• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RAS MOROGORO aiomba Serikali Maafisa Ustawi wa Jamii.

Posted on: November 9th, 2020

Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Mhandisi Emmanuel Kalobelo amewasilisha ombi Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto la kuomba kuongezewa Maafisa Ustawi wa Jamii katika Mkoa huo kwa kuwa waliopo hawatoshi ukilinganisha na uhitaji na migogoro iliyopo.

Mhandisi Kalobelo ametoa Ombi hilo Novemba 9 mwaka huu Ofisini kwake mbele ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii Dkt. John Jingu ambaye yupo Mkoani hapa kikazi.

Akiwa na mgeni wake ofisini, wawili hao walizungumzia umuhimu wa Maafisa wa Ustawi wa Jamii, huku Mhandisi Kalobelo akitoa ombi maalum kwa Dkt. Jingu kuona namna ya kuongeza Maafisa Ustawi wa Jamii  Mkoani humo ili kutatua changamoto na kero ambazo pamoja na kuzipunguza bado zipo kwa kiwango kikubwa.Mhandisi Kalobelo amesema kuna upungufu wa Maafisa Ustawi wa Jamii hali inayopelekea mrundikano wa wananchi katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa,  amemuomba Katibu Mkuu huyo kumuongezea Maafisa Ustawi wa Jamii ili wasaidie katika kupunguza mrundikano wa kero Mkoani humo.

“Ustawi wa Jamii wapo wachache hilo ndilo ombi langu pia katika sekta yako tusaidie, tuombee tupate Maafisa Jamii wa kutosha kwa sababu tunatumia gharama kubwa sana” Alisema Kalobelo.

Kwa upande wake Dkt. John Jingu amekiri kuwepo kwa upungufu wa Maafisa Ustawi wa Jamii ambapo amesema kwa sasa wamewasilisha taarifa TAMISEMI juu ya hitaji hilo na  wameandaa muundo wa kuwaajiri Maafisa Ustawi wa Jamii katika Kada mbalimbali katika Ofisi za Serikali.

Aidha, Dkt. Jingu amesema Maafisa Ustawi wa Jamii na Maendeleo ya Jamii ni Kada muhimu ambazo huwa za kwanza kupelekwa kwenye maeneo ya majanga ili kuiweka jamii husika katika hali ya utulivu kwa kuwa Kada hizo ndizo zinajua namna ya kufanya kazi na jamii iliyopatwa na majanga.

Akihakikisha dhana hiyo Dkt. Jingu amesema mafisa hao ndio waliosaidia sana wakati wa tukio la Moto lililotokea Mkoani Morogoro Agosti 10, 2019 na kusababisabisha zaidi ya watu 115 kupoteza maisha.

Hata hivyo, Dkt. Jingu ameonekana kupokea Ombi la Katibu Tawala wa Mkoa huo, huku akiwahakikishia wananchi kuwa kada hiyo imezungumzwa sana kwenye ilani ya sasa ya chama kilichoko madarakani hivyo wanaendelea kuiboresha kulingana na maelekezo ya Ilani hiyo ili maafisa hao waweze kutekeleza wajibu wao ipasavyo.

Kwa mujibu wa Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Mororgoro Bi. Jesca Kagunila amesema Mkoa wa morogoro una jumla ya Maafisa Ustawi wa Jamii 34 tu sawa na asilimia 10.4.

Aidha Mkoa huo una upungufu wa Maafisa Ustawi wa Jamii zaidi ya 282 jambo ambalo amesema linakwamisha ufanisi wa kutekeleza majukumu ya kada hiyo ndani ya Mkoa wa Morogoro.

MWISHO.


Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.