• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

ALHAJI SENGULO AIHIMIZA JAMII KUTENDA MATENDO YA HURUMA

Posted on: July 11th, 2021

Alhaji Sengulo na dhana ya kusaidia wahitaji.

Jamii imeaswa kuwa na tabia ya kusaidia watu wenye uhitaji wakiwemo yatima, wajane na wazee ili kujipatia thawabu za mwenyezi Mungu na kujenga jamii inayosaidiana bila kubaguana wala kujali utofauti wa imani zao.

Nasaha hizo zimetolewa Julai 11 mwaka huu na Alhaji Hamis Sengulo wakati wa sherehe ya kwaya ya Mtakatifu Petro  na Paulo ya Kigango cha Kristu Mfalme kilichopo Parokia ya Mtakatifu Maria Modeco Jimbo katoliki la Morogoro.

Alhaji Sengulo akipokelewa na baadhi ya Viongozi wa Kwaya ya Mt. Petro na Paulo Modeko baada ya kualikwa kuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo

Alhaji Sengulo (kushoto) akipokea Risalaya wanakwaya wa Mt. Petro na Paulo kigango cha Kristo Mfalme. Kulia ni mama Mlezi wa kwaya hiyo. 

Alhaji Hamisi Sengulo (aliyevaa koti Jeusi) akishiriki kuimba kwaya pamoja na wanakwaya ya Mt. Petro na Paulo kigango cha Kristo Mfalme

Alhaji Sengulo ambaye licha ya kuwa yeye ni Muumini wa Dini ya Kiislamu amealikwa na wanakwaya wa Kigango hicho  kusherehekea sherehe za somo wao Petro na Paulo huku akishauri kuwa dini zote zina lengo moja la kumwabudu mungu na kuhubiri Amani na upendo kwa watu wake.

“Kila mtu anaabudu mwenyezi Mungu kwa staili yake lakini anamwabudu mwenyezi Mungu, uwe unamwabudu kupitia kanisani, kupitia msikitini lakini unafanya ibada, kwa hiyo ndugu zangu naomba tuwe wamoja” alisema Alhaji sengulo.

Wanakwaya ya Mt. Petro na Paulo wakiimba nyimbo za kumwabudu Munguwakati wa maadhimisho ya sherehe yao

Katika hatua nyingine Alhaji Sengulo ameitaka jamii kwa jumla  kudumisha Amani ndani ya nchi yetu ili kuwa na mazingira tulivu ya watu kuabudu na kujiletea maendeleo yao kwani bila amani hakuna Ibada wala maendeleo hivyo amewaasa viongozo wa madhehebu na dini zote kwa jumla waendelee kuwahimiza waumini wao jumuhimu wa Amani.

‘’Tudumishe sana Amani ya nchi yetu, kwa sababu bila Amani ibada hazifanyiki, kukiwa kuna vita kuna shida hata ibada hazifanyiki. Huwezi kufanya ibada msikitini wala Kanisani kama hamna Amani’’ alisisitiza Alhaji Sengulo.

Akiwa mgeni rasmi katika sherehe hizo, Alhaji Sengulo ameahidi kukarabati baadhi ya miundombinu ya kigango hicho ikiwemo ukarabati wa vyoo na kuunganishe nguvu zake na rafiki zake kwenye ujenzi wa nyumba ya mapadre katika kigango hicho kinachotarajiwa kuwa parokia hivi karibuni nyumba ambayo inahitaji zaidi ya Tsh. 100 Mil. hadi kukamilika kwake.

Kwa upande wake Katibu wa Kwaya ya Mtakatifu Petro na Paulo Ndugu Bertam Minde amemshukuru Alhaji Hamis Sengulo kwa kukubali kukarabati miundo mbinu ya kigango chao huku akiendelea kumuomba asichoke kusaidia Ujenzi unaoendelea wa nyumba ya Mapadre unaoendelea kujengwa katika kigango hicho.

Kwa upande wake Mama mlezi wa kwaya ya Mtakatifu Petro na Paulo amesema uongozi wao kwama viongozi wanaendelea kutafuta njia mbalimbali za kukijenga kigango hicho kwa kuwaomba marafiki ndugu na kjmaa zao huku akiwataka kupendana, kuvumiliana na kumtanguliza Mungu kwa kila jambo.

Alhaji akipokea Risala iliyosomwa kwake.

Awali akisoma risala kwa mgeni rasmi, Bi. Edina Gutapaka alibainisha changamoto mbalimbali zinazokabili Kigango cha Kristo Mfalme kuwa ni pamoja na ukosefu wa fedha za ujenzi wa nyumba ya paroko, Ukarabati wa Miundombinu ya Kigango hicho na ukosefu wa vyombo vya muziki kwa ajili ya kwaya hiyo.

 

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.