• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Bajeti ya TARURA Mkoani Morogoro yapaa Hadi TSH. bilioni 61.

Posted on: November 3rd, 2023

Bajeti ya TARURA Mkoani Morogoro yapaa hadi Tsh. bilioni 61.

Meneja wa Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini Tanzania (TARURA) Mkoa wa Morogoro Mhandisi Emmanuel Ndyamukama ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa  kuwaongezea fedha za utekelezaji wa miundombinu ya barabara Mkoani humo kutoka shilingi bilioni 7 hadi kufikia shilingi bilioni 61.

Mhandisi Ndyamukama ameyasema hayo Novemba 2, mwaka huu wakati wa mkutano wa Mkuu wa Mkoa pamoja na Msemaji Mkuu wa Serikali na Waandishi wa Habari ikiwa ni Kampeni ya kutangaza Mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Sita yaliyofanyika mkoani humo, mkutano  uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo.

Mhandisi Ndyamkama amesema wakati Serikali ya Awamu ya Sita inaingia Madarakani imekuta bajeti ya TARURA Mkoani humo ikiwa ni shilingi bilioni 7. 9 kwa mwaka, lakini kwa kipindi cha miaka miwili na nusu ya Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan bajeti hiyo imeongezeka hadi kufikia shilingi bilioni 61.45.

“...wakati Serikali ya Awamu ya Sita inaingia Madarakani tulikuwa tunapata mgao wa fedha shilingi bilioni 7. 9 kwa mwaka, lakini alivyoingia tu mpaka sasa hivi tumeweza kupata jumla ya shilingi bilioni 61.45...kwahiyo hii ni kazi kubwa ambayo Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameifanya...” amesema Mhandisi Ndyamukama.

Aidha, ameongeza kuwa fedha hizo zimesaidia kufungua barabara mpya zenye jumla ya km 190 ambazo zimeelekezwa kwenye huduma za jamii zikiwemo shule, hospitali, masoko, maeneo ya utalii, maeneo ya kuabudia na maeneo ya uzalishaji hususan kilimo.

Sambamba na hayo, Meneja wa TARURA amesema fedha hizo zimeongeza mtandao wa barabara za lami kutoka km 87.63 hadi km 99. 15, changarawe km 987.24 hadi km 1456.75, barabara za kiwango cha zege km 5.6, Madaraja mawaili likiwemo daraja la Berega lenye urefu wa mita 140 amabalo limegharimu shilingi bilioni 7.9 na daraja la Luhembe lenye mita 40 amabapo gharama yake ni shilingi bilioni 1. 2.

Nao wakurugenzi wa halmashauri za mkoa huo akiwemo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mlimba Mhandisi Stephano Kaliwa wamekiri uboreshaji wa miundombinu katika halmshauri zao huku akimshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassa kupitia TARURAna kwamba Halmashauri ya mlimba inatarajia kuchonga barabara ya Mlimba - Uchindile yenye km 80 ambayo itawasaidia kuondokana na adha ya kuzunguka kwenda Mafinga Wilyani Mufindi Mkoani Iringa kufuata huduma za Afya.

“Mhe. Rais amewasikia na amewafikia Wananchi wake”.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.