• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

DKT. GWAJIMA AWATWISHA MZIGO MAAFISA MAENDELEO YA JAMII.

Posted on: October 16th, 2022

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wananwake na Makundi Maalum Dkt. Dorothy Gwajima amewataka Maafisa Maendeleo ya Jamii hapa Nchini kutimiza wajibu wao ikiwa ni pamoja na kuhakikisha wanawaezesha wanawake kiuchumi hasa walioko Kijijini ili kujikwamaua kiuchumi.

Waziri Gwajima ameyasema hayo Oktoba 15 mwaka huu wakati wa maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya mwanamke anayeishi kijijini ambayo kitaifa yamefanyika Wilayani Kilombero Mkoani Morogoro katika Kata ya Mang’ula.

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wananwake na Makundi Maalum Dkt. Dorothy Gwajima akitembelea mabanda ya maonesho ya bidhaa za mikono zinazozalishwa na wanawake.

Dkt. Gwajima amefafanua kuwa endapo mwanamke atajikwamua kiuchumi kupitia majukwaa ya uwezeshaji kiuchumi, atajiamini na kugombea nyadhifa mbalimbali za uongozi hivyo kuondokana na changamoto zinazomkabili ikiwa ni pamoja na ukatili wa kijinsia, mila kandamizi na ndoa za utotoni ambavyo vyote kwa kiasi kikubwa vichagizwa na na umaskini.

Dkt. Dorothy Gwajima, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wananwake na Makundi Maalum akisalimiana na viongozi mbalimbali baada ya kuwasili katika Maadhimisho ya siku ya Mwanamke anayeishi Kijijini.

Kwa muktadha huo, Dkt. Dorothy Gwajima amewataka Maafisa Maendeleo ya Jamii kote nchini kuimarisha majukwaa hayo kuanzia ngazi ya Vijiji, Kata, Wilaya na Mkoa ili kila mwananke apate fursa ya kujikwamua kiuchumi

“Majukwaa ya uwezeshaji kiuchumi yaanzie Mtaa, Kata, Halmashauri Mkoa ndio yaje Taifa,Taifa liko jukwaa moja tu lakini vijijini na kwenye mitaa yako Mengi tunataka yasimame imara” ameagiza Dkt. Dorothy Gwajima.

Amesema, yeye mwenyewe atafanya ziara kila ngazi kwa lengo la kutaka kuyaona majukwaa hayo na kuhakikisha yako hai lengo ni kuendelea kupunguza umaskini wa chakula kama takwimu zinavyoonesha kuwa umaskini unashuka kutoka 10% 2015 hadi 8% mwaka 2020.


Aidha amesema kwa mujibu wa takwimu za Ofisi ya Takwimu ya Taifa na kwa mujibu wa REPOA umaskini unakadiriwa kushuka 0.21% kwa kila mwaka hali inayoonesha kuwa Serikali ya Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaendelea kuwekeza katika kupunguza hali ya Umaskini hapa nchini.

Dkt. Dorothy Gwajima, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wananwake na Makundi Maalum akizungumza na wananchi katika Maadhimisho ya Siku ya Mwanamke anayeishi Kijijini.

Maadhimisho hayo ambayo yalikuwa na kaulimbiu “Mwanamke Aishiye Kijijini ni Mzalishaji Mkuu wa Chakula; Tumuwezeshe” yana lengo la kutambua mchango wa mwanamke anayeishi kijijini katika kilimo, uhakika wa chakula, kuinua uchumi wa Kaya na Taifa kwa ujumla.

 

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • Vyama vya Ushirika Vyatakiwa Kutumia TEHAMA

    May 14, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.