• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Wizara ya Maji kutatua changamoto ya maji Morogoro

Posted on: July 2nd, 2025

Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Mhandisi Mwajuma Waziri amesema, Wizara hiyo imedhamiria kutatua changamoto ya muda mrefu ya uhaba wa maji katika Manispaa ya Morogoro, kazi ambayo amesema itafanyika kwa ushirikiano na viongozi wa Mkoa huo na taasisi za maji, ili kuwapatia maji safi na salama wananchi wa Halmashauri hiyo pamoja na kushughulikia tatizo kubwa la upotevu wa maji.

Katibu Mkuu amebainisha hayo Julai 2, 2025, alipotembelea visima vya maji vilivyochimbwa katika eneo la Kayenzi, Kata ya Mafisa Manispaa ya Morogoro kujionea utekelezaji wa miradi ya maji ambapo pia alikutana na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima pamoja na wataalamu wengine wa maji kujadili suala la upatikanaji wa maji katika Manispaa hiyo.

Mhandisi Mwajuma amesema, Mkoa huo una vyanzo vya maji vingi, hivyo Wizara imejipanga kwa dhati kushirikiana na Mkoa kuhakikisha maji yaliyopo ardhini yanatumika ipasavyo kupitia uchimbaji wa visima ili kutekeleza agizo la Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kuhakikisha wananchi wa Morogoro wanapata maji safi na salama.

“Sisi kama Wizara ya Maji tutatekeleza maelekezo haya na wananchi wa Mkoa wa Morogoro waweze kupata huduma ya maji"  amesema. Mhandisi Mwajuma Waziri.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Mhe. Adam Kighoma Malima, amesema kama uongozi wa Mkoa wamejizatiti kuhakikisha wananchi wa Manispaa ya Morogoro wanapata huduma ya maji huku akiweka wazi kuwa walianza na kazi ya kuunda kamati ya kutafuta vyanzo mbadala vya maji, hatua iliyowezesha kupatikana kwa maeneo ya kuchimba visima kama Mafisa na Tungi.


Naye Mwenyekiti wa Mtaa wa Kayenzi, Bw. Mohamed Said ameishukuru Serikali ya Mkoa kwa kubuni njia za kutatua changamoto ya maji waliyokuwa wanaipata wananchi lakini zaidi amemshukuru Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwaletea viongozi wanaojali wananchi na kushughulikia changamoto zao kwa vitendo.



MWISHO.


Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • Wizara ya Maji kutatua changamoto ya maji Morogoro

    July 02, 2025
  • RAS MOROGORO AFUNGA MAFUNZO YA PEPMIS, ATAKA UWAJIBIKAJI NA UAMINIFU

    June 28, 2025
  • RC MALIMA AMUUMA SIKIO DC MVOMERO, KUTUMIA BUSARA ZAIDI.

    June 27, 2025
  • RC MALIMA AENDELEA NA MAONO YA KUKUZA KILIMO MKOANI MOROGORO.

    June 27, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.