• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Barabara ya Dodoma sasa kuwa ya njia Nne

Posted on: October 2nd, 2021

Barabara ya Morogoro - Dodoma kujengwa njia nne, nayo Mikumi – Ifakara yawekewa usimamizi wa karibu 

Serikali imesema iko katika hatua za awali za kujenga barabara ya kutoka Morogoro kwenda Jiji la Dodoma yenye urefu wa kilometa 267 kuwa barabara ya njia nne ili kurahisisaha usafiri na usafirishaji katika njia hiyo.

Kauli hiyo imetolewa Oktoba 2 mwaka huu na Msemaji Mkuu wa Serikali ndugu Gerson Msigwa wakati ikitoa taarifa ya wiki ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ikiwa ni utaratibu wake aliojiwekea wa kutoa taarifa hiyo kwa watanzania kila wiki.

Msemaji Mkuu wa Serikali Gerson msigwa akizungumza na waandishi wa habari wa Morogoro (hawapo pichani) wakati akitoa taarifa ya Serikali  katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Morogoro.

Msigwa amesema kwa sasa Serikali anamtafuta Mkandarasi mshauri ili kuanza hatua za awali za Upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara hiyo kwa ajili ya kuipanua ili kuwa na njia Nne yaani njia mbili kwa kila upande.

Akifafanua zaidi, Gerson Msigwa amesema malengo ya Serikali katika kupanua barabara hiyo, kwanza barabara hiyo ndiyo inayounganisha maeneo ya katikati ya nchi, lakini pia inaunganisha mikoa ya kanda ya ziwa na ukanda wa magharibi mwa nchi yetu, aidha amesema ndiyo kiunganishi kikuuu cha nchi ya Tanzania na nchi jirani za Uganda, Rwanda, Burundi na Kongo na kwamba ni muhim barabara hiyo ikaongezewa uwezo kwa kuwa inatumika kusafirisha mizigo inayokwenda katika nchi hizo jirani.

Katika hatua nyingine, Msemaji huyo wa Serikali amezungumzia ujenzi wa barabara ya  Mikumi - Kidatu – Ifakara yenye urefu wa Km 66.9 kutoka Kidatu – Ifakara, pamoja na ujenzi wa Daraja la Ruaha Mkuu kwa kiwango cha lami.

Baadhi ya viongozi wa Chama cha waandishi wa habari  Mkoa wa morogoro (Morogoro Press Club - MORO PC)  wakiwa katika picha ya pamoja na Msemaji Mkuu wa Serikali. kulia kwa Msemaji ni Mwenyekiti wa MORO - PC Nickson Mkilanya na kushoto kwake ni Katibu wa chama hicho Lilian Kasenene

Amesema, barabara ya Kidatu – Ifakara ni sehemu ya barabara kuu ya Mikumi - Kidatu - Ifakara - Mahenge/Lupiro – Malinyi – Kilosa kwa Mpepo – Londo – Lumecha yenye jumla ya urefu wa kilometa 547 amabayo inaunganisha Mikoa ya Morogoro na Ruvuma na kudai kuwa barabara hiyo itakuwa na msaada mkubwa kwa watanzania wote lakini zaidi sana kwa wakulima wa ukanda huo hususan wa Bonde la Mto Kilombero na Mkoa wa Morogoro kwa jumla.

“Mradi huu wa kujenga sehemu ya barabara kati ya Kidatu na Ifakara kwa kiwango cha lami na Daraja la Ruaha Mkuu ni sehemu ya Mkakati wa Taifa kusaidia wakulima Wakubwa na Wadogo kupitia Program ya Uendelezaji Kilimo katika Ukanda wa Kusini mwa Tanzania-SAGCOT, walioko katika Bonde la Mto Kilombero, ili kuyafikia masoko ya uhakika ya mazao yao kipindi chote cha mwaka”. Amesema Gerson Msigwa.

Waandishi wa Habari wa Mkoa wa Morogoro walioshiriki Mkutano wa Msemaji Mkuu wa Serikali Oktoba 2 mwaka huu wakiwa katika picha ya Pomoja na Kiongozi huyo mara baada ya Mkutano huo.

Hata hivyo amesema barabara hiyo imekuwa inasua sua kwa muda mrefu kwani amesema hadi  Julai 2021, Ujenzi wa Barabara hiyo ulikuwa umefikia asilimia 27 pekee ya Utekelezaji wake hali ambayo amesema Serikali haikufurahishwa hata kidogo na ucheleweshaji wa kukamilika kwa barabara hiyo.

Serikali baada ya kutambua  tatizo, imechukua hatuaza haraka, ikiwa ni pamoja na Wizara kuagiza Usimamizi wa Mradi huo sasa ufanywe na Wakala ya Barabara kupitia Idara ya Usimamizi wa Miradi, TANROADS Engineering Consulting Unit (TECU), baada ya muda wa mkataba wa Mhandisi Mshauri kukoma, Mwanzoni mwa Mwezi Agosti, 2021.

Afisa Habari, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Andrew Chimesela akiwa katika picha ya pamoja na Msemaji Mkuu wa Serikali na Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo hapa nchini Bw. Gerson Msigwa.

Serikali pia imemuonya Mkandarasi anayejenga barabara hiyo na kutakiwa kuongeza kasi ya ujenzi huo huku akiwekewa usimamizi wa karibu ili kukahikiasha kazi hiyo inakamilika mapema. Baada ya usimamizi huo kuchukuliwa na Wakala ya Barabara – TANROAD tayari mabadiliko yameanza kuonekana na kazi inakwenda kasi kwani hadi kufikia mwezi Septemba mwaka huu ujenzi huo umeshafikia  asilimia 37.5.

Mwenyekiti wa Morogoro Press Club Nickson Mkilanya akiteta jambo na Msemaji Mkuu wa Serikali 

Kazi ya ujenzi wa barabara ya Kidatu – Ifakara ulianza Oktoba 02,  2017, na muda wa Mkataba ulikuwa ni miezi 30, ambapo Mradi ulipaswa kukamilika tangu Aprili, 02, 2020 na Mkandarasi ameongezewa muda hadi tarehe 31 Oktoba, mwaka huu.

Ujenzi wa barabara hiyo unafadhiriwa na European Development Fund (EDF) kwa Ushirika na UKAID pamoja na USAID kwa gharama ya Euro 40,441,890.81 sawa na Shilingi za Kitanzania 120Bilioni.

kutoka kushoto ni Lilian Kasenene Katibu wa MORO PC na mwandishi wa gazeti la Mwananchi, Idda Mushi Mwandishi wa ITV na Redio One na Latifa Ganzel (Mhe. Diwani) na Mwandishi wa gazeti la Uhuru

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.