• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Morogoro yapongezwa upangaji wamachinga

Posted on: September 21st, 2021

Waziri Ummy apongeza uongozi Morogoro upangaji  “Wamachinga”

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Ummy Mwalimu ameupongeza Uongozi wa Mkoa Morogoro kuwa Mkoa wa kwanza kutekeleza agizo la Mhe. samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania la kuhakikisha wafanyabiashara ndogo ndogo maarufu kama wamachinga wanapangwa na kufanya biashara zao katika maeneo yaliyo rasmi na salama.

Waziri Ummy Mwalimu ametoa pongezi hizo Septemba 21 mwaka huu wakati wa uzinduzi wa mpango wa kuwapanga  wafanyabiashara ndogo ndogo 788 wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kwa kuwapatia vibanda vya kufanyia biashara zao katika eneo la Soko Kuu la Chifu Kingalu lililopo katika Halmashauri hiyo.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela (kushoto) akimpokea Waziri wa Nchi OR - TAMISEMI Mhe. Ummy Mwalimu

Amesema mafanikio ya kutekeleza agizo la Mhe. Samia Suluhu Hassan alilolitoa Juni 15 mwaka huu la kutaka wamachinga kutafutiwa maeneo rasmi ya kufanyia biashara, yanatokana na uongozi Mzuri wa Mkuu wa Mkoa huo Martine Shigela kwa kupenda kulea, kuwaamini na kuwashirikisha viongozi waliochini yake masuala ya kimaendeleo huku akimtaka Mkuu huyo wa Mkoa kuendelea na utamaduni huo.

 “shigela ni Mkuu wa Mkoa anaependa kushirikisha na kuwaamini waliochini yake….. kipekee na mimi nipongeze sana viongozi wa Mkoa wa Morogoro chini ya Jemedali Martine Shigela kwa kuongoza vyema na kusimamia vyema jambo hili” amesema Ummy Mwalimu.

Mhe. Ummy Mwalimu akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya morogoro Albert Msando (wa pili kulia)na baadhi ya viongozi wa Wilaya hiyo.

Aidha, amempongeza Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Albert Msando kwa uthubutu, ubunifu na kujitoa kwake kuhakikisha kwamba maagizo ya Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan yanatekelezwa kwa wakati.

“Hongera sana Mkuu wa Wilaya kwa kuanza vizuri ninaamini Wakuu wa Wilaya wengine watajifunza kutoka kwako, ukipewa nafasi acha alama katika kuwatumikia wananchi hususan wanyonge” aliongeza Waziri Ummy.

Baadhi ya Wajumbe wa Kamati za Ulinzi na Usalama Mkoa na Wilaya wakimpokea Waziri

Waziri Ummy amesema lengo mahususi la kutatua kero za wamachinga ni kutaka kujenga uchumi imara unaoakisi hali halisi ya Mtanazania kwa kujenga viwanda vidogo na biashara ndogo ili kukuza pato la Taifa, hii pia ni utekelezaji wa ilani ya Chama Tawala ya mwaka 2020/2025.

Ameongeza kuwa takwimu mbalimbali zinaonesha kuwa wafanya biashara ndogo ndogo wanaajiri watanzania takriban milioni 31 kati ya watanzania takriban milioni 60 waliopo hapa nchini hivyo Wamachinga ni sehemu muhimu ya kuifanya Tanzania isonge mbele kiuchumi.

baadhi ya mitaa ya maeneo ya kufanyia biashara  wamachinga inavyoonekana 

Kwa sababu hiyo, Ummy Mwalimu ameziagiza Halmashauri zote hapa nchini, kutenga maeneo maalumu kwa ajili ya wafanyabiashara ndogo ndogo na kuyaendeleza maeneo hayo kulingana na wakati na idadi ya wamachinga inavyoongezeka katika eneo husika huku akitaka mikoa mingine kujifunza Mkoa wa Morogoro jinsi ulivyotekeleza agizo hilo.

Baadhi ya Wafanyabiashara ndogo ndogo (wamachinga) walioshiriki kwenye uzinduzi huo, kulia ni sehemu ya jengo la Soko Kuu la Chifu Kingalu

Sambamba na agizo hilo amezitaka halmashauri hizo kutatua changamoto za Wamachinga za kutosajiri biashara au huduma wanazotoa ili kuwafikia kiurahisi lakini pia wao kupata fursa mbalimbali zinazotolewa na Serikali huku akiagiza Uongozi wa Mkoa na Halmashauri zake kutoa mikopo isiyo na masharti magumu kwa wamachinga hao ili dhamira ya kulinyanyua kundi hilo iweze kufikiwa.

Mhe. Ummy Mwalimu Waziri na MB

Naye Waziri wa Viwanda na Biashara Prof. Kitila Mkumbo ambaye alishiriki uzinduzi huo pamoja na kuwatambua wamachinga kuwa ni kundi muhimu kwa uchumi wa nchi bado amewataka kuheshimu taratibu wanazokubaliana ili kuendeleza Amani, utulivu na ustawi wa nchi kupitia kazi wanazozifanya katika maeneo yao.

Katika hatua nyingine Prof. Mkumbo amewataka wamachinga kuwa wazalendo kwa kununua bidhaa za viwanda vidogo vilivyoanzishwa hapa nchini na kuwauzia wananchi bidhaa hizo pamoja na wao wenyewe kuanzisha viwanda vidogo au vidogo sana ili kuendelea kukuza uchumi wa nchi.

Waziri wa Viwanda na Biashara Prof. Kitila Mkumbo (kulia) mara baada ya kuwasili Soko Kuu la Chifu Kingalu

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela pamoja na kuwapongeza Viongozi wa Halmashauri ya Manispaa na Wilaya ya Morogoro amewataka wamachinga kuungana na kuwa wamoja huku akiwataka wenye tabia ya kuuza kwa watu wengine maeneo waliyopewa kuacha mara moja tabia hiyo na kwamba atakayebainika kufanya hivyo atachukuliwa hatua kwa mujibu wa makubaliano.

Mkuu wa Mkoa Martine Shigela akimuongoza mgeni wake kukagua vibanda vya wamachinga kabla ya kuzindua. Kushoto ni Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro Mhe. Pascal Kihanga

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa mpango huo wa kuwapanga wamachinga kwenye maeneo rasmi kwa kuwajengea vibanda unatekelezwa kwa awamu awamu, ambapo awamu hii ya kwanza wamachinga wapatao 788 wamejengewa vibanda vya kufanyia biashara zao na awamu zijazo zitaelekezwa sokoni hapo na kwenye masoko mengine yaliyopo ndani ya Halmashauri hiyo.

 

wa tatu kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Morogoro mjini Mhe. Abood Azizi


MWISHO

 

 

 

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.