• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

SERIKALI KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA VIJANA KUTATUA CHANGAMOTO ZAO

Posted on: August 12th, 2025



Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imeendelea kutatua changamoto zinazowakabili vijana kwa kuweka mikakati ya kuboresha miongozo ya stadi za maisha ili kuwawezesha vijana kupata stadi za mahusiano, mawasiliano na ujasiriamali.

Hayo yamebainishwa Agosti 12 mwaka huu na Mkurugenzi wa Hifadhi ya Jamii kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Festo Fute, wakati akifungua kongamano la vijana la Chama cha Wafanyakazi wa Taasisi za Elimu ya Juu Tanzania (THTU) lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Hoteli ya Edema uliopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Bw. Fute amesema Serikali imeendelea kufanya mapitio ya Sera ya Maendeleo ya Vijana, kuanzisha mifuko ya mikopo yenye masharti nafuu kwa vijana, pamoja na kuongeza nafasi za ajira kila mwaka kupitia bajeti kuu ya Serikali, ambapo vipaumbele hivyo vinakusudia kutatua changamoto zinazowakabili vijana.

“Serikali itaendelea kushirikiana nanyi katika kutafuta ufumbuzi wa masuala yote mlioeleza kwa kuwa yanagusa malengo ya Taifa kuhusu ajira zenye staha,” amesema Fute.


Kwa upande wake, Mratibu wa Vijana THTU Taifa, Bi. Julieth Mchunguzi, amesema lengo la kongamano hilo ni kuwaleta pamoja vijana kutoka taasisi mbalimbali ili kujadili changamoto na kuweka mikakati ya namna ya kuzitatua changamoto hizo.


Baadhi ya changamoto zinazowakabili vijana wa elimu ya juu ni pamoja na kutopewa nafasi za kiutawala hata wanapokuwa na sifa na kutopatiwa kipaumbele katika utoaji wa nyumba za watumishi.


Changamoto nyingine ni pamoja na pesa za kujikimu kutotosheleza mahitaji ya waajiriwa wapya, kuwepo kwa ajira za mikataba ya muda mfupi hasa katika taasisi za elimu ya juu, kukosa fursa za kujiendeleza kielimu, kunyimwa likizo za masomo, pamoja na ugumu wa kupata mikopo au kuwepo mikopo yenye masharti magumu.


Naye Mwenyekiti wa THTU Taifa, Dkt. Paul Loisulie, amesisitiza umuhimu wa kudumisha uhusiano mzuri baina ya taasisi zinazoshirikiana katika kuhakikisha vijana wanaondokana na changamoto walizonazo jambo ambalo litaleta uhai mzuri katika taasisi hizo na kuboresha maslahi ya vijana wa elimu ya juu.


Kongamano hilo lilikuwa na kaulimbiu iliyosema "Vijana katika Maendeleo: Kuimarisha Uvumbuzi kwa ajili ya Malengo ya Maendeleo Endelevu"


Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • SERIKALI KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA VIJANA KUTATUA CHANGAMOTO ZAO

    August 12, 2025
  • WADAU WA MAONESHO YA NANENANE WAAGIZWA KUTEKELEZA WALIYOJIFUNZA

    July 12, 2025
  • RC CHALAMILA AWATAKA WATANZANIA KUTUMIA MAONESHO YA NANENANE KUPATA ELIMU MPYA.

    August 06, 2025
  • RAS Morogoro awasisitiza watumishi kufanya mazoezi, awataka kutumia mazingira mazuri yaliyopo

    August 04, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.