• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Viongozi wa Serikali Mkoani Morogoro watakiwa kulinda UHAI wa Bonde la Kilombero.

Posted on: September 26th, 2025


Viongozi wa Serikali Mkoani wa Morogoro, wametakiwa kulinda uhai wa Bonde la Mto Kilombero linalochangia asilimia 65 ya maji yote yanayoingia kwenye mradi wa kufua umeme wa Bwawa la Julius Nyerere ili bwawa hilo liwe endelevu.

Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima Septemba 26, 2025 wakati wa kikao cha pamoja cha kujadili athari zinazolikabili bwawa la umeme la Julius Nyerere baada ya kuona kuwa kuna viashiria vya uharibufu wa vyanzo vya maji  hususan mito inayopeleka maji kwenye bwawa hilo.


Akiwa Mwenyekiti wa kikao Mhe. Malima amewataka Wakuu wa Wilaya ambao ni wenye viti wa Kamati za Ulinzi za Wilaya pamoja na Wakurugenzi watendaji wa Halmashauri za Mkoa huo kuhakikisha ajenda ya kujadili uhai wa Bonde la Mto Kilombero inakuwa ajenda ya lazima katika vikao vyao vyote vya kisheria.


Amesema, jukumu la kulinda vyanzo vya maji vinavyohusisha bwawa hilo ni jukumu la kila mmoja, kwa kuwa bwawa hilo linazalisha megawati 2,115 za umeme na kusisitiza kuwa ni lazima kulinda vyanzo vyake vya maji ili viendelee kudumu na kuliwezesha bwawa kutumika sasa na vizazi vijavyo.


“Suala la uhai wa bonde la kilombero ni la lazima. Naagiza kwamba, katika kila kikao cha Halmashauri, ajenda ya kulinda uhai wa Bonde la Kilombero ni ya lazima na izingatiwe kwa ukamilifu,” amesisitiza Mhe. Malima.


Kiongozi huyo amebainisha kuwa, endapo hatua za haraka hazitachukuliwa kuzuia uharibifu wa vyanzo hivyo vya maji, baada ya miaka kadhaa bonde hilo litaathirika vibaya na kupoteza uhai wake kutokana na ukosefu wa maji.


Katika hatua nyingine Malima amesema, ili kufanikisha ajenda hiyo ya kulinda bonde hilo, Shirika la Umeme Tanzania -TANESCO lishirikiane na Maafisa Maendeleo ya jamii pamoja na Maafisa Mazingira ngazi ya Wilaya na Mkoa ili kutoa elimu kwa wananchi kuhusu njia bora za kutunza vyanzo vya maji na kuendeleza kilimo hifadhi (kilimo misitu) ambacho hakiharibu mazingira.


Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO Bw. Lazaro Twange, amesema shirika hilo linaendelea kutekeleza mikakati ya kufuatilia na kulinda vyanzo vya maji vinavyopeleka maji katika bwawa hilo huku akikiri kuwepo kwa changamoto za shughuli za kibinadamu katika maeneo yote ya vyanzo vya maji yanayoingia bwawani ndio maana wameanza kuchukua hatua za kudhibiti hali hiyo mapema.


Naye Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano na Huduma kwa Wateja wa Shirika la TANESCO, Bi. Irene Gowelle, amesema kikao hicho ni mwanzo tu wa utekelezaji wa yale waliyoyapanga kuyafanya na wana imani matokeo yatakuwa yenye mafanikio kwa sababu kikao hicho kimehusisha wadau wote muhim watakaoshirikiana nao katika kulinda vyanzo vya bwawa hilo la Julius Nyerere.


Ametaja mikakati iliyopo ni pamoja na kuwezesha zoezi la upimaji viwango vya maji vinavyoingia kwenye mabwawa ya umeme, kufukia mifereji isiyo na vibali vya kutumia maji, Kuendelea na upandaji wa miti rafiki kwa maji na Mazingira na kurudisha mito ya maji iliyopoteza mikondo yake.


Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • Morogoro kuanzisha jarida la programu ya PJT–MMMAM

    September 30, 2025
  • Viongozi wa Serikali Mkoani Morogoro watakiwa kulinda UHAI wa Bonde la Kilombero.

    September 26, 2025
  • Gairo kuanza kuhamasisha kilimo biashara.

    September 25, 2025
  • Gairo kuanza kuhamasisha kilimo biashara.

    September 25, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.