• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC Malima atoa siku saba kuunda SACCOS

Posted on: August 22nd, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Mhe. Adam Kighoma Malima, ametoa siku saba kwa viongozi wa ushirika Mkoani humo kuhakikisha wanaanzisha ........(SACCOS) kwa ajili ya wafanyabiashara wadogo (machinga), ili kundi hilo liwe rasmi na kuwa na mchango katika maendeleo ya mkoa wa Morogoro na Taifa.

Mhe. Kighoma Malima ametoa agizo hilo Agosti 23, 2025, wakati wa kongamano la wamachinga Mkoa wa Morogoro lililofanyika katika stendi ya zamani ya mabasi madogo ya mjini Manispaa ya Morogoro kongamano lililokuwa kaulimbiu iliyosema: “WAFANYABIASHARA WADOGO WOTE TUJITOKEZE KUSHIRIKI UCHAGUZI MKUU OKTOBA 2025 KWA AMANI NA UTULIVU.”

Kiongozi huyo wa Serikali amesema, kundi hilo la wafanyabiashara wadogo ni muhimu kulidhamini na kulifanya kuwa kundi rasmi la kiuchumi na kijamii, kwa sababu linachangia pato la halmashauri na taifa kwa jumla.

Aidha, amesema kuazishwa kwa SACCOS hiyo kutasaidia kuwekeza fedha zao na hatimaye kuwawezesha kukopa katika taasisi za kifedha kwa urahisi ili kukuza biashara zao, uchumia wao na wa taifa, hivo akatumia fursa hiyo kutoa maagizo kwq viongozi wa Ushirika wa Mkoa wa Morogoro.

“...Nataka ndani ya siku saba suala la SACCOS la wamachinga lifanyiwe haraka. Ndani ya siku hizo niletewe karatasi nisaini...” amesema Mhe. Adam Kighoma Malima.

Aidha, mkuu huyo wa mkoa amewataka viongozi wanaokusanya mapato kutoka kwa wamachinga kutowafungia biashara zao, hatua kama hizo zinaweza kuchukuliwa kwa mhusika endapo hajalipa kodi yake kwa kipindi cha miezi mitatu.

Kwa upande wake Afisa Maendeleo ya Jamii Mkoa wa Morogoro, Bw. Gibson Mwakoba, amebainisha kuwa wanyabiashara hao waliosajiliwa kwenye mfumo ni 9,792, ambapo kati yao wanaume ni 3,799 na wanawake 5,993 na walio lipia vitambulisho ni 3,044 na kati yao, wafanyabiashara 2,627 sawa na asilimia 86.3 wamepatiwa vitambulisho.

Naye Mwenyekiti wa Machinga Mkoa wa Morogoro, Bw. Faustine Francis Almasi, ameishukuru Serikali inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kulijali kundi hilo kwa kutoa mikopo mbalimbali inayowasaidia kuinua biashara zao.


Sambamba na hilo, amebainisha changamoto zinazowakabili wafanyabiashara hao, ikiwemo kufungiwa mabanda yao bila makubaliano huku akikiri kuwa changamoto hiyo imeanza kufanyiwa kazi na Mkuu wa Mkoa.


MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • RC Malima atoa siku saba kuunda SACCOS

    August 22, 2025
  • SERIKALI KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA VIJANA KUTATUA CHANGAMOTO ZAO

    August 12, 2025
  • WADAU WA MAONESHO YA NANENANE WAAGIZWA KUTEKELEZA WALIYOJIFUNZA

    July 12, 2025
  • RC CHALAMILA AWATAKA WATANZANIA KUTUMIA MAONESHO YA NANENANE KUPATA ELIMU MPYA.

    August 06, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.