• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Serikali Mkoani Morogoro yatoa wito kwa wadau kuhusu UKIMWI

Posted on: December 1st, 2020

Serikali Mkoani Morogoro imetoa wito kwa Mashirika mbalimbali yasiyo ya Kiserikali, kwa ajili ya kutoa Elimu inayolenga kupambana na maambukizi ya Virusi vya Ukimwi ili (VVU) ili kupunguza au kutokomeza kabisa ugonjwa wa UKIMWI.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mkoani Morogoro Mhe. Albinus Mugonya Disemba Mosi mwaka huu kwenye maadhimisho ya siku ya UKIMWI Duniani yaliyofanyika eneo la Mafiga katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Mugonya ambaye kwenye maadhimisho hayo alimwakilisha Mkuu wa Mkoa huo Loata Ole Sanare amesema, utoaji wa Elimu kuhusu namna ya kujikinga na maambukizi ya UKIMWI utasaidia jamii kujikinga vema na maambukizi kwani bado watanzania wengi wanaendelea kupoteza maisha utokana na kukosa elimu hiyo.

Kwa sababu hiyo Albinus Mgonya ametoa wito kwa mashirika yasiyo ya kiserikali, Makampuni, Taasisi za Kidini, vyama vya kiraia, mtu mmoja mmoja na wadau wengine kushirikiana na Serikali kutokomeza gonjwa hilo hapa nchini.

Mugonya amesema Mkoa wa Morogoro kushirikiana na Wadau unaendelea na jitihada mbali mbali za kupambana na Ukimwi ikiwa ni pamoja na kutoa kinga, tiba, mafunzo na kuweka mazingira wezeshi katika kutekeleza hatua za mapambano dhidi ya ugonjwa huo.

Katika jitihada hizo Mugonya amebainisha kuwa Mkoa wa Morogoro una vituo vya kutolea Afya 440 ambapo kati hivyo, vituo vinavyotoa huduma za tiba na matunzo kwa wanaoishi na VVU ni vituo 90 ambavyo vimeongezwa kutoka vituo 66 vilivyokuwepo mwaka 2019.

Pia ameongeza kuwa katika jitihada za kuzuia maabukizi ya VVU kutoka kwa Mama kwenda kwa Mtoto Mkoa wa Morogoro una Vituo hivyo 350 zikiwa ni juhudi za Mkoa katika kupambana na ugonjwa huo.

Aidha, ametoa maelekezo kwa kila Halmashauri katika Mkoa wa Morogoro kuunda kamati za kudhibiti UKIMWI hususan katika ngazi ya kata na katika ngazi ya Vijiji ambazo zitakuwa na majukumu ya kufanya utafiti wa hali ya maambukizi ya VVU katika maeneo husika, lakini pia kutambua vichocheo vya maambukizi na kuweka mikakati ya kukabiliana nayo.

Kwa upande wake Kaimu Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya mipango na uratibu Anza-Amen Ndossa amewataka wakazi wa Morogoro kuvunja ukimya katika familia zao na kuwataka wazazi wawaelimishaje juu ya ugonjwa huo kutokana na ugonjwa huo kutokuwa na tiba.

“Baba vunja ukimya ongea na mtoto wako wa kike, ongea na mtoto wako wa kiume. Mama vunja ukimya ongea na mtoto wako wa kike, ongea na mtoto wako wa kiume. Baba ongea na Mke wako, Mama ongea na Mme wako. Ukimwi upo, Ukimwi unauwa” alisisitiza Ndossa.

Akisoma hutuba Mbele ya Mgeni rasmi Kaimu Mratibu wa Ukimwi Mkoa wa Morogoro Bi. Tumaini Wapalila, amesema uwepo wa Madangulo, Kumbi za Starehe zinazofanya kazi usiku kucha, Ubakaji, ndoa  za utotoni, watoto wa mitaani na mimba za utotoni ni moja ya vyanzo vya maambukizi ya VVU na kuiomba serikali iwasasaidie kudhibiti mambo hayo.

Naye Mratibu wa Kudhibiti Ukimwi Mkoa wa Dr. Neema Mtaubo amesema kwa Mwaka 2020 Wananchi waliojitokeza kupima Virusi vya Ukimwi ni 153,367, waliogundulika wameathirika ni 11,809 ambapo Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro inaongoza kwa maambukizi hayo ikifuatiwa na Kilosa.

Sambamba na hayo, Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Albinus Mugonya ametumia fursa ya maadhimisho hayo kukabidhi Pikipiki 37 zenye thamani ya Tsh. 88,000,000 kwa Vikundi viwili vya Bodaboda vya Bomsate na Tunaweza kutoka katika  Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro pesa ambazo zimetokana na  asilimia 10 za mapato ya ndani ya Halmashauri hiyo.

Siku ya UKIMWI duniani ambayo huadhimishwa Disemba Mosi kila mwaka hulenga jamii kujitathmini katika maambukizi ya Virusi Vya Ukimwi, ambapo mwaka huu kauli mbiu ilikuwa MSHIKAMANO KITAIFA, TUWAJIBIKE PAMOJA. 


MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.