• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Huduma za Watumishi


WATUMISHI WA MKOA

Utekelezaji wa majukumu ya Sekretariati unaongozwa kwa mujibu wa sheria  ya Tawala za Mikoa Na. 19 ya mwaka 1997 ambayo inatambua uwepo wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na kuainisha majukumu ya Ofisi hiyo. Ili kurahisisha utekelezaji wa majukumu yaliyoainishwa na sheria hiyo, Serikali iliunda muundo wa kiutawala wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa kuzingatia sekta mbalimbali. Muundo huo unajumuisha Sehemu (Sections) nane na vitengo (units) vitano

Kwa mujibu wa Sheria hiyo shughuli au majukumu ya Mkoa yanatekelezwa na kuongozwa na Mkuu wa Mkoa kwa kushirikiana na Katibu Tawala wa Mkoa ambaye ni Mtendaji Mkuu na Afisa Masuuli (Accounting Officer). Chini ya Viongozi hao wawili (2) kuna Wakuu wa Sehemu nane (8) na Vitengo vitano (5) na kwa pamoja husimamia utekelezaji wa majukumu/ utendaji mzima unaoelekezwa au unaotakiwa kufanywa kwa kila siku.  Sehemu na Vitengo vya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa  ni kama ifutavyo;

 

Sehemu

Sehemu ya Utawala na Rasilimali watu

Sehemu ya Mipango na Uratibu

Sehemu ya Uchumi na Uzalishaji Mali

Sehemu ya Miundo Mbinu

Sehemu ya Menejimenti ya Serikali za Mitaa

Sehemu ya Maji

Sehemu ya Afya

Sehemu ya Elimu

Vitengo

Uhasibu

Sheria

Ugavi

Ukaguzi wa Ndani

Tehama

Nafasi za wakuu wa sehemu na baadhi ya vitengo katika  Sekretarieti ya Mkoa zimekwisha jazwa. Vitengo ambavyo wakuu wake wanakaimu ni kitengo cha sheria, Tehama na Kitengo cha manunuzi, pia yapo mapungufu na nafasi wazi ya baadhi ya wataalam. Jumla ya watumishi wanaotakiwa ni 1,111  kati ya hao waliopo ni 818 na pungufu ni 276 ambayo ni upungufu wa asilimia 14.8.  Mpaka tarehe 31 Januari, 2017, idadi ya Watumishi wote katika Sekretarieti ya Mkoa na Serikali za Mitaa  ni 24,467 Mchanganuo wa watumishi waliopo na Ikama ya Watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa ni kama ifuatavyo;-.

Ikama ya Watumishi katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro hadi Machi, 2016

NA.
SEHEMU/KITENGO
IKAMA
WALIOPO
UPUNGUFU
1
Utawala na Utumishi
71
52
19
2
Mipango na Uratibu
8
8
0
3
Miundombinu
9
8
2
4
Serikali za Mitaa
10
7
3
5
Huduma za Maji
5
3
2
6
Huduma za Elimu
7
5
2
7
Uchumi na Uzalishaji
19
17
2
8
Huduma za Afya na Ustawi wa Jamii.
8
8
0
9
Uhasibu na Fedha
12
11
1
10
Sheria
2
2
0
11
Ukaguzi wa Ndani
3
3
0
12
Manunuzi na Ugavi
3
3
0
13
TEHAMA
6
3
2
14
Ofisi ya Mkuu wa  Wilaya Morogoro
48
19
29
15
Ofisi ya Mkuu wa  Wilaya Kilosa
53
26
27
16
Ofisi ya Mkuu wa  Wilaya Kilombero
43
24
19
17
Ofisi ya Mkuu wa  Wilaya Mvomero
38
13
25
18
Ofisi ya Mkuu wa  Wilaya Ulanga
40
9
31
19
Ofisi ya Mkuu wa  Wilaya Gairo
28
7
21
20
Ofisi ya Mkuu wa  Wilaya Malinyi
18
6
12
21
Hospitali ya Rufaa ya Mkoa
680
584
79
 
Jumla
1,111
818
276

 

 

Jedwali Na.3 Idadi ya Watumishi katika Mkoa

Mkoa/Halmashauri
Mahitaji
Waliopo
Upungufu
Mkoa
1,111
818
276
H/Manispaa Morogoro
4018
4137
+73
Morogoro DC
3299
2870
429
Mvomero
4180
3239
941
Kilosa
3039
2861
178
Kilombero
1545
968
577
Ulanga
2695
1754
941
Gairo
1858
1427
451
Malinyi
1626
887
680
Ifakara TC
1096
998
99
JUMLA
24,467
 
19,965
4583

Chanzo: Taarifa za Mkoa na Wilaya ,2017

HALI YA UTUMISHI NA UTAWALA KATIKA SEKRETARIETI YA  MKOA

 

  1. Utumishi

Watumishi katika Sekretariati ya Mkoa inawajumuisha Watumishi waliopo Makao Makuu ya Mkoa, Ofisi za Wakuu wa Wilaya 7 na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa. Kwa mujibu wa Ikama ya Mkoa wetu wanahitajika Watumishi 1,111 hadi taarifa hii inapowasilishwa kuna Jumla ya Watumishi/Viongozi wa kuteuliwa katika kada/ngazi mbalimbali 789 hivyo  kuwa na upungufu wa watumishi 322

 

Majukumu yaliyotekelezwa

Idara inaendelea kutekeleza jukumu muhimu la usimamizi na uendelezaji wa Rasilimali watu ambalo limesaidia kuimarisha utendaji kazi wa watumishi, ustawi na hali zao mahali pa kazi ambao umefanikisha kwa kipindi chote huduma bora kwa wananchi.

Ili kutekeleza adhma ya Serikali ya kuhakikisha watumishi wa umma wapo kwa mujibu wa Sheria, Kanuni na Taratibu na kudhibiti ajira zisizostahili, Watumishi 31 wameondolewa katika utumishi wa Umma kutokana na kubainika kughushi vyeti na 2 kwa sababu za kimuundo yaani kutokuwa na vyeti vya kidato cha nne wakati masharti ya ajira zao zinahitaji wawe na sifa hiyo. Aidha, watumishi 2 walibainika kuwa ni hewa wakati wa zoezi la kuhakiki watumishi.

Tunashukuru Serikali kwa utekelezaji wa masuala mbalimbali ambayo yatasaidia kuboresha hali ya utumishi na motisha kwa watumishi wake yakiwemo yafuatayao;

Kuanza kutoa vibali vya ajira mpya ambavyo hadi sasa wamepatikana watumishi 5 (4 wa Afya na 1 Utawala) kati ya 22 walioombwa katika kibali cha mwaka 2015/2016. Vipaombele vya watumishi ni katika eneo la Afya na maeneo mapya ya Utawala yaani Wilaya ya Malinyi na Gairo.

Kulipa madeni mbalimbali ya watumishi katika mwaka wa fedha wa 2016/2017.

Kulipa madeni ya gharama za samani kwa viongozi ya kiasi cha shilingi 112,000,000

Kutoa nafasi ya kuwapandisha vyeo watumishi 82 wanaostahili

 

  1. Utawala

Utekelezaji wa jukumu hili katika Mkoa umejikita kwenye usimamizi wa milki na vifaa vinavyotumika na watumishi na viongozi katika ngazi ya Mkoa na Wilaya. Serikali imetekeleza wajibu wake kwa kiasi kikubwa kuwezesha upatikanaji wa vifaa muhimu vinavyotumika na watumishi/viongozi ili kutekeleza majukumu yao. Pamoja na hatua hizo zilizochukuliwa na Serikali bado kuna changamoto ya uchakavu wa vifaa na miundombinu ya muda mrefu pamoja kuanzishwa kwa maeneo mapya ya Utawala ya Wilaya ya Malinyi na Gairo.

Maeneo ya kipekee yanayohitaji kushughulikiwa kwa haraka ni yafuatayo;


Eneo
Hali kwa sasa
Njia mbadala
1
Ununuzi wa Gari la Mkuu wa Mkoa
Liliharibika baada ya kupata ajali
Kuazima la Mkuu wa Wilaya Mvomero
2
Ununuzi wa Gari la Katibu Tawala wa Mkoa
Liliharibika
Kutumia la Idara
3
Ununuzi wa Gari la Mkuu wa Wilaya Malinyi
Halikuwahi kununuliwa
Kuazimwa la Idara japo ni bovu

Ujenzi wa nyumba na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Malinyi
Wilaya mpya
Kuazimwa vyumba 3 katika Hospitali ya Lugala
4
Ujenzi wa nyumba na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Gairo
Wilaya iliyoanzishwa mwaka 2012
Kutumia sehemu ya Jengo la Mamlaka ya Mji Mdogo Gairo na Resti house ya Halmashauri
5
Ununuzi wa Gari la Mkuu wa Wilaya Kilosa
Lililopo ni chakavu hivyo kuwa na gharama kubwa za matengenezo
Kulikarabati mara kwa mara.

Pamoja hali iliyoelezwa hapo juu utekelezaji wa majukumu kwa viongozi hao na wengine wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na Wakuu wa Wilaya zimeendelea kutekelezwa ipasavyo.

 Hitimisho

Mkoa wa Morogoro kwa ushirikiano na Halmashauri za Wilaya , wananchi, Wadau, Wahisani na Asasi mbalimbali     wote kwa pamoja wanatekeleza majukumu yao kikamilifu katika kujiletea Maendeleo ya Kiuchumi na Kijamii. Mafanikio yaliyopatikana katika Serikali ni matokeo ya Uongozi      wa pamoja, uwajibikaji na uwazi katika kuleta maendeleo             stahimili.

Tutaendeleza juhudi mbalimbali za kuvutia wawekezaji katika  maeneo mbalimbali katika Mkoa wa Morogoro ili kufanikisha mapinduzi ya uchumi wa viwanda. Mafanikio  ya juhudi  hizo yatakuwa chachu ya ongezeko la ajira na kukuza   uchumi kwa wananchi na Taifa  kwa ujumla.

Azma ya Mkoa ni kuhakikisha kuwa mazingira bora ya utoaji huduma kwa wananchi yanaendelea kuboreshwa.  Mkoa unahitaji             ujitosheleze kwa chakula kwa malengo aliyopewa kwa malengo aliyopewa na kuboresha hali ya mazingira yake.  Kuongezeka kwa vitendo vya uharibifu wa mazingira kutachochea zaidi kuongezeka kwa umaskini miongoni mwa wanamorogoro.  Kwa ujumla azma ya kuleta maendeleo endelevu kwa wananchi ikifikiwa basi lengo la kufikia uchumi wa kati na kumpatia maisha bora mwananchi wa Mkoa wa Morogoro ifikapo 2025 itafanikiwa.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • Vyama vya Ushirika Vyatakiwa Kutumia TEHAMA

    May 14, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.