• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Baraza la Madiwani latakiwa kufuatilia asilimia kumi za mapato ya ndani.

Posted on: December 15th, 2020

Baraza jipya la Madiwani katika Halmashauri  ya Wilaya ya Ulanga Mkoani Morogoro limetakiwa kufuatilia Shilingi Mil. 137 zinazotokana na asilimia kumi za mapato ya ndani ya Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu ili pesa hizo zirudi kuwafaidisha wananchi wengine.

Hayo yamebainishwa Disemba 15 Mwaka huu na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare wakati wa kikao cha  kwanza cha baraza la Madiwani kilichofanyika katika Halmashauri hiyo.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare akihutubia Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga Mkoani Morogoro.

Akiwa Mgeni rasmi katika kikao hicho, Loata amesema Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga imeshindwa kujibu hoja ya Mdhibiti na Mkaguzi wa pesa za Serikali (CAG) juu ya upotevu wa shilingi Mil.137 zinazotokana na  asilimia kumi ya Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu.

Aidha, Loata amewataka Madiwani kutojihusisha na ukusanyaji wa pesa za mapato ya ndani bali wasimamie katika upatikanaji wa mapato hayo ili kuleta miradi ya maendeleo kwa wananchi wao.

Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga wakiwa makini kumsikiliza Mkuu wa Mkoa akiwa anawahutubia.

Kwa upande wake Mwenyekiti Mteule wa baraza la Madiwani  wa Halmashauri ya Wilaya ya  Ulanga Edison William amesema atalifanyia  uchunguzi agizo la Mkuu wa Mkoa huyo ili kubaini watendaji ambao wametumia vibaya pesa hizo na kuhakikisha  zinarejeshwa ili ziweze kuwanufaisha walengwa

Akizungumzia suala la uwepo wa vikundi hewa ambavyo inasemekana kunufaika na asilimia kumi za mapato ya ndani, William amesema atahakikisha anaunda baraza maalumu la kusimamia vikundi hivyo lengo likiwa ni kuwafikia walengwa wa fedha hizo kwa mujibu wa sheria inavyowataka.

 Mwenyekiti Mteule wa baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga  Edison William akitoa nasaha kwa Madiwani wenzake

Naye, Diwani wa Kata ya Lupingu Amina seif, amesema katika kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) atahakikisha anawasimamia vyema asilimia hizo kumi za Wanawake, Vijana na watu wenye ulemavu hivyo kuwataka kutokuwa na hofu

Hata hivyo, Kaimu Afisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri hiyo Fabian Likoko amesema mpaka sasa wameweza kupunguza deni kutoka Mil. 137 nadi Mil. 66 ambapo jitihada zinaendelea kufanyika kwa vikundi ambavyo havijarejesha ili viweze kurejesha pesa hizo kwa wakati.


Maafisa Kutoka Sekretarieti ya Mkoa, Idara ya Serikali za Mitaa, walishiriki Kikao cha Madiwani katika kuhakikisha kuwa uchaguzi wa Viongozi wa Baraza hilo unafuata Sheria,Taratibu na kanuni. kutoka Kulia ni Christer Njovu na Marcelin Ndimbwa

Pia, Likoko amesema Idadi ya Vikundi ambavyo vimesajiriwa tangu mwaka 2011 ni 1,027, ambapo mwaka wa fedha 2018/2019 na 2020/20021 jumla ya vikundi ambavyo vimekopeshwa ni 169 na kupewa jumla ya shshilingi Mill 388.


MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.