• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

WANANCHI WA MSOGEZI ULANGA WAJAWA NA FURAHA KUPELEKEWA UJENZI WA BARABARA

Posted on: June 15th, 2022

Wananchi wa Msogenzi Wilayani Ulanga wajawa na furaha

Wananchi wa Kijiji cha Msogezi Tarafa ya Vigoi Wilaya ya  Ulanga Mkoani Morogoro wamejawa na furaha baada Serikali ya awamu ya sita kuwapelekea mradi wa Barabara ya Makanga hadi Mafingi yenye urefu wa km 10 ambayo hadi kukamilika kwake itagharimu kiasi cha shilingi milioni 489.


 Wananchi wa Msogezi wakiwa katika furaha na kucheza ngoma ya asili

Furaha za wananchi hao zimedhihirika mara baada ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela kuwasili katika kijiji hicho akiendelea na ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo na kusikiliza kero za wananchi ikiwa ni siku ya nne ya ziara yake.

Furaha ya wananchi wa kijiji hicho baada ya ahadi iliyotolewa na Mkuu wa Mkoa huo kuwahakikishia kuwa barabara hiyo ambayo imekuwa changamoto kwao kwa kipindi kirefu kukamilika ifikapo mwezi Oktoba ,mwaka huu ambapo pia kwa niaba yao amemshukuru Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha hizo za kujenga barabara hiyo.

Katika hatua nyingine Martine Shigela amemuagiza Meneja wa TARURA Wilaya ya Ulanga kuhakikisha bajeti ijayo wanatenga fedha za kumalizia barabara hiyo kwa kuwa amesema kipande hicho cha barabara  hata kikikamilika bado kitakuwa hakina umaana sana endapo barabra hiyo haitaungana na barabara nyingine zinazopitika.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela (katikati) akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Ulanga Ngollo Malenya (kulia) pamoja na Mbunge wa Jimbo la Ulanga Mhe.Salim Alaudin Hasham wakiangalia ngoma ya asili iliyokuwa inachezwa na wananchi wa Msogezi kuonesha furaha yao

Ngollo Malenya, Mkuu wa Wilaya ya Ulanga amesema barabara hiyo itakapokamilika itakuza uchumi wa Wilaya hiyo kwa kuwa kutakuwa na mwingiliano kibiashara baina ya wilaya yake na Wilaya jirani za Kilombero na Malinyi.

Naye mbunge wa Jimbo la Ulanga Mhe. Salim Alaudin Hasham amesema ilikuwa ni ahadi yake kuona wananchi wa Msogezi wanapata barabara, hata hivyo amesema lengo kubwa si tu barabara hiyo kufika Majengo bali kufika Iragua hivyo ataendelea kupambana hadi ndoto yake itimie huku akimshukuru Mhe. Rais kwa kuwaongezea bajeti ya barabara wananchi wa Ulanga.

Kwa mujibu wa maelezo ya Meneja wa Wakala wa Barabara  Vijijini na Mijini TARURA Wilaya ya Ulanga, barabara hiyo itakayojengwa kwa kiwango cha changarawe itahusisha vijiji vya Makanga, Mdindo, Msogezi na Iragua huku msogezi  hadi iragua.

Aidha ametaja baadhi ya manufaa ya mradi huo kwa wananchi wa maeneo tajwa kuwa ni pamoja na kuongeza Ukuaji wa uchumi kwa viijiji vinavyopitiwa na barabara hiyo lakini pia itakuwa njia mbadala ya kutoka mahenge mjini kwenda Iragua badala ya ile ya mlima Ndororo.

Barabara hii imeanza kujengwa tangu Januari 20 mwaka huu na ilitakiwa kukamilika Julai 22 mwaka huu, na haikukamilika kwa sababu ya mvua hivyo sasa inatarajiwa kukamilika Mwezi Oktoba mwaka huu ambapo ujenzi wake uko 45%.

Meneja huyo wa TARURA Wilaya ya Ulanga amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuongeza bajeti ya ujenzi wa barabara za Wilaya hiyo kutoka milioni 514 kwa mwaka wa fedha uliopita hadi kufikia shilingi 2.2 Bil. Sawa na ongezeko la asilimia 312.


Mhe. Shigela akiwa katikati ya wananchi wakimshangilia kwa kufanya ziara katika kijiji cha Msogezi

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.