• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

BALOZI WA NORWAY, DENMARK WAZUNGUMZIA MAENDELEO YA MOROGORO.

Posted on: March 15th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima, Machi 15,2024 ametembelewa na Balozi wa Norway hapa nchini Mhe. Tone Tinnes Pamoja na mwakilishi wa Balozi wa Denmark Dkt. Mette Bech Pilgaard na kufanya mazungumzo kuhusu maendeleo ya Mkoa huo.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima kushoto akiagana na mwakilishi wa Balozi wa Denmark Dkt. Mette Bech {kulia} mara baada ya kumaliza mazungumzo.

Wakiwasili Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa nyakati tofauti, Balozi wa Norway hapa nchini Pamoja na kufika Ofisini hapo kusaini kitabu cha wageni, mefanya ziara ya kujionea utekelezaji wa miradi ya wadau wa SAGCOT inayotekelezwa mkoani humo Pamoja na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa ambaye ndiye mdau namba moja katika kuratibu uwekezaji wa Kilimo biashara na utuzaji wa mazingira.

Aidha, Balozi  huyo alifanya ziara ya kukagua miradi inayotekelezwa kwenye hifadhi ya Taifa ya milima ya Tao la mashariki, miradi ambayo inafadhiriwa na Ubalozi huo kwa lengo la kuongeza kipato kwa wananchi wanaozunguka milima hiyo ili kupunguza kasi ya uharibifu wa mazingira wa milima hiyo kupitia  kilimo na ukataji miti kwa lengo la kujipatia kipato.Mkuu wa Mkoa ameahidi kuendeleza Ushirikiano na SAGCOT ili kuleta mapinduzi ya kilimo hususan mazao ya viungo na matunda ndani ya Mkoa wa Morogoro.

Mkuu wa Mkoa ameahidi kuendeleza Ushirikiano na SAGCOT ili kuleta mapinduzi ya kilimo hususan mazao ya viungo na matunda ndani ya Mkoa wa Morogoro.

Baadhi ya wataalam wa Kilimo na biashara kutoka Sekretarieti ya Mkoa wa Morogoro wakati wa Mazungumzo ya Mkuu wa Mkoa na Mgeni wake. Kulia ni Dkt. Rozaria Rwegasira ambaye ni Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Uchumi na uzalishaji Mali

Kwa upande wake Mwakilishi wa Balozi wa Dermark Dkt. Mette Bech Pilgaard na Mwenyeji wake wamezungumzia Uhifadhi wa Mazingira katika Bonde la Mto Kilombero  Wilayani humo  pamoja na ukuaji wa Uchumi kwa wananchi wa Wilaya hiyo na Mkoa wa Morogoro kwa ujumla.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amemwambia Mwakilishi wa Balozi wa Denmark hapa nchini, nia ya Mkoa ya kurudisha uoto wa asili katika milima ya Uluguru, Udzungwa na milima mingine ndani ya Mkoa huo ambayo ni vyanzo vikuu vya maji yanayozalisha Umeme wa maji hapa nchini lakini pia maji hayo yanatumika katika kilimo cha mazao mbalimbali yakiwemo zao la mpunga Pamoja na zao la miwa ambalo linatoa sukari katika Viwanda vya Sukari vya Kilombero, Mtibwa na Mkulazi.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima (kushoto} akiwa na Balozi wa Norway Mhe. Tones Tinnes alipomtembelea Ofisini kwake

Kwa sababu hiyo Mkuu huyo wa MKoa amemwambia Dkt. Mett Bech Pilgaard kuwa Mkoa umeanzisha program ya kuwahamasisha wananchi kupanda mazao ya kimkakati ili kurudisha uoto wa asili kwenye milima hiyo ambayo pia itawaongezea kipato wananchi hao.

Kulia ni Balozi wa Norway hapa nchini Mhe. Tones Tinnes 

Ameyataja Mazao hayo kuwa ni Karafuu, Kakao, Michikichi, Kahawa na Parachichi, kwamba wananchi wakipanda mazao hayo katika milima hiyo itasaidia kutunza mazingira na kuondoa uharibifu wa mazingira unaojitokeza kila uchao hivyo kumuomba Balozi kusaidia programu hiyo.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.