |
||
UZITO (tani)
|
THAMANI (Tsh)
|
UZITO (tani)
|
THAMANI (Tsh)
|
||
1.
|
Kilombero
|
187.8 |
1,039,985,692.25 |
158.9 |
684,501,589.26 |
2.
|
Kilosa
|
1.7 |
9,801,500 |
6.75 |
35,025,000 |
3.
|
Morogoro MC
|
5.3 |
41,814,000 |
2.63 |
9,758,500 |
4.
|
Ulanga DC
|
25.1 |
101,980,200 |
25.98 |
93,373,820 |
5.
|
Mvomero
|
6.1 |
33,715,000 |
4.156 |
25,863,000 |
6.
|
Morogoro DC
|
2.5 |
10,000,000 |
3.25 |
14,878,000 |
7.
|
Ifakara Mji
|
50.4 |
310,546,653.25 |
59.67 |
356,477,774.5 |
8.
|
Malinyi
|
3.5 |
20,700,000 |
214.6 |
1,308,353,000 |
9.
|
Gairo
|
- |
- |
- |
- |
|
JUMLA
|
282.4 |
1,568,543,045.5 |
475.936
|
2,528,230,683.76
|
Chanzo: Taarifa kutoka Halmashauri
3.3: Changamoto katika sekta ya Uvuvi.
Kuna changamoto nyingi ambazo zinajitokeza katika suala zima la sekta ya uvuvi. Miongoni mwa changamoto hizo ni kama ifuatavyo:
3.4 Ufumbuzi wa changamoto
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
||
|
|
|
|
||
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.