• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC Malima alipongeza Jeshi la Polisi.

Posted on: November 28th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amelipongeza jeshi la polisi hapa nchini kwa kazi nzuri inayoendelea kufanywa na jeshi hilo, kwa weledi mkubwa na kasi inayotakiwa katika kuwalinda watanzania na mali zao.


Mkuu wa Mkoa mhe, Adam Malima amesema kwa sehemu kubwa jeshi hilo limekuwa likitupiwa lawama nyinngi kuhusu utendaji wake wa kazi kubadilika na kuwa na mtazamo chanya kwa jeshi hilo kwa kuwa linakabiliana na uhalifu kila kukicha hivyo watanzania hawana budi kulishukuru.


Mkuu wa Mkoa huyo amebainisha hayo Novemba 27, mwaka huu kutokana na kukamatwa kwa  Seleman Mabura Sita mtuhumiwa wa mauaji ya Mama na Mtoto yaliyotokea kata ya Milola Wilaya ya Ulanga Mkoani humo Novemba 24, mwaka huu kwa kuwakata vichwa na kutokomea navyo kusikojulikana.


Hata hivyo, jeshi hilo la polisi chini ya Uongozi wa  Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Camilius Wambura mtuhumiwa wa mauaji amekamatwa ndani ya saa 36 na kwa sasa anashikiliwa na jeshi hilo kwa mahojiano zaidi.


Kutokana na kazi hiyo kubwa na nzuri iliyofanwa na jeshi hilo kwa kumkamata mtuhumiwa aliyefanya tukio hilo ambalo limeleta simanzi kwa jamii, Mkuu wa Mkoa huyo amempongeza IGP. Camilius Wambura,  Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro  ACP Alex Mukama na Watendaji wake pamoja na vyombo vingine vya Ulinzi na Usalama kwakuendelea kutekeleza vema majukumu yao.


Aidha, Mhe. Malima amesema kuwa ukatili kwa jamii ni jambo lisilokubalika na kuwataka wananchi kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama kutoa taarifa mapema kwa vyombo hivyo ili kufanya kazi haraka na kwa weledi.


"...sisi hatutokaa tukayachekea kabisa matukio haya na niwahakikishie wanamorogoro waendelee kushirikiana na kuwa na Imani na vyombo vya ulinzi na usalama vifanye kazi yao lakini hata serikali ya awamu ya sita haikubaliani na matukio ya ukatili kama huu..."


Katika hatua nyingine, Mkuu huyo amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa vifaa muhimu vyenye teknolojia ya kisasa sambamba na magari, vitendea kazi ndivyo vilivyosaidia jeshi hilo la polisi kufanya kazi zao haraka na kwa ufanisi.


Pia, Mhe. Adam Malima ametoa salamu za pole kwa ndugu, jamaa na marafiki kwa kuondokewa na wapendwa wao na kuwataka kuwa wavumilivu na wztulivu wakati jeshi hilo linaendelea kukamilisha taratibu nyingine za kisheria  ili haki iweze kutendeka.


Mwisho

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.