• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC Malima awataka Maafisa Tarafa, watendaji wa Kata kuwajibika.

Posted on: August 15th, 2024

RC Malima awataka Maafisa Tarafa, watendaji wa Kata kuwajibika.


Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amewataka Maafisa Tarafa na Watendaji wa Kata kuwajibika kufanya kazi kwa kujitambua katika maeneo yao ili waweze kuwaletea maendeleo wananchi na Taifa kwa ujumla.

Mhe. Malima ametoa agizo hilo wakati akifungua mafunzo ya kuwajengea uwezo maafisa tarafa na watendaji wa kata wa Mkoa wa Morogoro kata yaliyofanyika katika ukumbi wa mbarak mwinshehe uliyopo halmashauri ya manispaa ya Morogoro.

".. ninachotaka kutoka kwenu ni ubunifu, kujituma, muonekane kuwa mnajua mnachofanya, usimamizi wa miradi.." Amesisistiza Mhe. Malima

Aidha,  amesema kuna umuhimu mkubwa wa maafisa hao kujua majukumu yao vilivyo na kufanya kazi kwa kujituma, kujitoa na kufanya usimamizi mzuri katika miradi ya maendeleo kwa maslahi mapana ya Taifa na sio kwa maslai yao binafsi.

Pia kiongozi huyo amesema moja ya changamoto inayowakabili maafisa hao ni kutokuwa na ubunifu katika utendaji kazi wao hivyo amewataka Maafisa Tarafa na Watendaji wa kata wawe wabunifu ili kuweza kutatua changamoto zinazowakabili katika maeneo wanayosimamia.

Katika hatua nyingine Mhe. Malima amewataka watendaji hao wa Serikali  kujituma na  kusimamia miradi ya maendeleo kwa kuwa ni jukumu lao la kuhakikisha miradi inayotekelezwa inakamilika kwa wakati lakini ikiwa na ubora unaohitajika.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI, Bw. Simoni maganga amesema mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo Maafisa Tarafa na Watemdaji wa Kata ili kuweza kuongeza ufanisi katika utoaji huduma kwa wananchi.

Ameongeza kuwa mafunzo hayo yalianza Juni 6, 2023 katika Mikoa ya Songwe, Njombe, Katavi na Rukwa na kubakiza Mikoa nane ambayo yatafanyika kwa mwaka wa fedha 2024/ 2025.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.