• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

WAJUMBE KAMATI YA MAADILI WAAZIMIA KUKAA KIKAO CHA PAMOJA

Posted on: February 9th, 2021

.Wajumbe wa kamati ya maadili kwa maafisa wa Mahakama ngazi ya Mkoa wameazimia kufanya kikao cha pamoja na wajumbe Kamati kama hiyo ngazi ya Wilaya ili waweze kupitia kwa pamoja mwongozo wa Uendeshaji wa Kamati za Maadili kwa lengo la kuboresha zaidi utendaji wa Kamati hizo.

Hayo yamebainishwa wakati wa kikao cha Kamati ya Maadili kwa maafisa wa Mahakama ngazi ya Mkoa yenye wajumbe saba (7) kilichofanyika leo Februari 9 mwaka huu katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.

Wakiwa katika kikao hicho cha kawaida kwa ajili ya kujadili ajenda mbalimbali ikiwa ni pamoja na malalamiko ambayo yamepokelewa kutoka kwa wananchi kuhusu Utendaji wa mahakama likajitokeza suala la kutakiwa kupitia mwongozo wa Uendeshaji wa Kamati za Maadili.

Hilo limejotokeza kutokana na wajumbe wa Kamati hiyo kuchaguliwa kwa mara ya kwanza kuingia kwenye Kamati hiyo hivyo kulazimika kuutambua vyema mwongozo huo ili iwe rahisi kwao katika kutekeleza majukumu yao.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Mhandisi Emmanuel Kalobelo ambaye pia ndiye alikuwa Katibu wa kikao hicho alikubaliana na hoja hiyo ya wajumbe na kwamba itatengwa siku ambapo wajumbe wa Kamati ya Maadili ngazi ya Mkoa na wale wa ngazi  ya Wilaya kufanya kikao cha pamoja ili kupitishwa kwenye mwongozo huo na mtaalam atakayeandaliwa.

Kwa upande wake Hakimu Mfawidhi Mkazi Mkoa wa Morogoro  ambaye pia ni mjumbe wa kamati hiyo ya Maadili Abeesira Kalegeya amesema wananchi wanatakiwa kupewa Elimu mahususi kuhusu namna ya kuwasilisha malalamiko yao kwa Kamati ya maadili kwa kuwa wengi wanawasilisha malalamiko yao bila kuwa na ushahidi unaojitosheleza.

Akifunga kikao hicho Mkuu wa Mkoa wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare ambaye pia ndiye Mwenyekiti wa kamati ya Maadili ya Mkoa amesema kuwepo kikao baina ya wajumbe Kamati ya Maadili ya Mkoa na Wajumbe wa Kamati ya Maadili ya Wilaya itasaidia kupunguza kero mbalimbali za wananchi katika maeneo yao.

Loata Sanare amebainisha kuwa wananchi wamekuwa wakiandika barua za malalamiko dhidi ya mahakama na kuziwasilisha ofisini kwake bila uthibitisho  hivyo kupitia kikao watakachokaa pamoja watabaini tatizo na kulifanyia kazi.

Aidha, Loata Sanare ameitaka Kamati ya Maadili ngazi ya Mkoa kufanya kazi zake kwa uaminifu, bidii na weledi katika kuwatumikia wananchi.

“Inaonekana wazi kuwa Kamati hii ina jukumu la kuimarisha uadilifu wa watendaji wa Maafisa wa Mahakama ndani ya Mkoa wetu wa Morogoro hivyo tunalazimika kutekeleza majukumu yetu kwa weledi ya hali ya juu katika kutoa huduma kwa wananchi wetu ndani ya Mkoa’’ amesisitiza Sanare

Kamati ya Maadili ngazi ya Mkoa imeundwa kwa mujibu wa sheria ya uendeshaji wa Mahakama, sheria Na. 4 ya mwaka 2011, kifungu cha 50 (a) – (c) na kuwataja wajumbe wake kuwa ni Mkuu wa Mkoa (Mwenyekiti), Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mkoa husika, Katibu Tawala Mkoa, wajumbe wawili walioteuliwa na Mkuu wa Mkoa  na wajumbe wawili walioteuliwa na Jaji Mfawidhi.

 

MWISHO 

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.