• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

ZAIDI YA TRILIONI 3 ZATEKELEZA MIRADI YA MAENDELEO MKOANI MOROGORO

Posted on: June 16th, 2025



Mkoa wa Morogoro ulipokea shilingi zaidi ya trilioni tatu (3) kwa kipindi cha miaka mitano chini ya uongozi wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), fedha ambazo zilielekezwa kwenye utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma malima wakati akiwasilisha taarifa hiyo mbele ya kikao cha wajumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Mkoa wa Morogoro kilichofanyika katika Ukumbi wa Magadu, Manispaa ya Morogoro.

"...Serikali inaendelea kutekeleza ilani, hadi sasa juni 2025 Mkoa wa Morogoro kwa kutekeleza ibara 14 kwa vyanzo vya fedha 21 jumla ya fedha zilizotambulika kutumika ni zaidi ya Bil.3 ," amesema Mhe. Adam Kighoma Malima.

Mhe. Malima amesema kwa kipindi cha miaka mitano, utekelezaji wa Ilani CCM umeigusa sekta mbalimbali zenye thamani ya shilingi Bil. 618 zikiwemo Utawala, Elimu, Afya, Kilimo, Mifugo na Uvuvi, uwezeshaji wa kiuchumi, Maendeleo ya ushirika, maliasili na utalii, ardhi, ustawi wa jamii, usafi na mazingira, masoko, michezo na utamaduni pamoja na usafirishaji.

Sambamba na taarifa hiyo, amesema taasisi za umma kwa kipindi cha miaka mitano katika sekta ya miundombinu ya barabara na madaraja zimepokea zaidi ya shilingi bilioni 948.7, sekta ya maji bilioni 422.4, na sekta ya nishati zaidi shilingi trilioni 1.2.

Mhe. Malima amefafanua kuwa sekta ya afya imetumia zaidi ya shilingi bilioni 64.6 kujenga vituo vya afya 33, zahanati 82 na hospitali za wilaya 7. Aidha, fedha hizo zimetumika kununua vifaa tiba pamoja na kuongeza watumishi wa kada ya afya.

Sekta ya elimu imetumia zaidi ya shilingi bilioni 261 kwa ajili ya ujenzi wa shule za msingi na sekondari 165, vyuo vya ufundi stadi, vyuo vya kati na vyuo vikuu, pamoja na utekelezaji wa mpango wa elimu bila malipo kwa ngazi ya msingi na sekondari.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Morogoro Mhandisi Joseph Masunga ameishukuru Serikali ya CCM chini ya Mwenyekiti wake Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Kwa kuendelea kutekeleza ilani ya chama hicho kwa kutoa fedha nyingi kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo ambayo imewagusa moja kwa moja wananchi na kutatua kero zao.

Kikao hicho kimetoka na maazimio kumi ambayo yalisomwa na Katibu wa CCM Mkoa wa Morogoro, Ndg. Nuru Ngereja. Baadhi ya maazimio hayo ni pamoja na kuiagiza Serikali ya Mkoa huo kuratibu mashamba yote yanayomilikiwa na watu kwa muda mrefu lakini hayatumiki na kuandaa mpango mkakati wa kurejesha ardhi hiyo kwa wananchi.

Mashamba hayo ni pamoja na shamba la mwekezaji wa zao la karangamiti lenye ukubwa wa zaidi ya hekta 40,000 lililoko Wilaya ya Ulanga, pamoja na mashamba mengine yaliyoko Wilaya ya Kilosa na Mvomero.

Mazao mbadala na ya kimkakati kama vile tumbaku, michikichi, kakao, viazi mviringo, parachichi na mazao ya viungo kama karafuu, yamepewa msisitizo kulimwa mkoani humo kulingana na maeneo yaliyopo na hali ya hewa ya eneo husika.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • ZAIDI YA TRILIONI 3 ZATEKELEZA MIRADI YA MAENDELEO MKOANI MOROGORO

    June 16, 2025
  • UPUNGUFU WATUMISHI WAIBUKA HOJA ZA CAG MLIMBA.

    June 11, 2025
  • UPUNGUFU WA TUMISHI WAIBUKA HOJA ZA CAG MLIMBA.

    June 11, 2025
  • HOJA ZA MANUNUZI ZASABABISHA RC KUTOA MAAGIZO MAZITO IFAKARA.

    June 09, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.