• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Halmashauri ya Mji Ifakara yatakiwa kujibu hoja za CAG

Posted on: December 16th, 2020

Halmashauri ya Mji Ifakara Mkoani Morogoro imetakiwa kujibu hoja za Mkaguzi na Mdhibiti wa hesabu za Serikari (CAG) kwa mwaka 2018/2019 juu ya fedha zilizotolewa na Serikali kwa ajili ya ujenzi wa jengo la Halmashauri kutokamilika bila sababu.

Hayo yamebainishwa Disemba 14 Mwaka huu na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare wakati wa Kikao cha kwanza cha baraza la Madiwani kilichofanyika katika Halmashauri hiyo.

Akifafanua zaidi, Sanare amesema katika hoja 26 zilizoibuliwa na CAG, Halmashauri ya Mji wa Ifakara imejibu hoja 22 huku hoja 4 zikishindikana kupatiwa majibu, ambapo moja kati ya hoja hizo inahusu zaidi ya Shilingi Bil. 7 zilizotolewa na Serikali  kushindwa  kukamilisha ujenzi wa jengo la Halmashauri hiyo hadi sasa bila sababu ya msingi.

Aidha, Loata Sanare ametaja hoja nyingine  ambayo bado haijajibiwa ni pamoja na zaidi ya Shilingi Mil. 200 kulipwa nje ya mfumo wa ulipaji mapato ya Serikali badala yake fedha hizo zililipwa kinyume na maelekezo yaliyotolewa na Serikali.

Pia, Loata ameongezea hoja nyingine ya CAG ambayo haikupatiwa majibu ni ukusanyaji wa fedhaa kutoka kwa wananchi bila kuingizwa katika mapato ya ndani ya Halmashauri  huku takwimu zikionesha zaidi ya Mil. 200 zilizokusanywa zilitumiwa na watu binafsi kwa maslahi yao.

Kutokana na hoja hizo, Loata Ole Sanare amelitaka baraza jipya la Madiwani la Mji wa Ifakara kufanya kazi kwa kutanguliza maslahi ya wananchi, kuwa na vikao kila baada ya miezi mitatu kujadili hoja mbalimbali na kutekeleza ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ili kuunga mkono jitihada za Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mwenyekiti wa muda wa Baraza la kwanza la Madiwani ambaye pia ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Kilombero Adam Bibagamba akiongoza kikao hicho 

Sambamba na hayo, Loata amelitaka baraza hilo la Madiwani kuhakikisha wanasimamia miradi ya maendeleo inatekelezwa kwa wakati huku akiwasisitiza madiwani hao kulinda fedha zinazotolewa na Serikali katika kutekeleza miradi ya maendeleo iliyopo katika maeneo yao.

Naye, Mbunge wa Jimbo la Ifakara Abubakari Asenga amewasisitiza Madiwani kufanya kazi kwa ushirikiano mkubwa na wananchi, watendaji wa vijiji, watendaji wa Kata, Wakuu wa idara na wataalamu wengine ili kufikia lengo la kumletea maendeleo mwananchi mmoja mmoja.

Kwa upande wake, Katibu Tawala wa Wilaya ya Kilombero ambaye alikuwa mwenyekiti wa muda wa kikao cha Baraza hilo Adam Bibagamba amelitaka baraza la Madiwani hao kufanya kazi kwa mujibu wa miongozo waliyopewa bila kuangalia changamoto ya mtu mmoja mmoja, Chama au migogoro binafsi.

Akizungumza mara baada ya kuthibitishwa kuwa Mwenyekiti wa Baraza la madiwani katika Mji wa Ifakara Kassim Nakapala ametumia fursa hiyo kuwashukuru Madiwani wote kwa kumthibitisha kuwa mwenyekiti wa Halmashauri hiyo amewaomba madiwani wenzake kutekeleza wajibu wao katika kuwatumikia wananchi kulingana na ahadi walizozito wakati wa kampeni.

Maafisa kutoka Sekretarieti ya Mkoa wa Morogoro Crister Njovu (kushoto) na Marcelin Ndimbwa wakijadili jambo wakati wa Kikao hicho

MWISHO.

 

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • RAIS MSTAAFU WA AFRIKA KUSINI AWATAKA WAAFRIKA KUENZI MASHUJAA WAO.

    May 23, 2025
  • MAFUNZO YA AMIS NA TAUSI YATOLEWA MKOANI MOROGORO.

    May 21, 2025
  • MAFUNZO YA AMIS NA TAUSI YATOLEWA MKOANI MOROGORO.

    May 21, 2025
  • Zaidi ya Mil. 125 zachangwa kupitia chakula cha hisani kukarabati Hospitali ya Rufaa Morogoro.

    May 18, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.