• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

ADHA YA MAJI YAISHA MANGAE, MHE. MKUCHIKA AISHUKURU HALMASHAURI KWA USIMAMIZI BORA.

Posted on: October 28th, 2024


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Ikuku (kazi Maalum) Captain Mstaafu Mhe. George Mkuchika (MB) ameishukuru na kuipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Mkoani Morogoro kwa usimamizi na ufuatiliaji mzuri wa fedha zinazotolewa na Serikali kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo  ili kutatua changamoto zinazowakabili wananchi.

Mhe. Mkuchika amebainisha hayo Oktoba 27, 2024 wakati akizindua mradi wa maji wa Mangae ikiwa ni siku ya pili ya ziara yake ya kikazi Mkoani Morogoro ya kukagua, kutembelea na kuzindua miradi mbalimbali inayotekelezwa ndani ya Mkoa huo.

Mhe. Mkuchika amesema nia ya Serikali inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni kuendelea kutoa fedha na kutekeleza miradi ya maji hapa nchini ili kumtua mama ndoo kichwani na kuwashukuru watendaji wa Halmashauri hiyo kwa usimamizi bora wa fedha na kuweza kutekeleza miradi kwa kiwango cha juu.

"...Naishukuru Halmashauri kwa kusimamia vizuri matumizi ya fedha hizi hamkuruhusu mchwa kula noti za hapa..." amesema Mhe. George Mkuchika.

Kwa upande wake,  Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amemshukuru Mhe. Rais kwa niaba ya wanamorogoro kwa kuwajali na kuwaletea miradi mbalimbali hususan ya maji ambapo hapo awali kipindi cha kiangazi idadi ya mifugo hupungua kwa sababu ya uhaba wa maji ya kutosha ya kunywesha mifugo.

Pia amesema uwekezaji wa ujenzi wa tenki la maji katika kijiji cha Mangae  utaondoa kero ya  upatikanaji wa maji ambapo amemuomba Mhe. Rais kuendelea kutoa fedha katika Mkoa huo ili kuweza kutokomeza adha ya maji.

Naye, Meneja wa RUWASA wa Wilaya ya Mvomero Mhandisi Mlenge Nasib akisoma taarifa ya mradi huo wa maji wa Kijiji hicho amesema mradi huo umegharimu jumla ya shilingi Milioni 643.7 hadi sasa fedha zilizotumika ni shilingi Milioni 388.8  ambapo mradi huo umefikia asilimia 85% kukamilika ambpo utahudumia wakazi 4049 na kuweza kuondoa changamoto ya upatikanaji wa huduma ya maji katika kijiji cha Mangae.

Nao wakazi wa kijiji hicho akiwemo Bi. Clinsensia Cosmasi amemshukuru Mhe. Rais kwa kuwaletea mradi huo wa maji ambapo hapo awali walikuwa wakichota maji kwenye mito hivyo mradi huo pindi utakapokamilika utaenda kuondoa adha walizokuwa wanakumbana nazo kutokana na kutafuta maji.


Ikiwa ni siku ya pili ya ziara ya Mhe. Mkuchika katika Mkoa wa Morogoro ambapo Leo ametembelea miradi mitano iliyopo Wilayani Mvomero hususan ya Afya, Elimu na miundombinu ya Barabara, ambapo Oktoba 28, 2024 kiongozi huyo ataendelea na ziara katika Wilaya ya Gairo.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.