• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RAS AWAKINGIA KIFUA TARURA.

Posted on: December 3rd, 2020

Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Mhandisi Emmanuel Kalobelo ametoa Ombi kwa niaba ya TARURA Mkoa wa Morogoro kuongezewa fedha kwa ajili ya Taasisi hiyo Mkoani humo kwa bajeti ya mwaka wa fedha  2020/2021.

Mhandisi Kalobelo amewasilisha ombi hilo Disemba 3 mwaka huu  mbele ya wajumbe wa Bodi ya Mfuko wa Barabara hapa nchini (Road Board Fund) walipofika Ofisini kwake kujitambulisha kuwa wapo Mkoani humo kwa ziara ya siku moja ya kutembelea taasisi za TARURA na TANROAD.

Amesema, Mkoa wa Morogoro una changamoto nyingi za barabara hususan za vijijini kwa sababu ya  ya mkoa kuwa na Milima na Mabonde kunapelekea uwepo wa madaraja na makaravati mengi, kati ya hayo mengi huharibika kipindi cha masika hivyo, amewaomba wajumbe kupokea maombi ya TARURA Mkoa wa Morogoro ya kuongezewa bajeti mara watakapowasilisha maombi yao kwao kwa bajeti ya mwaka wa fedha 2020/2021.

“Naomba niwasilishe rasmi pale ambapo wataomba kuongeza ongeza keki ya uhitaji wa fedha, naomba muwafikirie. Kwa sababu hawa sasa ndio wanaohudumia barabara sio za mijini peke yake lakini hata zinazokwenda kwenye uzalishaji” amesema Mhandisi Kalobelo.

Aidha, Katibu Tawala huyo wa Mkoa ameipongeza Serikali kwa kuanzisha chombo cha kushughulikia barabara, yaani TARURA. Amesema huo ni utaratibu mzuri na ana imani kuwa kwa kuanzishwa kwa taasisi hiyo kutakuwa na mafanikio mazuri zaidi katika sekta ya miundombinu.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Barabara Joseph Haule amewataka Mameneja wa TARURA hapa nchini kuwa na utamaduni wa kuweka kwenye bajeti kazi zote zinazotakiwa kufanyika ndani ya kipindi husika zikitanguliwa na kazi ambazo ni vipaumbele vyao, badala ya Mameneja hao kuomba fedha kwa mtindo wa dharura hali inayopelekea kuwa ni vigumu kutoa fedha hizo kwa vile haziko kwenye bajeti zao.

Maelezo hayo ya Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Barabara yalikuja baada ya Meneja wa TARURA Mkoa wa Morogoro Mhandisi Benjamin Maziku na Mhandisi wa Barabara na Meneja wa TARURA wa Halamshauri ya Manispaa ya Morogoro Mhandisi Macknon Nkwera kuomba kuongezewa fedha za Dharura kutokana na miundombinu mingi kuharibika hususan wakati wa Masika.

Wajumbe wa Bodi ya Mfuko wa Barabara wapo Mkoani Morogoro kwa ziara ya siku moja kutembelea Taasisi za TARURA na TANROAD Mkoa wa Morogoro ili kuona kazi wanazozifanya, changamoto wanazokumbana nazo na kujifunza shughuli mbalimbali zinazofanyika katika Taasisi hizo mkoani humo.

 

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.