• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Afisa Mtendaji wa Kata, Kijiji wapewa siku 4 kufuatilia watoto ambao hawajaripoti shule.

Posted on: January 17th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima ameiagiza serikali wilaya ya Morogoro kufuatilia wanafunzi 82 ambao hawajaripoti katika shule ya Sekondari Majimoto kutokana na sababu mbalimbali na kuwasilisha taarifa hiyo kwenye ofisi yake ndani ya siku nne.

Mhe. Malima ametoa agizo hilo januari 16, 2024 alipotembelea shule mpya ya Sekondari Majimoto iliyopo Tarafa ya Kisaki katika Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro ikiwa ni muendelezo Wa ziara yake ya kikazi ya kukagua miradi ya maendeleo na kusikiliza kero za wananchi.

Mh. Malima ametoa agizo hilo na kumtaka Afisa Tarafa ya Bwakila, Afisa Mtendaji  wa Kata ya Kisaki pamoja na Kijiji cha Kisaki Kituoni kufuatilia wanafunzi 82 ambao hawajaripoti kwa ajili ya kuanza kidato cha kwanza.

Mkuu huyo wa Mkoa amebainisha kuwa wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza 2024 katika shule hiyo ni 187 lakini hadi sasa walioripoti ni 105 hivyo amewataka Viongozi hao ngazi ya Tarafa, Kijiji na Kata kufuatilia sababu iliyopekea wanafunzi 82 kutoripoti shuleni hapo.

“...kwanza kuna watoto 82 hawajaripoti naondoka leo kisaki jumanne hadi kufika jumamosi lazima mniambie kwa majina na namba za simu...alafu DC utaniambia umewachukulia hatua gani...” amesema Mhe. Adam Malima.

Aidha, Mhe. Malima ametoa wiki mbili kwa uongozi wa shule hiyo kukamilisha ujenzi wa vyoo vya wanafunzi pamoja na ujenzi wa maabara hadi kufikia Mwezi Machi mwaka huu.

Katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa Mkoa amewataka viongozi hao kufanya utaratibu wa kuwahamisha wanafunzi wanaosoma mbali hususan wa kidato cha Pili na cha Tatu katika shule hiyo ya ya Sekondari Majimoto ili kuwapunguzia adha ya kutembea umbali mrefu.

Kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa shule ya Sekondari Majimoto Bw. Edmund John amesema wanafunzi waliochaguliwa kuanza masomo ya kidato cha kwanza 2024 ni 187 lakini hadi sasa wanafunzi walioripoti ni 105, hivyo wanaendelea kufanya jitihada za kubaini Watoto ambao bado hawajaripoti shuleni hapo.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.