• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

AFISA MTENDAJI MJI MDOGO MIKUMI ASIMAMISHWA KAZI

Posted on: February 28th, 2021

Afisa Mtendaji wa Mji mdogo wa Mikumi Wilayani Kilosa Mkoani Morogoro Bw. Omari Jaka amesimamishwa kazi ili kupisha uchunguzi wa tuhuma zinazomkabili za matumizi mabaya ya fedha na madaraka.

Omari Jaka amesimamishwa kazi Februari 18 mwaka huu na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare siku ya pili ya ziara yake Wilayani Kilosa wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya bustanini vilivyoka katikati ya mji huo.

Kaimu DC Gairo Albinus Mgonya ambaye alimwakilisha DC Gairo akiwasilisha taarifa za ujenzi wa vyumba vya madarasa katika Mji Mdogo Mikumi.

Katika Mkutano huo Bw. Jaka amenyooshewa vidole na wananchi mara kadhaa kumtuhumu kutumia vibaya fedha mbalimbali zinazochangwa na wananchi kwa ajili ya maendeleo ya mji huo ikiwa ni pamoja na kujenga kituo cha mabasi.

Aidha, Mtendaji Jaka anatuhumiwa kuwa na matumizi yasiyoeleweka ya fedha zinazopatikana kwenye mikataba ya minara ya simu makampuni zaidi ya manne ambapo kwa mwaka zinakusanywa takribani shilingi milioni saba ingawa matumizi yake yamekuwa hayako wazi.

Mbunge wa Jimbo la Mikumi Denis Londo akitoa pongezi kwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare kwa namna ambavyo anawasaidia wananchi wa Jimbo lake katika kutatua kero mbalimbali za wananchi.

Kutokan na tuhuma hizo Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare amechuua hatua ya kumsimamisha kazi Bw. Jaka kupisha uchunguzi wa tuhuma zinazomkabili baada ya kutolewa na wananchi wa mji huo.

“nasema tena TEO atasimamishwa, Mkurgenzi ataunda tume itapitia hayo na ripoti hiyo nitapewa na mimi nijiridhishe, mambo hayaende kabisa kwenye mji huu” alisisitiza Loata Sanare.

Kwa upande wake Omari Jaka amesema kwa mjibu wa uendeshaji wa Serikali za mitaa Mamlaka ya miji midogo haina kasma, kwa hiyo haiwezi kutoa fedha benki na kutumia bila kuhamishiwa kwenye mfuko mkuu wa halmashauri na Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri kuidhinisha matumizi yake.

Kwa msingi huo, kazi ya miji midogo ni kukusanya fedha pekee na si kutumia, na  endapo wanataka kutumia lazima waandike madokezo ya kuomba fedha za kutumia kwa Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri.

Baadhi ya wananchi kutoka Mji Mdogo Mikumi waliohudhuria katika mkutano wa hadhara kumsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata sanare ameagiza viongozi wote wa Serikali ndani ya Mkoa huo kuendelea kusikiliza kero za wananchi kwa kutekeleza sheria, taratibu na kanuni zote ikiwa ni pamoja na kufanya mikutano ya mara kwa mara ili kupunguza maswali kwa wananchi.

Mwisho

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.