• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Wito watolewa kwa wakulima nchini kukata Bima ya Mazao.

Posted on: December 11th, 2020

Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Ndg. Gerald Kusaya ametoa wito kwa wakulima wote nchini kukata Bima ya mazao ili iwakinge na maafa  mbalimbali na kuwapa uhakika na usalama wa shughuli zao kabla na baada ya kupata maafa yatokanayo na changamoto za kilimo.

Ndg. Kusaya ametoa wito huo Disemba 11, mwaka huu wakati wa hafla ya malipo ya fidia kwa wakulima watano kupitia shirika la bima la Taifa (NIC) waliopata hasara  ya mazao kutokana na majanga mbalimbali iliyofanyika katika Ofisi za Shirika la Bima hiyo iliyopo katika Halmashauri Manispaa ya Morogoro.

Mgeni rasmi (wa pili kulia) Ndg. Kusaya akikabidhi Kitabu cha mwongozo wa Bima ya Mazao kwa Mkulima mmoja aliyehudhuria hafla hiyo, wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Bima ya Mazao Tanzania  (NIC) Dkt. Doriye

Katika hafla hiyo Ndg. Kusaya amewashauri wakulima katika Mikoa yote hapa nchini kutembelea NIC ili kupata huduma ya bima ya kilimo ambayo itawakinga na changamoto zinazosababishwa na mabadiliko ya tabia nchi ikiwemo mlipuko wa magonjwa wa mimea, visumbufu, ukungu, mafuriko na ukame.

Aidha, katika tukio hilo Ndg. Kusaya amekabidhi hundi ya Shilingi Mil. 23,000,000/= kwa wakulima hao watano kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero ikiwa ni fidia ya hasara waliyoipata katika mashamba yao yaliyoathiriwa na mafuriko na visumbufu hali iliyopelekea wakulima hao kupata mavuno pungufu.

Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi inayojihusisha na utoaji wa huduma za kuendeleza biashara (TAPBDS) Nyakainja Manyama (wa pili Kulia) ambaye amehudhuria hapo kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo.

Katika hatua nyingine Ndg. Kusaya ametoa wito kwa Mkurugenzi  Mtendaji wa shirika NIC Kutanua wigo wa kutoa huduma zao ili kuwafikia wakulima wengi zaidi nchini kutokana na fursa iliyotolewa na Mhe. Dkt .John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya kuondoa tozo zisizo za lazima katika bidhaa za Bima ya mazao.

Akizungumzia lengo la kuanzishwa mfuko wa shirika la Bima ya mazao Tanzania, Mkurugenzi Mtendaji wa shirika hilo  Dkt. Elirehema Doriye, amesema ni kuwawezesha wakulima kukabiliana na majanga yanayoisumbua sekta ya kilimo kwa muda mrefu Tanzania.

Mgeni rasmi (wa kwanza kushoto) akiwakabidhi wakulima watano Hundi ya Mil. 23,000,000/= ikiwa ni sehemu ya fidia ya mazao yaliyo haribikia shambani.

Dkt. Doriye ametaja mafanikio amabayo yametokana na kuanzishwa kwa huduma ya Bima hiyo kuwa zaidi ya wakulima 562  wamejiunga katika huduma ya Bima  ya mazao ambapo idadi hiyo inajumuisha wakulima wa Pamba, Mpunga, Mahindi na Pareto.

Dkt. Dorinye ametaja mafanikio mengine ikiwa ni  pamoja na wakulima zaidi ya 10,716 kutoka Mikoa ya Simiyu, Morogoro, Njombe na Iringa wameweza kupata Elimu ya Bima, faida zake na jinsi inavyofanya kazi.

Mkuu wa  Kitengo cha Afisa Mahusiano NIC Karimu  Meshacki akitoa shukrani kwa Katibu Mkuu mara baada ya hutuba yake.

Licha ya mafanikio hayo, Dkt Dorinye ametaja moja ya changamoto wanazokumbana nazo katika kutekeleza majukumu yao ikiwa ni wakulima wengi kutokuwa na imani juu ya huduma ya Bima ya mazao hivyo kufikiria kutopata fidia  ikiwa watapata hasara katika mazao yao.

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi inayojihusisha na utoaji wa huduma za kuendeleza biashara (TAPBDS) Nyakainja Manyama, amesema taasisi yake inasimamia ubunifu unaoongeza hamasa ya wakulima ikiwa ni pamoja na kuweka bidhaa ya mazao ya bima katika mtindo wa vocha inayouzwa shilingi 5,000/=.

 Mgeni rasmi akiwa katika Picha ya pamoja na wanufaika wa fidia ya mazao yaliyoharibikia shambani.

Manyama amesema ili Mkulima aweze kukatia bima shamba la ekari moja  atahitajika kununua vocha kumi zenye thamani ya shilingi 50,000/= huku akipata kinga yenye thamani ya shilingi 500,000/=

“Mtindo huu wa vocha ni ubunifu uliolenga kuwawezesha wakulima kujinunulia bima taratibu kabla ya msimu wa kilimo na pengine unapofika msimu awe amekamilisha kadi  zote kumi” amesema Manyama.

Akizungumza kwa niaba ya wakulima wenzake ambao wamepata fidia ya mazao yao, Mwenyekiti Msaidizi wa Mtandao wa Vikundi vya Wakulima Tanzania (MVIWATA) kanda ya Mvomero Dorica Mlacha, ametoa shukrani kwa shirika la Bima la Taifa kupitia bima ya mazao kwa kuwaaminisha wakulima kuwalipa fidia ya mazao yanayoharibika kutokana na mabadiliko ya tabia nchi.

Baadhi Wafanyakazi wa Shirika la Bima ya mazao waliohudhuria katika hafla hiyo.

Shirika la Bima ya mazao la Taifa (NIC) lina uzoefu wa Miaka 57 katika kutoa  huduma nchini. Lilianzisha Bima ya mazao Agosti  2019 ikiwa ina lengo la kuwawezesha wakulima kukabiliana na majanga yanayoisumbua sekta ya kilimo kwa muda mrefu hapa nchini.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.