• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Morogoro yajizatiti kivitendo kuitwa Ghala la Taifa

Posted on: February 15th, 2021

Mkoa wa Morogoro uko mafichoni kwa sasa kwa ajili ya kujitathmini na kuweka mpango mkakati wa kurudisha heshima ya Mkoa huo kuitwa ghala la Taifa ili jina hilo litafisiliwe kwa vitendo zaidi.

Hayo yamebainishwa Februari 15 mwaka huu na Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Mhandisi Emmanuel Kalobelo wakati akifungua kikao cha kuhuisha mpango mkakati wa maendeleo wa sekretarieti na mamlaka ya serikali za mitaa kinachoendelea kufanyika Mkoani humo.

Mhandisi kalobelo amesema bado anaendelea kujiuliza swali ambalo Dkt. John Pombe Magufuli amekuwa akijiuliza mara nyingi sababu ya Tanzania kuwa maskini ilhali ina utajiri wa kutosha, hali kadhalika amesema Morogoro ni moja ya mikoa hapa nchini yenye utajiri wa kila aina haoini sababu ya kuwa maskini.

Amesema haoni sababu ya Mkoa kuendelea kuimba kuwa ghala la taifa bila kuona manufaa yake wala uhalisia wa kaulimbiu hiyo, hivyo amewataka wadau wa kikao hicho wanaoendelea kuandaa Mpango mkakati wa maendeleo wa sekretarieti na mamlaka ya serikali za mitaa kinachoendelea kufanyika Mkoani humo kurejesha kwa vitendo kauli hiyo.

“Mpango Mkakati huu utuambie kwa sababu tuna ardhi nzuri ya Kilimo, basi tunataka mwaka huu zao Fulani lisipungue kiasi hiki na ndani ya miaka mitano uzalishaji wetu ufikie huku” alisisitiza Mhandisi Kalobelo.

Katika kikao hicho ambacho kinafanyika katika ukumbi wa Elimu ya Watu Wazima (WAMO) Mhandisi Kalobelo aligusia namna Mkoa unayvotakiwa kujiandaa kutangaza masuala ya Utalii, na vivutio vyote vilivyoko ndani ya Mkoa huo.

Kwa upande wake Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Mipango na Uratibu Anza - Amen Ndossa amesema  bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limepitisha mpango wa tatu wa maendeleo wa miaka mitano 2021-2022 hadi 2025-2026 Mkoa unalazimika kuutafsiri mpango huo kikamilifu kwenye mipango ya maendeleo ya Mkoa na mamlaka ya Serikali za mitaa.

Mkurugenzi wa Idara ya Mipango Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Cosmas Ngangaji amebainisha kuwa mpango Mkakati huo unaoandaliwa utasaidia kuweka shabaha zitakazotekelezwa katika kipindi cha miaka mitano huku matarajio makubwa ni kuwa na uchumi shindani unaoongozwa na mazao yanayotokana na viwanda kwa maendeleo ya wananchi wa Mkoa wa Morogoro.

Naye Mshiriki wa wa Mpango mkakati huo Afisa Elimu Sekondari Manispaa ya Morogoro Janeth Balongo amesema hatua hii ya kutekeleza mpango mkakati sekta ya Elimu inatekeleza Ilani ya Chama Cha Mapinduzi – CCM kwa kuongeza idadi ya wanafunzi wanaojiunga kidato cha kwanza hadi cha nne na kuendelea na ngazi zingine za Elimu ikiwemo Chuo kikuu.

Mpango Mkakati ni nyaraka muhimu ambayo inaoonesha dira ya taasisi kwa miaka mitano ijayo. Uwepo wa mpango huo utaongeza uwajibikaji wa utendaji kazi kuanzia ngazi ya taasisi, Idara, vitengo hadi ngazi ya mtumishi.

Mpango Mkakati huo utaleta uwazi na kuboresha mawasiliano kati ya menejimenti watumishi na wadau wengine wa maendeleo na kuongeza kasi ya utoaji huduma kwa wananchi.

Mpango Mkakati huo una maudhui yasemayo Kujenga uchumi shindani, unaoongozwa na mauzo ya nje na pia utasaidia upangaji mzuri wa rasilimali kwa kuzingatia vipaumbele vya taasisi, lengo kuu la Mpango huo ni kutekeleza mpango mkakati wa Taifa awamu ya tatu.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • Zaidi ya Mil. 125 zachangwa kupitia chakula cha hisani kukarabati Hospitali ya Rufaa Morogoro.

    May 18, 2025
  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.