• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

33 wapewa mafunzo ya usuluhishi wa Migogoro ya Ardhi

Posted on: November 28th, 2020

Jumla ya Wataalamu na watumishi 33 kutoka katika Wilaya ya Kilombero wamehitimu mafunzo ya siku tano yanayolenga kutatua migogoro ya Ardhi ikiwa ni jitihada za Serikali katika kutafuta njia mbadala ya kupunguza kama sio kumaliza kabisa migogoro hiyo Wilayani Kilombero.

Mafunzo hayo yanayoendeshwa na Chuo cha Uongozi wa Mahakama kilichoko Lushoto Mkoani Tanga na kushirikisha viongozi kutoka Serikalini ngazi ya Mkoa, Wilaya, Serikali za Mitaa na Mabaraza ya Ardhi ya Vijiji yalihitimishwa mwishoni mwa wiki hii na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare kwa kutoa vyeti kwa wahitimu wote wa mafunzo hayo katika Ukumbi wa Halmashauri ya Mlimba ulioko katika Mji wa Ifakara.

Kabla ya kugawa vyeti kwa wahitimu hao Mkuu wa Mkoa huyo alisema Mkoa wa Morogoro unakumbwa na changamoto nyingi za ardhi ambapo kupitia mafunzo hayo wahitimu watajengwa uwezo wa kuelewa njia mbalimbali za namna ya kutoa usulihishi kwa kuzingatia  ukweli wa kesi zinazowafikia na kuwataka wote waliopata mafunzo hayo kufanya kazi kwa uadilifu na kutoa maamuzi bila upendeleo kwa pande mbili zilizotofautina.

“Ndani ya Mkoa wetu wa Morogoro tuna tatizo kubwa la migogoro ya ardhi karibia kila Wilaya kote mpaka pale Manispaa, achilia mbali hizi wilaya zingine tuna kazi kubwa ya kuhangaika na migogoro ya ardhi ndani ya maeneo yetu” alisema Loata

“…..kwahiyo mlipoamua kutoa mafunzo kwenye Mabaraza haya ni jambo jema kweli, na hasa ukizingatia kuwa kazi ya mabaraza haya ni ya usuluhishi kujua ukweli na kujaribu kusuruhisha, suluhisha kwa kujua ukweli bila kupendelea” alisisitiza Loata.

Katika hatua nyingine Loata Ole Sanare amemwagiza Katibu Tawala wa Mkoa huo Mhandisi Emmanuel Kalobelo kuomba nafasi za maafisa wawili wa ngazi ya Mkoa kushiriki mafunzo ya usuluhishi wa migogoro ya ardhi yanayoendeshwa na Chuo hicho cha Uongozi wa Mahakama cha Lushoto Mkoani Tanga.

Sambamba na hilo, Mkuu wa Mkoa huyo amewaagiza Wakurugenzi na Wakuu wa Wilaya Mkoani humo kutenga bajeti kwa ajili ya kusaidia mafunzo ya usuluhishi ambayo yatawashirikisha wafanyakazi kutoka ngazi ya Kijiji hadi Mkoa ili kutambua mbinu za kushughulikia migogoro hiyo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya Kilombero  SACP Ismail Twahil amesema kutokana na changamoto nyingi zilizopo katika Wilaya hiyo anaamini kupitia mafunzo waliyoyapata washiriki hao watawasaidia wananchi katika kufikia maamuzi ya sahihi katika kutatua migogoro kwa kuzingatia mafunzo  waliyoyapata.

Naye, Mratibu wa Mafunzo hayo ambaye pia ni Mhadhiri wa Chuo cha Mahakama cha Lushoto Bw. Mlokozi ametoa shukrani kwa uongozi wa Mkoa wa Morogoro, Wilaya wanazotoa mafunzo hayo kwa kuchangia utoaji wa Kumbi kwa ajili ya mafunzo hayo hali ambayo imesaidia pesa ambayo ingetumika kulipia ukumbi kutumika kulipia ushiriki wa mafunzo husika.

Akizungumza kwa niaba ya washiriki wenzake Katibu wa Baraza la Usuluhishi wa Kijiji cha Miwangani Masa Nkuba, amesema amenufaika na elimu ambayo ameipata hali itakayosaidia kufanya kazi kwa ufanisi pale ambapo wadau watawaletea kesi za migogoro ya ardhi.

Hata hivyo, ameahidi kumuomba Mwenyekiti wake wa Kijiji kuitisha Mkutano wa hadhara ili kuifikisha kwa wananchi elimu aliyoipata kupitia mafunzo hayo lengo ni  kupata urahisi wa kufanya kazi hiyo, lakini pia amewataka wanawake watakao pata nafasi hiyo kuitumia vizuri  ili kuelimisha Jamii nzima juu ya namna ya kutatua migogoro katika sehemu zao.


Mafunzo hayo ambayo kwa kiasi kikubwa yanafadhiliwa na Shirika la Chakula na Kilimo Duniani – FAO yanalenga kutoa mafunzo kwa Taasisi za Serikali katika ngazi ya Mkoa, Wilaya, Serikali za Mitaa na Mabaraza ya Ardhi ya Vijiji.

Walengwa wengine ni CSOs zinazohusika na usimamizi wa Maliasili katika ngazi za Vijiji, wasomi katika maeneo ya usimamizi wa rasilimali za asili na kilimo na jamii, makundi ya wakulima, wafugaji, wavuvi, kamati za amani na makundi ya watu walio katika mazingira hatarishi.

Mafunzo hayo ambayo hadi sasa yamekwishafanyika katika Wilaya ya Mvomero na Kilombero, yanaendelea kutolewa katika Wilaya za Malinyi na Ullanga kuanzia Novemba 30, mwaka huu na lengo ni kuhakikisha yanatolewa kwa Wilaya zote za Mkoa wa Morogoro.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.