• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Morogoro kuanzisha jarida la programu ya PJT–MMMAM

Posted on: September 30th, 2025


Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro, Dkt. Mussa Ali Mussa, amewataka viongozi wanaotekeleza Programu Jumuishi ya Taifa ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (PJT–MMMAM) kuanzisha jarida maalumu litakalohifadhi na kusambaza taarifa za utekelezaji wa programu hiyo na kubainisha mafanikio na changamoto zake.

Dkt. Mussa ametoa ushauri huo leo Septemba 30, 2025 wakati wa kikao cha tathmini ya utekelezaji wa afua tano kuu za PJT–MMMAM, kilichofanyika ukumbi wa mikutano wa Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Morogoro na kubainisha kuwa jarida hilo litasaidia wananchi kuelewa kwa kina mchango wa programu hiyo katika kuboresha maisha ya watoto.

“Embu tuanzishe Morogoro Journal ya mradi huu, ili  kuelezana mafanikio na changamoto” ameshauri Dkt. Mussa.


Aidha, amesisitiza umuhimu wa kuwa na mfumo wa uandishi wa taarifa na ushirikiano wa karibu kati ya viongozi wa Serikali na wadau wengine wa maendeleo na vingozi kuacha kufanya kazi kwa mazoea bila kushirikiana, jambo linaloweza kudhoofisha kasi ya mafanikio ya programu.

“Ni lazima tushirikiane, tuache kufanya kazi kivyetu. Ushirikiano ndio utakaoleta matokeo chanya na kufanikisha malengo tuliyojiwekea,” amesema.


Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Shirika la Inlighten Development Organization (IDO), Bw. Benito Miwando, amesema Serikali imekuwa ikishirikiana kwa karibu na mashirika yasiyo ya kiserikali kuhakikisha utekelezaji wa programu hiyo unafanikiwa na kubainisha kuwa shirika lake limeendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa malezi bora na makuzi ya watoto, ili kuhakikisha jamii inakuwa na uelewa wa pamoja.

Naye Afisa Ustawi wa Jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Gairo, Bi. Joanita Mshasi, amesema halmashauri hiyo imeweka kipaumbele kwenye masuala ya lishe kwa watoto shuleni. Ameeleza kuwa chakula chenye virutubisho sahihi kimekuwa kikitolewa mashuleni ili kuhakikisha watoto wanakua vizuri kiakili na kimwili.


Afua zinazotekelezwa kupitia programu hiyo ni Lishe, Afya, Elimu, Ulinzi na Usalama pamoja na Malezi Yenye Mwitikio.


Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • Morogoro kuanzisha jarida la programu ya PJT–MMMAM

    September 30, 2025
  • Viongozi wa Serikali Mkoani Morogoro watakiwa kulinda UHAI wa Bonde la Kilombero.

    September 26, 2025
  • Gairo kuanza kuhamasisha kilimo biashara.

    September 25, 2025
  • Gairo kuanza kuhamasisha kilimo biashara.

    September 25, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.