• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MALIMA AMUUMA SIKIO DC MVOMERO, KUTUMIA BUSARA ZAIDI.

Posted on: June 27th, 2025



Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Mhe. Adam Kighoma Malima, amemshauri Mkuu mpya wa Wilaya ya Mvomero, Maulid Hassan Dotto kufanya kazi zake kwa kutumia busara zaidi badala ya kutumia mabavu akifuata maadili ya uongozi huku akitambua lengo mahususi kuwa ni kuwafanya wananchi wa wilaya ya Mvomero waishi kwa amani na utulivu.

Mhe. Malima ametoa wito huo Juni 27, 2025, wakati wa hafla fupi ya kumwapisha Mkuu wa Wilaya huyo iliyofanyika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kufuatia uteuzi wa viongozi mbalimbali uliofanywa na Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Juni 23 mwaka huu.

Mhe. Malima amesema, maamuzi ya busara ni bora zaidi kuliko maamuzi yale ya kutumia nguvu, mabavu na kutumia vyombo mbalimbali alivyokabidhiwa kumsaidia huku akimsisitiza kwenda kufanya kazi bila ubaguzi wa rangi, kabila au dini.

“Nakutakia kila la heri. Maamuzi mengi yanapaswa kufanywa kwa misingi ya busara kuliko kutumia mabavu,” amesisitiza Mhe. Adam Malima.

Katika hatua nyingine amemkumbusha Maulid Hassan kwamba hiki ni kipindi cha kuelekea uchaguzi Mkuu wa Urais, wabunge na Madiwani, hivyo amemtaka kwenda kuimarisha hali ya ulinzi na usalama Wilayani humo ili uchaguzi ujao katika Wilaya hiyo ufanyike kwa Haki, Amani na Utulivu.

Naye katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Alhaji Dkt. Mussa Ali Mussa amemtaka kwenda kuendeleza mazuri yaliyofanywa na mtangulizi wake hususan programu ya TUTUNZANE ambayo imeleta matunda mema baina ya wakulima na wafugaji wa Wilaya ya Mvomero hivyo akaiimarishe ili makundi hayo yaendelee kuishi kwa amani  kama ilivyo sasa.

Kwa upande wake Kaimu Katibu Msaidizi kutoka Ofisi ya Rais – Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Mashariki Selemani Shabani Selemani amemtaka Mkuu huyo wa Wilaya kuishi kwa kufuata kiapo cha maadili alichoweka leo huku akimtakia utekelezaji mwema wa majukumu yake.

Mhe. Maulid Hassan alipopewa fursa ya kusema neno, pamoja na kumshukuru Mkuu wa Mkoa kwa mapokezi yake mazuri, amemshukuru Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kumuamini huku akiahidi kufanya kazi kwa bidii kwa ajili ya wananchi wa Wilaya ya Mvomero na Taifa kwa ujumla.


MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AMUUMA SIKIO DC MVOMERO, KUTUMIA BUSARA ZAIDI.

    June 27, 2025
  • RC MALIMA AENDELEA NA MAONO YA KUKUZA KILIMO MKOANI MOROGORO.

    June 27, 2025
  • Maadhimisho ya miaka 80 hospitali ya Rufaa Morogoro yaanza kuleta Matokeo

    June 25, 2025
  • RC MALIMA AENDELEA KUPAMBANA KUTATUA KERO YA MAJI MANISPAA YA MOROGORO.

    June 21, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.