• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Wananchi Mkoani Morogoro wanufaika na Kuku wanaostahimili Magonjwa.

Posted on: December 10th, 2020

Wananchi hususan wajasiliamali wadogo Mkoani Morogoro wameendelea kunufaika na Mradi wa ufugaji kuku wanaostahimili magonjwa unaoendeshwa na Mradi wa Lishe Endelevu na kufadhiliwa na shirika la Misaada ya Kimataifa  kutoka  Marekani (USAID) hivyo kuendelea kukuza uchumi wao

Hayo yamethibitika Disemba 10, 2020 wakati Meneja wa Mradi wa Lishe Endelevu Mkoa wa Morogoro Bw. Nuhu Yahya, alipokuwa anakabidhi kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Mhandisi Emmanuel Kalobelo Vifaranga  vya Kuku 800 kwa ajili ya wanavikundi wa Wilayani Kilosa kwa ajili kuwapatia wakulima au wafugaji wa mfano ambao wataendelea kutoa mafunzo kwa akina Mama  wanaowazunguka.

Bw. Yahya amesema wakulima au wafugaji hao wa mfano watapata vifaranga 200 na baada ya mwezi mmoja mfugaji atatakiwa kutoa robo tatu ya vifaranga hivyo kwa vikundi malezi vya kinaMama ambavyo vinapata mafunzo kutoka Mradi huo wa Lishe Endelevu.

kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Mhandisi Emmanuel Kalobelo amewaagiza Wakurugenzi na Maafisa Ugani Mkoani humo kutoa ushirikiano katika mradi huo ili kufikia malengo ya Serikali katika mipango yake ya kuimarisha Lishe bora kwa wananchi.

Mhandisi Kalobelo amesema mradi huo unalenga kuisaidia serikali katika mipango ya kuimarisha Lishe bora kwa wanawake wenye umri wa uzazi na  Kupunguza Udumavu kwa watoto walio chini ya miaka mitano.

Aidha, amesema licha ya mradi huo kupunguza udumavu kwa watoto hao, unakuza shughuli za kiuchumi katika jamii ikiwa ni pamoja na kuongeza kipato hivyo kuwataka wananchi watakaonufaika na mradi huo  kuutunza kikamilifu msaada watakaopewa.

Katika hatua nyingine, Mhandisi Kalobelo ametumia nafasi hiyo kumuagiza Mkuu wa Idara ya Uchumi wa sekretarieti ya Mkoa wa Morogoro, kuongeza uratibu wa programu  ya mradi huo katika kutambua Maafisa Ugani katika kata na Halmashauri namna wanavyo jishughulisha na uendelevu wa programu hiyo.

Naye,  Afisa Kilimo na Mifugo wa shirika la lishe endelevu Agnes January, amesema Jamii imeupokea mradi huo kwa mwitikio chanya kutokana na elimu ambayo wameitoa juu ya faida zinazotokana na Ufugaji wa vifaranga hivyo.

Mradi wa USAID Lishe Endelevu hapa nchini umeanza rasmi mwaka 2018 na kuzinduliwa  rasmi Mei 30, 2019 Mkoani Rukwa na Mhe. Selemani Jafo Waziri katika Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Mradi huu unaofadhiliwa na Shirika la Misaada ya Kimataifa la Marekani (USAID) ni wa miaka minne na unalenga kuisaidia serikali katika mipango ya kuimarisha Lishe bora kwa wanawake wenye umri wa uzazi kuanzia miaka 15 hadi 49, kupunguza udumavu kwa asilimia 15 kwa watoto walio chini ya miaka mitano ifikapo mwaka 2022, na kuwaandaa wasichana 330,000 wa umri wa kubalehe.

Kwa sasa Mradi wa Lishe Endelevu katika Mkoa wa Morogoro unaendesha shughuli zake katika Halmashauri za Ifakara, Ulanga, Kilosa, Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro na Malinyi, lengo ni kutoa misaada ya uwezeshaji huo kwa Halmashauri zote tisa za Mkoa huo.

MWISHO  

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.