• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

WADAU WA MAONESHO YA NANENANE WAAGIZWA KUTEKELEZA WALIYOJIFUNZA

Posted on: July 12th, 2025


Wadau mbalimbali wa maonesho ya wakulima, wafugaji na wavuvi maarufu kama Nanenane wamewatakia kutekeleza kwa vitendo ujuzi, maarifa na teknolojia mpya walizopata kwa kipindi chote cha maonesho ya Nanenane ili waweze kuongeza tija na thamani ya mazao yatokanayo na sekta hizo.


Agizo hilo limetolewa leo Agosti 8, 2025 na Balozi Dkt. Batilda Burian Mkuu wa Mkoa wa Tanga ambaye pia alikuwa mgeni rasmi katika hafla ya kufunga Maonesho ya Nanenane Kanda ya Mashariki yaliyofanyika Viwanja vya Mwalimu J.K. Nyerere, vilivyoko katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro Mkoani humo.


Amesema, wananchi wanapaswa kuyatumia kikamilifu maarifa waliyoyapata wakati wa maonesho, hususan yale yanayohusu teknolojia za kisasa katika sekta za kilimo, mifugo na uvuvi, ili waweze kuongeza kipato chao na kukuza uchumi na pato la Taifa.


“Tuhakikishe tunaishi kile tulichojifunza. Tusiruhusu teknolojia hizi zipite bila kuzitumia,” amesema Mhe. Batilda Burian.


Aidha, amewataka viongozi wa Serikali kutoyachukulia maonesho ya Nanenane mzaha, kwani kufanya hivyo ni kunapoteza malengo msingi ya maonesho hayo badala yake wayatilie mkazo ili yawe chachu ya katika kutoa elimu ya kisasa kwa wananchi, ikiwemo mbinu bora za kilimo, ufugaji na uvuvi ili kuongeza tija.


Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Mhe. Adam Kighoma Malima, amesema Kanda ya Mashariki inajipanga kuhakikisha maonesho hayo yanakuwa ya mfano kwa kutekeleza na kusambaza teknolojia zilizowasilishwa katika maeneo mbalimbali ya kanda hiyo ili ziweze kutumika kwa manufaa ya Halmashauri zao.


Aidha, Mhe. Malima amesema katika maonesho hayo kulikuwa na jukwaa la biashara lililojulikana kwa jina la B2B (Business to Business) amesema jukwaa hilo limewakutanisha wataalamu zaidi ya 1,200 wa sekta za kilimo, mifugo na uvuvi pamoja na taasisi mbalimbali, ambao walipata elimu watakayopeleka maeneo yao kwa lengo la kuongeza thamani katika sekta hizo.


Maonesho hayo yaliyokuwa na kaulimbiu "Chagua Viongozi Bora kwa Maendeleo endelevu ya Kilimo, ufugaji na Uvuvi, 2025" ingawa yamehitimishwa leo, bado yataendelea kufanyika kwa siku mbili ili kutoa nafasi kwa wananchi kuendelea kununua bidhaa mbalimbali ndani ya viwanja hivyo.


Mwisho

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • SERIKALI KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA VIJANA KUTATUA CHANGAMOTO ZAO

    August 12, 2025
  • WADAU WA MAONESHO YA NANENANE WAAGIZWA KUTEKELEZA WALIYOJIFUNZA

    July 12, 2025
  • RC CHALAMILA AWATAKA WATANZANIA KUTUMIA MAONESHO YA NANENANE KUPATA ELIMU MPYA.

    August 06, 2025
  • RAS Morogoro awasisitiza watumishi kufanya mazoezi, awataka kutumia mazingira mazuri yaliyopo

    August 04, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.